Mama'ake anapodandia bili ya mwanawe!

Mama'ake anapodandia bili ya mwanawe!

Akiugua kadi ya bima inampeleka hospitali, risiti ya shule inampandisha daladala au gari la shule, akiwa na njaa anajilisha mwenyewe, nguo zikichafuka zinajifua zenyewe, ankiwa na njaa mchele, unga, mayai, n.k. ulivyopeleka vinajipika vyenyewe. Kwani Kutompa pesa ndio mnaona manafaidi sana? Mtoto akikuwa atasimuliwa na mama yake. ATAWACHUKIA TU.

sasa mtu ameolewa na maisha yake tumfanyeje? akiumwa ndio tunampeleka hospital, akitaka tumpikie we will do that, ni vile ye mwenyewe kakatalia, unasema atatuchukia?? imagine huwa we are praying yasijetokea, coz mwisho wa cku she is our blood! na ameolewa na mdhungu, but the guy yupo so strictly kwamba matumizi yamtoto yapelekwe home and not money, mkewe atahudumia mwenyewe. HATAKI KABISA KUSIKIA AMETUMIWA PESA!
 
ruta kwa kuona hoja yako ya laki saba imepigwa chini na strong woman wa jf umeamua wazi kumsingizia mwanamke mwenzetu kwa kudai hiyo 2.1 milion si ndio eeeh!!.kama ww ni mmoja wa mawaziri waliotemwa na jk hata sion tabu kudai hiyo pesa ati.
 
dah resonable unayoitaka ww umeshajibiwa na lizzy.kama unataka mtoto alelewe kwa matabara ya kufua na kuanika ,kwa unga wa dona kama toto yenu sio gojwa gojwa hapo naweza kusema kwamba walau chenchi itabaki kidogo.

Nina kaka angu ameachana na mke wake anatoa hiyo laki saba kila mwenzi na bado mtoto akiumwa gharama juu yake na kumchukua mtoto haiwezekani causemtoto bado mdogo upo hapo kijana.

ummu kulthum angalau huyo wa akaka yako alikuwa ni mke huyu siye ni mtu baki tu ambaye tulifanya maamuzi fulani miaka michache iliyopita....................sasa kaja juu hataki utani.....lol
 
Last edited by a moderator:
Kaunga umenitia kitanzini......nikijibu haya maswali niakuwa nimejimaliza........................kwa kifupi tu bila ya kumwaga mtama kwenye kuku wengi................maana hata yeye ni mwana JF...............kwa hiyo asije akajua udhaifu wangu a akautumia dhidi yangu ni kuwa...................I have a name to protect..........sleaze publicity will hurt my name........

Pole in that case, blackmailing ni saizi yake; she knows how to play her cards well!

Ni ndege mjanja kanaswa kwenye tundu bovu! Ila kwa mnavyotutenda, bora wengine watulipizie kidogo! LOL
 
Last edited by a moderator:
Huyo mtoto wa maige....baba anajikamua kutoka laki saba na wewe unatumia kama zilivyo jamani na bado unataka zaidi....mwalimu anaishi na mtoto,mume na mdogo wake kwa laki na nusu na mtoto ana survive fresh....uko ni kukomoana...kwanza ni bahati kapata baba responsible hata baada ya ndoa kuisha mahakamani na kugawana vitu..

Ilitakiwa baada ya kugawana na bwana anasepa uone kama mtoto atakufa na njaaa....kukuta mwanaume responsible kama ruta....few in milion....wengine wameolewa na waume zao wana pesa lakini laki tatu kuona live ni ngumu...sebuse waishi mbali kudeka tu.

[MENTION]Buswelo[/MENTION].....................u are very wise wawe na hata wanajua kusema asante kwa yote yale tuliyowafanyia badala ya kuona huu sasa umekuwa mradi wa kivuno cha bei poa..........
 
