Mambo 10 yaliyopo Ulaya, hasa hasa Sweden, pengine kwako ni mageni, na ungependa kuyafahamu

Mambo 10 yaliyopo Ulaya, hasa hasa Sweden, pengine kwako ni mageni, na ungependa kuyafahamu

Uwe na sababu za kufika kwanza. Sababu zipo nyingi. Masomo, tourist, kikazi, biashara n.k. Katika hizo sababu unaweza ipi?

Hapo ni kuja kibiashara kwanza kuchukua vitu used vya huko kama tv, fridge, na kadhalika unakuja bongo kupiga pesa tu maana bongo hata vyombo vya ndani used twende kazi tena ukitangaza umetoa ulaya vinaisha haraka sana
 
Uwe na sababu za kufika kwanza. Sababu zipo nyingi. Masomo, tourist, kikazi, biashara n.k. Katika hizo sababu unaweza ipi?
Kwenda tuul kutafuta maisha.
Ujue vijana wengi hatujui tunataka kwenda nje kutafuta Nini.
Yaani mtu atajua huko huko ili mradi katoka
 
Hapo ni kuja kibiashara kwanza kuchukua vitu used vya huko kama tv, fridge, na kadhalika unakuja bongo kupiga pesa tu maana bongo hata vyombo vya ndani used twende kazi tena ukitangaza umetoa ulaya vinaisha haraka sana
Hii aina ya baishara inabidi utafiti wa muda. Kubaini aina ya bidhaa specifically na uingizwaji wake ndani ya nchi. Namanisha masuala ya kodi n.k Mfano, nimwahi kufatilia kuhusu biashara ya used furniture, niliponda TRA nikagundua unaweza kupata hasara, maana sera ya kodi kwa furniture kwa mtizamo wangu ni kama inalinda bidhaa za ndani hivyo kodi yake nikaona ni kubwa. Kingine, hizi bidhaa used siyo kwamba utazitukua sehemu moja kwa kiwango unachotaka. Inaweza kukuchukuwa muda mrefu kukusanya mzigo wa kutosha maana inakubidi kukusanya kimoja kimoja kulingana na upatikanaji wake huko kwenye maduka used.
 
Hii aina ya baishara inabidi utafiti wa muda. Kubaini aina ya bidhaa specifically na uingizwaji wake ndani ya nchi. Namanisha masuala ya kodi n.k Mfano, nimwahi kufatilia kuhusu biashara ya used furniture, niliponda TRA nikagundua unaweza kupata hasara, maana sera ya kodi kwa furniture kwa mtizamo wangu ni kama inalinda bidhaa za ndani hivyo kodi yake nikaona ni kubwa. Kingine, hizi bidhaa used siyo kwamba utazitukua sehemu moja kwa kiwango unachotaka. Inaweza kukuchukuwa muda mrefu kukusanya mzigo wa kutosha maana inakubidi kukusanya kimoja kimoja kulingana na upatikanaji wake huko kwenye maduka used.

Machine machine used unaweza ukapiga bingo kikubwa kama usemavo utafiti uwe wa kutosha kabisa
 
Waliojanjaruka mapema walisafiri hadi uholanzi kuchukua baiskeli used kwa sasa wako mbali sisi tukua tunategemea mzee wetu magu atuvushe
 
Kwenda tuul kutafuta maisha.
Ujue vijana wengi hatujui tunataka kwenda nje kutafuta Nini.
Yaani mtu atajua huko huko ili mradi katoka
Kutokana na sera ya uhamiaji siku hizi, hali imebadilika Ulaya siyo kama zamani. Wenyeji wanaona kuna kipindi serikali zao ziliruhusu wahamiaji kwa kiwango kikubwa na madhara yake yameanza kujitokeza. Mafano, matukio mengi kuhusu criminal issues zinachangiwa sana na wahamiaji. Sisi watu wa kuja tunakuja na tamaduni zetu na kuharibu ustaarabu wa wnzetu na kusababisha shida. Kwahiyo uzamiaji kwa sasa si rahisi sana. Ila nisikukatishe tamaa. Kila jambo chini ya jua linawezekana. Kama unataka kutafuta maisha, nakushauri ujaribu ku-focus Uingireza, huko hutapata taabu ya lugha na kazi za vibarua ni nyingi zaidi. Huku kwingine kama Sweden utapata shida mpaka kwanza ujifunze lugha. KJazi za kuzungumza English ni chache. Wakazi wanazungumza English vizuri kabisa, ila wanalinda sana tamaduni zao including language.
 
