Mama wa kizungu amenitafuta tena na leo anataka kampani yangu

Nenda wakakugeuze nyama choma
 
Hata Znz sijawahi kufika ningekua wewe hata ushauri nisingeomba. Zingeanza post na signature ya 'Signed in Bulgaria'
 
Hizi bahati huwa hazitokei mara mbili wengine tunazisaka kila siku hazisanuki,wewe unapata chance la life mbwelambwela unakenua meno humu JF.
 
Nchi iliyowahi kuwa Yugoslavia na baadhi ya Soviet block hunipeleki. Kwanza kule wabaguzi sana, ukienda naye akafa unaanza kuzibua vyoo sijui. Na hakuna pesa kivile.
 
Uende na vilainishi vyote unavyovijua hapa town pumbav
 
Kijana nenda watu wa huko wakarimu sana kuna demu nilikutana naye kwenye fb amenisaidia sana sana Kuhusu maswala ya kufundisha kwenye kaproject kangu

Hapa bongo ajira hazisomeki wala elimu ukimaliza chuo kama wewe huna connection utakipata cha moto moto tu

Go go achana na wabongo Mkuu
Hawawezi kukua kiboya boya huku taarifa zako zote zitakuwepo huko nenda kapambane Mkuu
 
Comment za humu zimesababisha nipate interpersonal conflict
Kwenda nataka but naogopa.
 
Ushamsilkia Dr.Shika, mtafute akakupe ushauri

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nenda ila angalià usije kuwa her success ladder.... Hapo kuna mawili either zali la mentali kama baadhi wanavyokuambia au umechezewa ule mchezo wa kurushia kuku mahindi ili ajilete ndani....Hongera...,Shauri yako.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…