acha ujinga nenda kwa gyno haraka, hasa hilo la kutoka damu wakati mja mzito sio dalili nzuri, anaweza poteza ujauzito huo.
Japo kuna baadhi ya wanawake wachache ambao hupata hedhi hadi miezi 5 au 6 ya ujauzito.
Kuhusu kuota anafanya mapenzi na watu tofauti inaweza tokana na wewe kushindwa kumkuna kisawa sawa sababu jogoo wako hawiki. Sambamba na jogoo wako kutowika, kuna baadhi ya wanawake hamu ya ngono huongezeka maradufu wakati wa ujauzito au akishajifungua. Inawezekana hivyo vyote viwili vinapelekea mke kuwaza ngono muda mwingi mwishowe anaota.
Ukishaenda hospitali, uchanganye na sala utafanikiwa. Hata tunapokuwa waumini wazuri tutumie na akili za hospitali hata hao madaktari wanatimiza mipango ya Mungu.
Wewe kaka kuhusu jogoo kutokuwika, inawezekana umejijaza hofu ya majini mahaba, hedhi ya mkeo na mimba, utawikaje sasa?