Kutokana na sera ya uhamiaji siku hizi, hali imebadilika Ulaya siyo kama zamani. Wenyeji wanaona kuna kipindi serikali zao ziliruhusu wahamiaji kwa kiwango kikubwa na madhara yake yameanza kujitokeza. Mafano, matukio mengi kuhusu criminal issues zinachangiwa sana na wahamiaji. Sisi watu wa kuja tunakuja na tamaduni zetu na kuharibu ustaarabu wa wnzetu na kusababisha shida. Kwahiyo uzamiaji kwa sasa si rahisi sana. Ila nisikukatishe tamaa. Kila jambo chini ya jua linawezekana. Kama unataka kutafuta maisha, nakushauri ujaribu ku-focus Uingireza, huko hutapata taabu ya lugha na kazi za vibarua ni nyingi zaidi. Huku kwingine kama Sweden utapata shida mpaka kwanza ujifunze lugha. KJazi za kuzungumza English ni chache. Wakazi wanazungumza English vizuri kabisa, ila wanalinda sana tamaduni zao including language.
Mpe connection ya jimama moja lugha atamfundisha huyohuyo.

Halafu zile mchongo za Au pair siku hizi Sweden hazipo?
 
Wakuu, heshima kwenu.!

Kama ilivyo ada, JF ni kisima cha habari, stories, ucheshi na mengineyo. Ili kuifanya JF iendelee kuwa kisima cha taarifa, naomba nami leo ku-share mawili matatu kuhusu mada tajwa hapo juu.

1) Kwa muda wote niliopo huku, miaka mitatu sasa, nimesafiri na kutembea maeneo mbalimbali. Safari za muda mrefu na fupi. Kwakweli sijawahi kushuhudia ajali ya barabarani. Simanishi kuwa ajali hazipo kabisa, ila ni kwa kiwango kidogo sana. Kwa mujibu wa utafiti wangu mfupi usio rasmi, nimegundua hii inatokana na sababu zifuatazo,

i) Leseni za udereva zinatolewa kwa njia ambayo ipo high secured. Yaani hata kama una leseni ya bongo, na una experience ya kuendesha kwa miaka 10, lazima ufanyiwe majaribio kabla ya kupewa leseni ya huku. Endapo utakosea hata kosa moja tu wakati wa majaribio, mfano kuchelewa kuwasha indicator kabla ya kukata kona, au ukaendesha gari huku umeegesha mkono dirishani kama ifanyikavyo bongo, hakika hautapewa leseni na inabidi urudie tena majaribio. Aidha, leseni mpya zinatolewa kwa mafunzo ambayo lazima uwe very compentent. Kwa ufupi wakuu ni kwamba, leseni hazitolewi kama njugu.

ii) Ikibainika umeendesha gari huku umekunywa pombe kwa kiasi kisichoruhusiwa, fine yake inaweza kukaribia nusu ya kipato chako cha mwezi. Kuna baadhi ya magari, hususan magari ya makampuni, ili uweze kuliendesha, lazima ufanye test ya kucheki kama umekunywa pombe. Usipofanya hiyo test ambayo ipo kwenye mfumo wa gari, hiyo gari haitoondoka wala kuwaka.

iii) Magari yote yanayotembea barabarani lazima yakaguliwe kila mwaka ili kujua kama bado yanakidhi vigezo vya kuwa barabarani.

iv) Njia nyingi hasa high way, ni one-way. Hizi ni barabara hasa zinazotoka mji mmoja kwenda mwingine. Baadhi ya miji, hata barabara za ndani zina mfumo huu. Yaani magari yanayoenda upande mmoja hayakutani na yanayokuja upande mwingine. Madereva wanafahamu nachomaanisha.

v) Barabara zina standard kiwango cha juu. Yaani ikitokea uharibifu tu mahala, haraka sana inafanyiwa marekebisho.