Ukute anakulipisha na uchakavu ('depreciation') uliomsababishia kwa kumzalisha. Kwa wengine kuzaa kunawachakaza kweli!

na huyo anayeishi naye mbona hambandiki hizo gharama za kuchakaa....................hivi ni nani humchakaza mwenzio.................mimi naona ndiye niliachwa nyan'ganyan'ga
 
JOJEETA....................mzazi mwenzangu anadai kuwa anataka kum'mwaga yule jamaa yake anirudie...lakini mimi sitaki kwa sababu naona hiyo ni vurugu........mtu akishaishia ni vyema aishie jumla.....................nikila matapishi yangu tena..........hata ardhi italaaniwa..........

haya kaka ruta nimekusoma.pole kwa matatizo,matatizo ni sehemu mojawapo ya maisha,hope u wil handle it.goodluk
 
Rutashubanyuma ushauri wangu kwako ni kumuuliza listi nzima ya mahitaji ya mtoto na ujitoe mazima kununua each and everything mwenyewe kwani unalipia na shelter?
Kama hiyo ikishindikana omba ushauri kwa lawyer wako, uone hatua gani za kisheria unaweza kuchukua.
Hivi wanaume hawako protected kwenye mambo haya?

lemonade huo muda uko wapi...........na isitoshe tuna makubaliano ambayo kila mwezi anatumiwa tatizo anadai hazitoshi ataka mara tatu yake......................
 
Last edited by a moderator:
Heri sisi wa zamani
Haya ya kwenu jamani
yanatisha si utani
Laki saba mfukoni
Eti yafaa nini,
Hamna huruma jamani?

Ziwe ngapi ziwatoshe,
kulea mwana mmoja,
Tena msizikwepeshe,
Na hawara mkafuja,
Mkaja zua kasheshe
siku kunena kwa mja.

Pole Rutashubanyuma,
Kwani Lizy naye mama,
Atatetea hujuma,
Hata kama linazama,
Hao wana chao chama,
Kuhujumu kina baba.

Kigarama it is tough being a man of substance and means......................
 
Last edited by a moderator:
lemonade huo muda uko wapi...........na isitoshe tuna makubaliano ambayo kila mwezi anatumiwa tatizo anadai hazitoshi ataka mara tatu yake......................

Kwakuwa unataka kuprotect jina lako inabidi uwe kondoo tu, labda ujaribu kurenagotiate.
Otherwise tazama jinsi ya kutumia intelejensia kwakuwa inaonekana wewe ni "mtu fulani" so utakuwa na maujanja ya kumbana
 
Last edited by a moderator:
Kwakuwa unataka kuprotect jina lako inabidi uwe kondoo tu, labda ujaribu kurenagotiate.
Otherwise tazama jinsi ya kutumia intelejensia kwakuwa inaonekana wewe ni "mtu fulani" so utakuwa na maujanja ya kumbana
[MENTION]
Lemonade[/MENTION] nakushukuru sana kwa ushauri wako mzuri.......................nitauzingatia.
 
Haika..........mie siyo hit and run hata chembe kila kitu kilikusudiwa ni mtu baadaye kunibadilishia somo kinyume na makubaliano yetu ya awali...............ninajilaumu kwanini sikuyaandika...........

Haswaaaaa, Makubalioano hayo hayo ndio niliataka kuongelea, siku hizi wasichana wachache sana wa umri wa over 20 wanaweza kujishtukia wana mimba bila kuua na kushindwa kufanya maamuzi ya kibinafsi zaidi.
Hivyo huo wa kwenu nahisi ulikuwa ni uamuzi wa watu wawili wazima, wenye utashi (uliokufa kwa muda) mkaamua kufanya mlilofanya.
Lakini kwa kuwa maamuzi yenu hayakusimama kwenye kweli, hayo ndio matokeo yake.
Kwa kawaida, maisha tangu vizazi vingi kiasi vilivyopita, mtoto anatakiwa azaliwe kwenye mazingira ya familia yenye baba mwanaume na mama mwanamke, wenye misimamo thabiti ya familia, hawajui kila kitu, lakini wamechagua kumsaidia Mungu na ulimwengu, kuongeza kizazi cha binaadamu, na kulea mtu ambaye atakuwa tegemeo la viumbe.
Shorkcut zilizopo siku hizi, hakuna wa kuzicontrol, ila ni wewe na utashi wako,
Na ujue sheria ya mungu ilvyo ya ajabu, kwa mtazamo wa kawaida, ni ngumu, ila kwa undani ni rahisi na shortcut kuliko zingine zote.
Hapa sisemei Dini,
Mtu yoyote akifuata utashi wake wa ndani, bila kuwa mnafiki, mbinafsi, huwezi kufanya maamuzi kama hayo. Kamwe!!!
Ila kwa udhaifu wetu, mara kwa mara tunarudia makosa yale yale.
Makovu lazima yawe machoni mwako, lazima ujifunze kuishi na matokeo ya makosa yako.
Yeye, dada, sitaki kumgusia, sitaki kuficha makosa yako kwa ajili ya makosa ya mtu mwingine, asingekuwa yeye angekuwa mwiningine, ila wewe uko hapa. Next time nadhani utaamua vingine, na pia wadogo zako, sidhani kama unaweza kuwashauri kuwa its okay kufanya maamuzi kama yako. (that is a good thing to the future generation)
 
Kazi nzuri tuliifanya mimi na maama'ake
Matunda yake si khaba na mwana tukajaliwa
Ndoa kati yetu tuliiogopa kwani ni ndoana
Mwafaka ukafikiwa wa mgawanyo wa majukumu
Lakini matunzo ni ya mtoto na mama'ake atoka wapi?

