Mambo 7 yanayopelekea kufa taratibu kabla ya kifo halisi

Mambo 7 yanayopelekea kufa taratibu kabla ya kifo halisi

Biblia haijawahi kudanganya wala kukosea, biblia ni kila kitu katika maisha yetu, sema shida yetu Ni upungufu wa Imani, au kuyumbishwa na Imani za wasioamini, niseme tu usimwamini mtu yoyote duniani ila tu ishi nao kwa akili na tahadhari kubwa, kuna watu waliwaamini ndugu zao wakawaangamiza, kuna waliowaamini wazazi wao wakawaangamiza, kuna wengine waliowaamini wenza wao wakawamaliza, Hali kadhalika hata watoto waliowazaa au marafiki wakawaamini wakawaangamiza, haya maisha hayana formula, bila Mungu kusimama upande wako hakika dunia itakuangamiza hadi ukashangaa, na kinachotuponza Ni kutanguliza mapenzi/upendo wetu kwa watu pasipo kumtanguliza Mungu, kumbuka Shetani yupo duniani na kazi yake Ni kutafuta wafuasi, Mara nyingi hushughulika na wanaomwamini Mungu ili awaangushe, hivyo basi yeyote umpendaye na kumwamini anaweza kutumiwa na Shetani na akakuangamiza, hatuwezi kukwepa Ila tukimtanguliza Mungu hakika hawatatudhuru, tuendelee kuwapenda na kuwakmbea tuwapendao. Tuzidishe maombi na kumtegemea Mungu tu.
Mambo Ni mengi sana, Mungu aturehemu kwa pendo lake.
Tafadhali,kama ni mkristo soma Yeremia 12:6 halafu naomba mrejesho. Nimewahi kufanyiwa kitu kibaya sana na ndugu zangu kwa matumaini yao kwamba ninaweza kujiua. Kwa kweli ilikuwa mtihani mkubwa sana. Nashukuru sana Mungu hali sasa imetulia

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Biblia haijawahi kudanganya wala kukosea, biblia ni kila kitu katika maisha yetu, sema shida yetu Ni upungufu wa Imani, au kuyumbishwa na Imani za wasioamini, niseme tu usimwamini mtu yoyote duniani ila tu ishi nao kwa akili na tahadhari kubwa, kuna watu waliwaamini ndugu zao wakawaangamiza, kuna waliowaamini wazazi wao wakawaangamiza, kuna wengine waliowaamini wenza wao wakawamaliza, Hali kadhalika hata watoto waliowazaa au marafiki wakawaamini wakawaangamiza, haya maisha hayana formula, bila Mungu kusimama upande wako hakika dunia itakuangamiza hadi ukashangaa, na kinachotuponza Ni kutanguliza mapenzi/upendo wetu kwa watu pasipo kumtanguliza Mungu, kumbuka Shetani yupo duniani na kazi yake Ni kutafuta wafuasi, Mara nyingi hushughulika na wanaomwamini Mungu ili awaangushe, hivyo basi yeyote umpendaye na kumwamini anaweza kutumiwa na Shetani na akakuangamiza, hatuwezi kukwepa Ila tukimtanguliza Mungu hakika hawatatudhuru, tuendelee kuwapenda na kuwakmbea tuwapendao. Tuzidishe maombi na kumtegemea Mungu tu.
Mambo Ni mengi sana, Mungu aturehemu kwa pendo lake.

Sent using Jamii Forums mobile app
Nimefurahi na kufarijika sana. Tafadhali on a pia Zaburi 55:12-14, 16
 
ukweli mtupu, iyo ya mwisho naigongelea msumari kabisa.
 
Binadamu ameumbwa katika hali ya kuwajibika kipekee sana kwa ajili ya maisha yake kuliko viumbe wengine wengi tunaowaona katika uso wa Dunia.

Kuna mambo mengi mno ambayo binadamu akiyafanya yanamuua taratibutaratibu na mara nyingi zaidi kabla ya kifo halisi.

Siyo jambo la kushangaza kukutana na mtu anatembea lakini alishajiua mara nyingi mno kuelekea kifo chake.

Mambo saba yanayodhihirisha njia hizo ambazo ni hatari ni:-

1. Kuhifadhi kinyongo-Mfano kutunza watu waliokuudhi moyoni mwako kwa muda mrefu "keeping toxic people in your life"

2. Kuamini maoni ya watu kuhusu wewe na kuwafanya kana kwamba ni maisha yako."Maoni ya watu kuhusu maisha yako hatupaswi kuwa uhalisia wa maisha yako".Ukiona unaamini unachoambiwa kuhusu wewe na unakifanya kuwa uhalisia wa maisha yako jua hiyo siyo dalili nzuri.

3. Kufikiri furaha ni suala la baadae. Furaha katika maisha siyo suala la kughairisha kwa ajili ya baadae.Ukiona unaamini katika kuhuzunia na kusinoneka sasa kwa ajili ya baadae elewa hiyo ni dalili ya hatari kwa sababu furaha ni kile unachofanya kwa ajili ya sasa "something you design for the present"

4. Ulalamishi sugu (chronically complaining).

5. Kuishi kwa hofu. William Shakespeare Mtu anayeishi kwa hofu hujiua mara 1000 zaidi kabla ya kifo halisi.

6. Kutokuzingatia muda. Uhai unaweza kukudanganya kuwa unaendelea na ukizubaa ukachezea muda unaopita unaweza ukajikuta umejiweka kwenye hatari kubwa mno.