2) Kwa muda wa miaka mitatu sasa, tangu niwepo huku (Sweden na Uholanzi), hakuna hata sekunde moja ambapo umeme na maji vimekatika. Hebu imagine huko Kilosa, Ileje, Nyapande, Nkasi, Ludewa, Liwale, Ngara, Uvinza, Makete kuwe na access ya umeme na maji ndani ya nyumba 24 hours/7 days. Maisha yangekuwaje? Raha si raha? Ha ha haa.!

3) Intrnent ni huduma muhimu kwa kila nyumba kama ilivyo umeme na maji. Namanisha kuwa, kila nyumba imeungunishiwa mfumo wa kupata internet.

4) Huduma za Elimu na Afya kwa Sweden ni bure. Elimu kwa Uholanzi unalipia kidogo, ila siyo gharama kubwa kivile.

5) Sweden ukiwa mgonjwa ukapelekwa hosp unapatiwa na huduma ya chakula. Ni bure, haulipii. Muhimu uwe mkazi au raia. Pesa zinatoka kwenye Tax unayolipa. Hapa ndipo kuna hoja kwamba, wanalipa Tax kubwa, mfano kwenye mji ambao huwa naishi, Tax ni almost 30% ya kipato chako.

5) Shughuli zote zimewekwa kwenye mfumo rasmi chini ya makampuni. Kwa ufupi hakuna eti ile kusema hii kazi i.e anapewa fundi locally na kuanza kujenga kwa kuwatafuta vibarua mtaani kienyeji. Namanisha kuwa, kila kazi, iwe ni kupanda maua, kupaka rangi, usafi, kusafisha vioo kwenye majumba n.k zipo kwenye mfumo rasmi. Na kila anayefanya kazi anaajiriwa katika mfumo rasmi. Nadhani hii njia inafanya hizi nchi za wenzetu kila mtu kuhakikisha analipa kodi.

6) Kila anayeajiriwa, hata iwe non-professional job, kwa kiasi kikubwa, mshahara anaolipwa mtu unamwezesha kukidhi maisha katika standard ya kawaida. Yaani anaweza kula chakula, kulipia rent, usafiri, n.k kwa mwezi mzima na akabakisha chenji kidogo. Nasisitiza kuwa ni kwa kiasi kikubwa, kulingana na uexperience niliyonayo. Huenda kuna baadhi ya kazi (zitakuwa chache sana) mtu anaweeza kulipwa below the standard. Wenzetu wana standard za mishahara kwa nchi nzima. Siyo kila mtu kujipangia tu.

7) Train na mabasi ya Public ndani na nje ya mji yana ratiba zinazofahamika. Mfano, kila baada ya robo saa gari inapita kwenye kituo. Kuwe na abiria ama hakuna abiria muda ukifika basi lazima liondoke/kusafiri kama ilivyopangwa. Hii ni kwa sababu, Serikali ina- provide subsdy kwenye sekta za usafiri. Kwahiyo kama kampuni itapata hasara, serikali inafanya ku-top up ili sekta hiyo iendelee ku-survive.

8) Hakuna masuala ya mfanyakazi wa ndani kumuangalia mtoto ama mtu mzee kama bongo. Hii ni kwa sababu, mama akijifungua, mama anapewa maternity leave na baba anapewa partenity leave ambapo kwa ujumla wake vikichanganywa inafikia mwaka mmoja. Hivyo mtoto atalelewa na wazazi mpaka afikishe mwaka mmoja. Baada ya hapo anapelekwa kwenye baby care center ambako anapelekwa asubuhi na kuchulkuliwa mchana. Kwa Wazee, akishafikisha umri wa kutojiweza, anapelekwa kuhudumiwa kwenye community center ambako pension yake itatumika kumuhudumia.

9) Kiwango cha ukosefu wa ajira ni kiasi kidogo sana. Yaani si rahisi kukuta mkazi yupo home muda mrefu bila kazi yoyote. Sisemi kuwa hakuna wasiokuwa na ajira, ila ni kwa kiasi kidogo sana. Suala la gharama za maisha ni jukumu la baba na mama. Sio kama sisi eti kazi ya kutafuta mahitaji ni suala la baba peke yake. Huku suala la usawa linafanyika kwa vitendo. Hii mada ya usawa nitaijadili siku nyingine.

