Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 28,297
- 68,017
SAFIRI SALAMA NA BINTI YAKO, USIMUACHE; HUKO MBELE HAKUFAI.
Kwa Mkono wa Robert Heriel
Andiko hili lamfaa mtu yeyote yule, hasa wazazi wenye watoto wakike. Bila shaka litakuwa msaada kwa sehemu kubwa ikiwa litazingatiwa.
Nilipokuwa mwaka wa pili pale UDSM nikiwa naishi Sinza Kwaremi, nilipata Rafiki jirani yangu ambaye alikuwa Fundi nguo. Huyu alikuwa kama kaka yangu, nikiwa sina vipindi chuoni nilikuwa nakaa ofisini kwake nakupiga stori za hapa na pale. Hata hivyo niliona kupiga stori pekee isingetosha hivyo nikamuomba anifundishe kushona nguo ili nami niweze kupata ujuzi wa kushona, na nimsaidie baadhi ya kazi ndogo ndogo.
Fundi alishangaa sana, akaniambia; Taikon acha utani bhana, wewe hutaweza kazi hizi, wewe ni msomi, kazi hii ya nini sasa.Wewe kazi zako ni kukaa ofisini na kushika kalamu tuu"
Kama alivyonishangaa ndivyo nami nilivyomshangaa kwa kauli yake. Hata hivyo baada ya kumsihi sana akakubali na safari yetu ya mafunzo ikaanza mara moja, mafunzo yaliboresha urafiki wetu na kufikia undugu kabisa.
Siku moja Fundi aliongea maneno ambayo leo ndio nimeona niyaeleze hapa baada ya mimi mwenyewe kufanya uchunguzi wangu kupitia wateja wengi wanaokuja pale ofisini.
Fundi akaongea; "Taikon, natamani watoto wangu wangekuwa na moyo wa kusoma angalau wafike hata chuo kikuu wawe na taaluma zao, lakini mabinti zangu shule imewashinda. Hata kushona kwenyewe hawataki, hivi watakuwa wageni wa nani kwa miaka ijayo? Wewe mwenyewe unaona wateja wetu wanaokuja hapa, si unaona lakini?"
Fundi aliongea kwa uchungu sana, nilimuelewa alikuwa anazungumzia nini. Fundi anawatoto wakike tuu.
Kwa ufupi wateja wetu waliokuwa wanakuja pale walikuwa ni wasomi wenye kazi zao, wengine walikuwa madaktari, waalimu, manesi, wahasibu, polisi, wanasheria ambao kwa sehemu kuja walikuja na magari yao. Hata hivyo kwenye stori zao baadhi yao walioonekana wao ndio wanaotunza familia, wanaohakikisha waume zao hawawatoroki kama manavyojua kwa sasa maeneo ya majiji makubwa vijana kwa sasa hawana kazi, hivyo wanawake wenye kazi wanaitumia fursa hiyo kuchagua mwanaume yeyote mzuri wamtakaye.
Fundi aliwahi sema kwa hali hii, kama binti yako hana maisha atapata kweli mwanaume wa maana wa kumuoa, maana vijana wenyewe wa siku hizi ndio hawa ambao kazi wamewaachia wanaume. Pengine nisieleweke vyema lakini najaribu kueleza kuwa kizazi kinachokuja wanaume wengi watapwaya, watapenda wanawake wenye kazi na pesa, je umemuandaaje binti yako?
Je umemuandaaje binti yako kukabiliana na fujo ya huko mbele?
Maisha yamebadilika lazima nasi tubadilike.
Usipomuandaa binti yako akawa mwanamke shupavu anayejiweza kifikra, kiroho na kiuchumi hakika usije mlaaumu huko mbeleni kwa sababu lazima atie aibu na kukudhalilisha.
Asijekukudanganya mtu TAMAA ya mwanamke Ipo kwa mwanaume kama alivyosema MUNGU, kila mwanamke hutaka kupendwa na mume wake, sasa mchakato wa kupata mume kwa siku zijazo utakuwa mgumu kidogo kwa wanawake wasio na vipato vizuri, na wasio na uimara wa kimaisha.
Imezoeleka kuwa wanawake wengi mkombozi wao ni Waganga wa kienyeji, wengi hukimbilia huko kupata msaada wa kupata au kumtuliza mwanaume, lakini mambo ya uganga ni teknolojia ya kizamani sana ambayo karne hii nguvu yake inazidi kupungua kila uchwao.
Kama Uganga na ushirikina unaisha nguvu na watoto wako hawajasoma na hawana vipato unafikiri dunia hii ataishije?
Wazungu kwa kulitambua hili ndio maana wakaona watoe fursa kwa jinsia zote kupata haki za huduma za kijamii kama elimu, urithi, uongozi nk.
MAMBO AMBAYO UNAPASWA UMPE BINTI YAKO KATIKA KARNE HII YAKAYOMSAIDIA KATIKA MAISHA YAKE.