Mie jukumu langu lawa ni kubeba gharama
Mzazi mwenzangu kazi yake ni malezi tu..
Baada ya kipindi mwenzangu somo kageuza!
Akidai bila kumbeba na yeye malezi hayawezekani!
Lakini matunzo ni ya mtoto na mama'ake atoka wapi?

Bili ya mtoto yabebeka lakini kero za mama'ake zatisha!
Kwani mtoto hana makuu lakini mama'ake ataka mengi!
Mtoto yeye ni wa kulamba celerac lakini ya mama'ake!
Mama'ake ataka atunzwe akidai bila yeye hakuna malezi!
Lakini matunzo ni ya mtoto na mama'ake atoka wapi?

Baada ya purukushani na kasheshe kibao sasa..
Siri sasa yafichuka na mama'ake kashindwa uteja!
Kumbe mwenzangu ana dongo aona kadhulumiwa!
Anipasha khabari kuwa mtoto ni wa kwangu tu!
Lakini matunzo ni ya mtoto na mama'ake atoka wapi?

Mama'ake apasua jipu kuwa jasho langu ni lake pia!
Adai kama tumeweza kuzaa kwanini tusile wote?
Mie simwelewi kwani mwafaka tuliweka sote.
Yawaje sasa anigeuzie kibao bila ya sababu?
Lakini matunzo ni ya mtoto na mama'ake atoka wapi?


Mpangie mwana chumba, ajitenge na mamaye,
hadi apate mchumba, hapa si wewe ni yeye,
tajitenga na ushamba, ka meno na kiseyeye,
VYA MLEVI VISHALIWA, MGEMA ATAPATAPA.

tashibisha vya mlevi, tumbole kuning'inia,
wala huu si uchimvi, wahenga wanatambua,
ngadu wala sii mwivi, mwendowe tu sio nia,
VYA MLEVI VISHALIWA, MGEMA ATAPATAPA.

Mgema atapatapa, zamu imemuwadia,
eti harufu ya papa, ndio anasingizia?
kitaa anajitapa, kama jaji rugazia!
VYA MLEVI VISHALIWA, MGEMA ANATAPATAPA.

kakongorokea mediko, kaponzewa na mwanao!
simchumie viboko, akageuka kideo,
ambebe kwa mbeleko, kama mbege kwa kileo.
VYA MLEVI VISHALIWA, MGEMA ANATAPATAPA.

Kaditama wa aama! sumari nagongomeka,
mwanao kwake mama, utumbo umeungika,
takulaje vya shirima, mwanao macho tumbuka?
KUZIZOA SIFA KWA MWANA, MTUNZE NA MAMAYE. Rutashubanyuma
 
Last edited by a moderator:
lemonade huo muda uko wapi...........na isitoshe tuna makubaliano ambayo kila mwezi anatumiwa tatizo anadai hazitoshi ataka mara tatu yake......................

Mkuu mbona wapata shida na kuianika akili yako kirahisi hivi, gharama ya upendo mmejaaliwa MTOTO, Hasara ya chuki timiza wajibu mchungu. hatuung'oi mwiba kwa kuushindilia utokee upande wa pili wa mguu!
 
Last edited by a moderator:
Pole in that case, blackmailing ni saizi yake; she knows how to play her cards well!

Ni ndege mjanja kanaswa kwenye tundu bovu! Ila kwa mnavyotutenda, bora wengine watulipizie kidogo! LOL

Kaunga kisasi siyo chako hata siku moja..........Mwachie Muumba
 
Last edited by a moderator:
Mkuu mbona wapata shida na kuianika akili yako kirahisi hivi, gharama ya upendo mmejaaliwa MTOTO, Hasara ya chuki timiza wajibu mchungu. hatuung'oi mwiba kwa kuushindilia utokee upande wa pili wa mguu!

jogi mawzo mazuri sana....................lakini msumari unapong'ang'ania mguuni unaufanyaje?
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom