Mambo 7 yanayopelekea kufa taratibu kabla ya kifo halisi

Mambo 7 yanayopelekea kufa taratibu kabla ya kifo halisi

Victor Mlaki

JF-Expert Member
Joined
May 1, 2016
Posts
4,151
Reaction score
4,277
Binadamu ameumbwa katika hali ya kuwajibika kipekee sana kwa ajili ya maisha yake kuliko viumbe wengine wengi tunaowaona katika uso wa Dunia.

Kuna mambo mengi mno ambayo binadamu akiyafanya yanamuua taratibutaratibu na mara nyingi zaidi kabla ya kifo halisi.

Siyo jambo la kushangaza kukutana na mtu anatembea lakini alishajiua mara nyingi mno kuelekea kifo chake.

Mambo saba yanayodhihirisha njia hizo ambazo ni hatari ni:-

1. Kuhifadhi kinyongo-Mfano kutunza watu waliokuudhi moyoni mwako kwa muda mrefu "keeping toxic people in your life"

2. Kuamini maoni ya watu kuhusu wewe na kuwafanya kana kwamba ni maisha yako."Maoni ya watu kuhusu maisha yako hatupaswi kuwa uhalisia wa maisha yako".Ukiona unaamini unachoambiwa kuhusu wewe na unakifanya kuwa uhalisia wa maisha yako jua hiyo siyo dalili nzuri.

3. Kufikiri furaha ni suala la baadae. Furaha katika maisha siyo suala la kughairisha kwa ajili ya baadae.Ukiona unaamini katika kuhuzunia na kusinoneka sasa kwa ajili ya baadae elewa hiyo ni dalili ya hatari kwa sababu furaha ni kile unachofanya kwa ajili ya sasa "something you design for the present"

4. Ulalamishi sugu (chronically complaining).

5. Kuishi kwa hofu. William Shakespeare Mtu anayeishi kwa hofu hujiua mara 1000 zaidi kabla ya kifo halisi.

6. Kutokuzingatia muda. Uhai unaweza kukudanganya kuwa unaendelea na ukizubaa ukachezea muda unaopita unaweza ukajikuta umejiweka kwenye hatari kubwa mno.

7. Kutokuwajibika. Hakuna mwenye wajibu wa kuyalinda maisha yako kama unavyopaswa kufanya wewe mwenyewe na unaposhindwa kuwajibika kikamilifu kwa ajili yako elewa hayupo atakayeweza kuchukua nafasi yako ya uwajibikaji juu yako.

Amua sasa "Maisha yako ni kwa ajili yako"

MoT.
 
Namba 5 inanisumbua sana.

Namba 5 inaelezea kile unachofikiri kuwa kinaweza kutokea ila hakijatokea. Ni sawa na kuogopa matokeo ya kitu ambacho hakijatokea. Hali hii imetuumiza wengi mno lakini ukitaka kushinda ni kukubali kuwa hiyo ni matokeo ya kitu ambacho hakijatokea na wakati mwingine kinaweza kisitokee.

Jizoeshe kupuuzia ili akili isizalishe picha za kukuumiza zaidi.

Wengi unaowaona kama hawana hiyo namba 5 kiuhalisia wanayo ila wanajitahidi kuisupress kwa sababu ni matokeo ya kitu ambacho hakijatokea.

Usipoteze muda kuwazia matokeo ya kitu ambacho hakijafanyika na wala hakijatokea (learn to attract good impressions).
Wanaothubutu haimaainshi namba 5 haiwahusu wanaipuuzia ili wawajibike kikamilifu kwa ajili ya maisha yao.
"Nothing to fear than the fear itself", Frankiln Delano Roosevelt.
 
Kweli, lakini mazingira yanayokuzunguka yanakurudisha kwenye mawazo. Dawa za Hosp kidogo zinasaidia.
Ni kweli mazingira yanaweza kuwa changamoto ila unao uwezo wa kuamua juu ya maisha yako katika mazingira yoyote yale "Amini hivyo na ndivyo ilivyo".
Dawa za hospitali ni kama placebo zinakughiribu akili hazitokupa msaada wa kudumu.
 
Yaani namba moja acha iniuwe na kunizika lkn Kuna watu siwezi kuwasamehe bure bure tuuu.
Inakutoa kwenye focus Mkuu inawezekana kuamua kusamehe na kusahau...Ukiiendekeza inakufanya uwaze mawazo hasi yatakayokuumiza sana.
Hata Mimi huwa inanisumbua ila nimejifunza kupuuzia ili nifanye yanayonihusu.
 