10) Pamoja na kodi kubwa wanayokatwa (atleast 30%), ila jamaa wanafaidi sana kodi yao. Yaani unakuta Serikali inampatia mzazi kiasi flani cha pesa kwa ajili ya huduma ya mtoto anapozaliwa mpaka anapokuwa mkubwa. Ha ha haa. Kwa lugha fupi ni kuwa, kila mtoto analipwa kiasi flani cha pesa mpaka afikishe umri mkubwa. Siyo kiasi kikubwa, ila kinamwezesha kuishi.

Kwa leo naomba niishiea hapa. Leo nimezungumzia upande wa +ve side, siku nyingine nitazungumzia -ve side pia. Haya niliyosema simanishi kuwa nchi za Ulaya wanaishi kama Mbinguni, na kwenyewe kuna shida zake nyingi tu.

Kama kuna mahala nimeteleza kidogo, basi ni sahihi kukosolewa na kurekebisha jambo ambalo naweza kuwa nime-overlook. Ila nilichokisema kina uhalisia mkubwa zaidi ya 90% maana ni mambo niliyoyaona na kusimuliwa.

NB: Siasa za huku kwa kiasi kikubwa, zimejikita kwenye sera za kupunguza wahamiaji ( Yaani malalamiko kuwa wahamiaji ni wengi yamekuwa makubwa sana miongoni mwa raia). Siasa nyingine zimejikitia kwenye masuala ya mabadilkiko ya Tabia ya nchi (Climate change). Yaani sisi Afrika tukiwa tunataka labda kuandamana kwa ajili ya kupatiwa huduma za msingi za maisha, huku wenzetu wameanza kuandamana kushinikiza Serikali zao zichukuwe hatua dhidi ya Mabadiliko ya Tabia ya Nchi . Naomba hii iwe mada ya siku nyingine pia.

Ahsanteni.
Mambo ya ulimwengu uliostaarabika
 
Bongo maisha hayo wanaishi viongozi na familia zao pamoja na kikundi cha wateule wachache huku wananchi wanaolalamika wanaishia kuwauwa, kutekwa na wasiojulikana,kukashifiwa kwa matusi na masimango ya kila aina lakini cha ajabu wengine ndio wanawasifu hao watesi wao na kutaka wawe watawala wa milele na kudai hivyo ndivyo inavyostahili kuongoza Wabongo na kwamba eti Mbongo ukimchekea mambo hayaendi!
 
Sweden hawaruhusu kusafirisha fridge kwa sababu fridge nyingi za zamani zinatumia gas inayoitwa refrigrant R 116 ambayo inaharibu mazingira.Na wao kama Serikali hawaoni ni sawa morally kuziruhusu na kupeleka tatizo kwingine duniani. Fridge mpya zinatumia gas inayoitwa isubotane.Hizi ni ruhsa kusafirisha.
Kuhusu mambo mengine aliyosema mleta mada karibu yote ameelezea ukweli.Isipokuwa mishahara inasimamiwa na mkataba unaoitwa kollektivavtal. Mkataba huu unasimamia mishahara ya sekta zote hata binafsi ili kulinda wafanyakazi wasipunjwe na kupewa mishahara isiyokidhi mahitaji ya mfanyakazi.Kila sekta ipo huru kutoa mishahara zaidi ya mkataba lakini sio pungufu.
Kila mwaka waajiri wanakutana na wafanyakazi wao katika kikao kinachoitwa medarbetare samtal ili kuzungumzia ajira yao na kuongeza mishahara kutokana na wajibu wao kazini.Kuhusu lugha inafundishika kama nia ipo.Ukiwa na bidii ndani ya miezi 6 unakuwa umejifunza svenska(lugha ya kiswidish) kwa kiwango cha kueleweka.
 
Hamna lolote. Simulizi za kawaida za Watanzsnia Wasafisha vyoo mchana na Wasambazaji magazeti nyumba hadi nyumba asubuhi saa 9 usiku kila siku. Wameridhika na maisha ya milele ya kuwa vijakazi wa Wazungu.
 
