Mambo 15 niliyoyaona Simba vs Al Hilal leo

Mambo 15 niliyoyaona Simba vs Al Hilal leo

Malizia kabisa kuwa Simba, Yanga na Azam kama mna mpunga wa kutosha kuna wachezaji watatu wakali sana pale Al Hilal. Kazi kwenu Magori, Hersi na Popat wafuatao ni watu hasa Adama Coulibaly, EtaneJunior Aime Tendeng na Steven Ebuela.
 
Kumekuchaaaaaaa!!!
Simba nguvu 1, Gari Limewakaa.
[emoji91][emoji91][emoji91][emoji91][emoji91]
Tena lipo kwenye mteremko..alieko mbele ajiangalia asije sombwa...😃😃😃😃
 
1. Aishi Manula amebadilika na hasa anapowaiga Mussa Camara na Diarra kutembea na mpira, anastahili mkataba mpya

2. Kapombe jamani amepungua sana kama sio umakini wa Manula leo ingekuwa aibu

3. Valentine Nouma ni mchezaji wa kawaida sana, anachojua yeye ni mashuti tu lakini kukaba zero.

4. Chamou Karaboue apunguze uzito halafu aachane na mpira wa akina Salum Kabunda Ninja au Abdallah Msheli au Juma Nyosso.

5. Hamza ni mzuri lakini ana mapungufu kwanza yuko slow then hana speed

6. Che Malone apunguze utoto atakuja kuigharimu timu hatutamwelewa

7. Yussuf Kagoma ndio aina ya viungo wanaotakiwa, anarusha mipira ya mbali ili mawinga wakimbize, ila ana tabia za Tadeo Lwanga mtupu.

8. Debora Mavambo amefaulu mtihani wote utadhan tulitunga wote.

9. Augustine Okajepha ni aina ya viungo wa kisasa kabisa sijui kocha ana tatizo naye gani?

10. Chasambi anahitaji kucheza zaidi ili kuiletea mafanikio Simba

11. Kibu Denis namkubali sana na ndio tegemeo langu mimi hata kama alizingua kwenye usajili.

12. Valentine Mashaka apunguze uzito awe fiti zaidi.

13. Lionel Ateba ni Joseph Kaniki Golota mtupu.

14. Joshua Mutale ni Issa Kihange mtupu

15. Awesu Awesu ameikosea nini nchi hii hadi anaachwa timu ya Taifa? Yaan akina Mudathir sijui andambwile ndio wamweke benchi Awesu, Hemed Morocco unamkosea sana kiungo huyu mwenye udambwi udambwi mwingi kama enzi zile Michael Paul au Nylon.
Nambao 15 ...huyo unayesema anakosewa AWESU AWESU ni TAKATAKA KABISA haifai hata kuchezea KENGOLD.

TAKATAKA
 
Back
Top Bottom