Inakutoa kwenye focus Mkuu inawezekana kuamua kusamehe na kusahau...Ukiiendekeza inakufanya uwaze mawazo hasi yatakayokuumiza sana.
Hata Mimi huwa inanisumbua ila nimejifunza kupuuzia ili nifanye yanayonihusu.

Nimeamua tuu kujitenga nae kwake siendi Wala simtafuti kbs.
 
UKWELI MTUPU...asante sana ila namba 5 ni changamoto kubwa kwa watu wengi
 
Nimeamua tuu kujitenga nae kwake siendi Wala simtafuti kbs.
That is one of the alternative itakusaidia Mkuu ila msaada wa kudumu ni kuendelea kuitrain akili yako kupuuzia masuala unavyoona yanakuumisa ili isizalishe mawazo yatakayokuumiza zaidi.
Ipo hivi ndugu ..."Unapowaza wazo moja baya linazalisha picha nyingi zaidi mbaya katika akili yako,picha ambazo zitakuumiza zaidi na unaweza kukuta aliyekukera alishasahau anakula raha wewe unamkeep tu.
......attract good to be good...
 
UKWELI MTUPU...asante sana ila namba 5 ni changamoto kubwa kwa watu wengi
Naam!.. hata kwangu inaniuhusu ila ninapokumbuka ninawajibu kwenye maisha yangu na hiyo inaniharibia huwa naipuuzia.
Kaka wanaothubutu haimaanishi haiwasumbui ila wanaipuuzia na wanasonga mbele.
 
Inakutoa kwenye focus Mkuu inawezekana kuamua kusamehe na kusahau...Ukiiendekeza inakufanya uwaze mawazo hasi yatakayokuumiza sana.
Hata Mimi huwa inanisumbua ila nimejifunza kupuuzia ili nifanye yanayonihusu.


Kwanza umeongea vitu vya muhimu sana, kuwasamehe na kutokubeba waliokukwaza au kukuumiza inahitaji ukomavu na rehema za Mungu, lakini inawezekana.

Mara zote napinga kauli ya kusamehe na kusahau. Kusamehe ntasamehe ila siwezi kusahau kama kuna mtu aliwahi kunikosea au kunikwaza, ntakachotakiwa ni nnafanyaje nnapokumbuka hilo tukio? Hapo ndio tofauti inakuja sasa.

Ukinitukana leo nikakusamehe kutoka ndani, akili yangu haitafuta kwamba umenitukana ila itajikumbusha kwamba tulishasameheana hakuna chochote kibaya. Hivyo hiyo kumbu kumbu ya tukio hainisumbui tena.

Kuna wale kila akikumbuka asira zinamjia anacharuka au kufanya kituko au tukio, hiyo ni kujiua pole pole bila kujua.
 
Embu tafakari hofu ilivyo mbaya,Hofu ni sawa na mfano huu hapa chini.
"Kitu ambacho hakipo sasa lakini kinaharibu maisha yako ya sasa (ni sawa na kujiuliza nini kitatokea kwenye maisha yako baadae na ni kweli huwezi kukijua )".....fear is about something that is yet to be..
Kama hatufahamu nini kitatokea kwenye maisha yetu kwa nini tuwazie hofu na matokeo yake?..ni jambo la hatari sana.
 
Binadamu wengi tunapiga hatua nusu kwa sababu ya hofu (maumivu) tunajiuliza kama kutokea hivi nitakuwa?Je ni nini kitanitokea?..lakini kama tukiweza kujitawala wenyewe " well managed" tukaweza kutawala miili yetu,hisia zetu,mawazo yeti n.k.

Kama hatuwezi kujitawala wenyewe hatuwezi kupiga hatua yoyote ya kuendelea,sisemi kwamba ni kosa kuwa hivyo ila ni kuwa kinyume na Kanuni za asili za kuwa binadamu (against the nature of existence)
Na ukiwa katika hali ya kushindwa kujitawala thamani na uwezo wa kuwa binadamu "ubinadamu wetu unakuwa umetoweka"

Kama binadamu ni kiumbe mwenye akili kuliko viumbe wengine wote tujiulize je tunapaswa kuzungumzia vikwazo au mafanikio na fursa za kuendelea vizuri?

Kwa mfano una akili nzuri na hajui namna ya kuitumia je ni jambo la kawaida?..(kuna haja ya kujifunza kutumia akili na mawazo yetu kwa ajili ya maisha yetu.

Let us talk about possibilities of being human rather than limitations.
 
Back
Top Bottom