7. Kutokuwajibika. Hakuna mwenye wajibu wa kuyalinda maisha yako kama unavyopaswa kufanya wewe mwenyewe na unaposhindwa kuwajibika kikamilifu kwa ajili yako elewa hayupo atakayeweza kuchukua nafasi yako ya uwajibikaji juu yako.

Amua sasa "Maisha yako ni kwa ajili yako"

MoT.
Kweli, kweli, kweli tupu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mi kinachonipunguzia furaha katika maisha ni kukosa Economic freedom!

Mpaka sasa sijafikia level ambayo naweza ku relax. Kuhusu kusamehe na kupotezea niko vyema na sina kawaida ya kusikiliza watu wanasema nini juu yangu so walimwengu hawaniumizi kwa maneno.
 
Ridhika na ulichonacho huku ukiendelea kupambana, kamwe huwezi ridhika hata ukifikia kiwango kikubwa cha uchumi endapo hutawajali wahitaji, kuwa mwema kwa wengine (kufanya udiakonia) itakusaidia kiasi
Mi kinachonipunguzia furaha katika maisha ni kukosa Economic freedom!

Mpaka sasa sijafikia level ambayo naweza ku relax. Kuhusu kusamehe na kupotezea niko vyema na sina kawaida ya kusikiliza watu wanasema nini juu yangu so walimwengu hawaniumizi kwa maneno.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimefarijika sana ndugu juu ya namna ulivyoonesha unafahamu ni kipi hasa unahitaji yaani "economic freedom".
Kutambua hitaji ni jambo moja na kupata unachohitaji ni kitu kingine.Tunapaswa kuwa makini sana katika kubaini ni kipi hasa tunahitaji.
Katika uzoefu wa maisha kwa mfano Mimi mwenyewe kuna wakati nilikuwa nafahamu kuwa nahitaji kitu fulani ila nilipokipata nilijikuta sijaridhika nahitaji kitu kingine zaidi.Hali hii ilinipa fundisho kuwa sikuweka utayari katika kubaini hitaji langu hasa ni lipi.
Tumeumbwa kwa namna ambayo tunaweza kuumba tuyatakayo au kutafuta tuyatakayo ili mradi mawazo yetu,hisia zetu,akili zetu na kani za uhai wetu zinaelekea kwenye uelekeo mmoja tunaouhitaji.Baadhi ya wataalamu wanamfananisha binadamu na sumaku kubwa "big magnet"inayoweza kuyavuta inayoyahitaji na kusukuma ambayo haiyahitaji.
Unakosa furaha kwa sababu ndiyo haswa unayoihitaji.Ngoja niandike taratibu huenda itaeleweka kiasi.
Economic freedom sicho hasa unachohitaji ila unachohitaji ni kuzalisha thamani zitakazokupatia uchumi ambao unadhani utakupa furaha "kwa maana nyingine economic freedom is not an end bu a means to an end.
You are welcome Brethren.
 
Kwa maana hiyo, wabongo wengi ni wafu wanaotembea. 🚶🏻🚶🏻
 
Ridhika na ulichonacho huku ukiendelea kupambana, kamwe huwezi ridhika hata ukifikia kiwango kikubwa cha uchumi endapo hutawajali wahitaji, kuwa mwema kwa wengine (kufanya udiakonia) itakusaidia kiasi

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu kuna contradictory argument hapo.
Sidhani kama unaweza ukaridhika halafu ukaendelea kupambana kwa tafsiri ya neno ridhika".
Uumbaji wetu unaonesha hatuna asili ya kuridhika ila kukua na kujua zaidi na zaidi.Ndiyo maana yupo hai hatujafa kifo halisi lakini tunatamani kujua habari na uzoefu wa kifo halisi.
 
Kuwa huru ndugu, si ungejenga hoja yako kwa uwazi ili tujifunze wote?
Unataka kusema niliandika bila kufikiri?..(sasa niliandikajeandikaje?..strong points unazoona zimekosekana ungeziandika hapa huoni kama ingesaidia zaidi ya unavyojisifu kuwa una uwezo mkubwa wa kufikiri.
Umetumia lugha iliyojaa dharau na haitokusaidia sana katika maisha yako " ni jambo la fedheha sana umrlifanya hapa"...kimantiki umemaanisha sikufikiri au nina uwezo duni wa kufikiri kuliko wewe.
Sasa nikuweke wa zi tu wenye uwezo wa kufikiri wanapotaka kuwasaidia ambao wanawahisi hawana uwezo wa kufikiri hujenga hoja zinazoonesha usahihi wa jambo unavyopaswa kuwa na siyo kujisifu.
Unge ainisha strong pointsculizoona zinakosekana hapo ili tujifunze na siyo kuishia kusema kuna strong points zimekosekana.Nimesikitishwa sana na lugha mbovu iliyojaa na dharau kutokea na "Mwanajamii forum kama wewe".
Peace


The Two Most Important Day In your Life Are The You Were Born And The Day You Find Out Why "

PEACE
 
Mkuu kuna contradictory argument hapo.
Sidhani kama unaweza ukaridhika halafu ukaendelea kupambana kwa tafsiri ya neno ridhika".
Uumbaji wetu unaonesha hatuna asili ya kuridhika ila kukua na kujua zaidi na zaidi.Ndiyo maana yupo hai hatujafa kifo halisi lakini tunatamani kujua habari na uzoefu wa kifo halisi.
Kuridhika Ni kuikubali Hali halisi na sio kuacha kusonga mbele

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hiyo ndiyo maana ya kuridhika au uliyomaanisha wewe Mkuu?.
Kama ndiyo uliyomaanisha naunga mkono hoja
 
Back
Top Bottom