Hamna lolote. Simulizi za kawaida za Watanzsnia Wasafisha vyoo mchana na Wasambazaji magazeti nyumba hadi nyumba asubuhi saa 9 usiku kila siku. Wameridhika na maisha ya milele ya kuwa vijakazi wa Wazungu.
Well kati ya hao wasafisha vyoo ulaya na wanapata kipato na kuishi kama binadamu anavyotakiwa kuishi, na hawa waliojichokea Bongo mpaka uchawa imekuwa ajira bora nani?

Ujuwe nilikuwa nakuonaga kama mtu muelewa na mwenye exposure kubwa kumbe sivyo,

Kwahiyo unataka kila mtu awe mwizi kama wewe mpaka viwango vya kusakwa na FBI?

Taarifa zako tunazo mtumishi, acha dharau.
 
Hamna lolote. Simulizi za kawaida za Watanzsnia Wasafisha vyoo mchana na Wasambazaji magazeti nyumba hadi nyumba asubuhi saa 9 usiku kila siku. Wameridhika na maisha ya milele ya kuwa vijakazi wa Wazungu.
Bora huko huo mshahara naweza kulisha familia na kutuma hela huku tz kwa ndugu na jamaa zake..niambie huyo msafisha choo wa tz ana maisha gani?

Tanzania ni nchi ya laana kuanzia viongozi wake.

#MaendeleoHayanaChama

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nchi yetu wenyewe hatujamaliza tunaanza kushobokea mambo ya sweden.
 
Well kati ya hao wasafisha vyoo ulaya na wanapata kipato na kuishi kama binadamu anavyotakiwa kuishi, na hawa waliojichokea Bongo mpaka uchawa imekuwa ajira bora nani?

Ujuwe nilikuwa nakuonaga kama mtu muelewa na mwenye exposure kubwa kumbe sivyo,

Kwahiyo unataka kila mtu awe mwizi kama wewe mpaka viwango vya kusakwa na FBI?

Taarifa zako tunazo mtumishi, acha dharau.
Mkuu Matola. Well said.
 
Ndugu yangu katika hiyo namba 2 Hadi chozi la huzuni [emoji25][emoji25]limenitoka. Hapa tulipo CCM wametukatia maji tokea 26/10/2021 hadi leo hii 20/11/2021 hakuna dalili ya maji kutoka yaani ni changamoto tupu.

Imagine ndugu yangu tunatamanije kuwa katika taifa lenye maisha ya pepo kama hilo?! Kwa maisha tunayoishi hapa Tanzania kiukweli kama kuna kwenda mbinguni au motoni basi watanzania nadhani tumeshatumikia 80% ya adhabu maana hawa wajaalaaana wanachofanya watajibia siku ya kiama mbwa hawa MUNGU mwenye neema awalaani wote.
Taratibu mkuu
 
Mpe connection ya jimama moja lugha atamfundisha huyohuyo.

Halafu zile mchongo za Au pair siku hizi Sweden hazipo?
Au pair Mkuu sina ufahamu nayo.

Mkuu, najuwa wewe ni senior kwenye masuala ya nchi za Ng'ambo kutokana na utafiti wangu humu JF. Ila mKuu siku hizi Sweden mambo yamebadilika, hata hiyo ya kutafuta ji-Mama siyo rahisi kama zamani. Yaani sera kuhusu wahamiaji zinaendelea kubanwa siku hadi siku. Hata ukipata mchumba, kwa sasa hupewi uraia mpaka huyo mchumba wako naye aje kwenu na kipindi cha kuomba ukazi urudi kwenu kwanza.
 
Sheria hiyo ya kuomba ukazi kwa kupata mke au mume anhörig invandring haijabadilishwa sana.Kilichoongezeka ni kwamba ukipata mchumba mume au mke ni lazima uwe na kipato cha kuwatosheleza na makazi.Sharti halikuwepo mwanzoni.Kuomba ukazi unafanya ukiwa nyumbani.Migrationsverket hawapokei maombi ukiwa Sweden.Maombi yanafanyika kwenye ubalozi wa Sweden Tanzania. Migrationsverket(Idara ya Uhamiaji) wanapokea maombi yako kutoka ubalozini.Interview unafanyia ubalozini.Sharti muhimu ni lazima uwe na passport kabla ya interview kurahisisha mchakato.
 
Back
Top Bottom