1. Mfunze habari za Mungu
Mfunze Mungu ni nani, mfunze yeye ni nani, mfunze mwaname ni nani. Kisha mfunze kwa mwanaume anatafuta nini, na atawezaje kuishi na mwanaume.
Ukishamfunza Mungu ni nani automatic atajua yeye ni nani, atajiheshimu na kujua nafasi yake kwenye jamii ni ipi. Kisha atamheshimu Mwanaume ambaye ndiye atakuwa Mume wake.
Kumfunza Mtoto habari za Mungu ni kumfunza utulivu katika maisha yake,
2. MPE ELIMU YA DUNIA.
Elimu ya Mungu haitoshi kabisa kwenye dunia hii. Hata ajue na akariri misahafu yote lakini kama hana elimu dunia bado ataonja joto la jiwe. Elimu ya Mungu inamsaidia mtu kuwa na utulivu na maadili, lakini haiamshi ari ya kufanikiwa kidunia. Elimu ya Dunia ni kichocheo cha maisha.
Mpe binti yako elimu ya kidunia ili awe kumudu maisha ya duniani, apate taaluma, aweze kuchanganua mambo na kuyachambua. Elimu ya kidunia hutumika pia kupata kazi za kidunia.
Binti asiye na elimu kwa wakati ujao atapata tabu sana. Na hii ni kutokana na ile dhana ya HAKI SAWA ambayo kimsingi itawaumiza wanawake wengi mno ambao hawatakuwa kwenye nafasi nzuri kiuchumi na kimaisha.
3. MUWEZESHE KIUCHUMI
Muwezeshe binti yako kiuchumi, mfundishe namna ya kutafuta pesa, kutunza pesa na kuzizalisha ziwe nyingi zaidi. 'Kizazi kinachokuja sifa namba moja ya mwanamke atakayetafutwa ni mwenye uchumi au kazi nzuri. Uzuri hautakuwa tena kipaombele namba moja.
Nguvu ya mwanamke itakuwa ni uchumi na pesa zake.
Hata sasa wanaume wengi wanatafuta mwanamke wa kusaidiana naye kwenye maisha, huu ni mwanzo tuu, tunapoelekea haitakuwa wakusaidizana naye bali atakayeweza kuisimamia yeye mwenyewe familia.
Kama ilivyosasa kuwa wanawake wanapenda wanaume wenye vipato vizuri ndivyo itakavyokuwa baadaye kuwa wanaume nao watapenda zaidi wanawake wenye vipato.
Kama ilivyosasa wanaume wenye pesa huweza kumnyang'anya mke mwanaume asiye na pesa, ndivyo itakavyokuwa siku zijazo kuwa mwanamke mwenye pesa atanyang'anya mume wa mtu, ambaye mke wake ni hohehahe.
Usije ukajidanganya kuwa sijui wajibu wa mwanaume ni kulisha familia, hilo halitakuwepo huko tuendako.
FAIDA YA KUMUINUA BINTI YAKO NA KUMFANYA KUWA NA MAISHA BORA
1. Ataweza kuitunza familia yake.
Siku hizi wanaume wengi huzitelekeza familia zao kutokana na sababu mbalimbali. Ikiwa binti yako atatelekezwa basi atakuwa na uwezo wa kuimudu na kuitunza familia yake, yaani watoto wake. Hii pia inaenda sambamba na kama binti yako atafiwa na mume wake bado atakuwa na uwezo wa kuitunza familia yake kwa vile anakazi yake au kiuchumi yuko fit
Lakini ikiwa hautamfanya binti yako awe imara kiuchumi basi majina yote mabaya ya kumdhihaki yatamhusu, atadanga(kufanya umalaya), ataitwa single Mother na majina mengine yatakayozuka wakati huo.
Binti yako ukimfanya kuwa bora nakuhakikishia wajukuu zako lazima wawe bora, kwani mama ndiye kashikilia malezi ya watoto
2. HATABABAISHWA NA MWANAUME MPUMBAVU
Binti ukishamfundisha mambo hayo matatu, nayo ni elimu ya Mungu, elimu dunia, na kujitafutia kipato akamaster yote kamwe hawezi babaishwa na wanaume wapumbavu ati kisa mapenzi. Mwanamke anayejitambua hawezi babaishwa na mwanaume asiye na akili.
Wanawake wengi wa siku hizi hubabaishwa kwa sababu ya kukosa mafunzo yaliyojitosheleza, unakuta binti anapesa na kazi nzuri lakini hana elimu ya Mungu, au anaelimu ya MUNGU lakini hana pesa, au anaelimu ya dunia na pesa lakini hana Elimu ya Mungu, huyu lazima ababaishwe tuu kivyovyote.
Niliwahi kumuona mwanamke mmoja msomi mwenye kipato kizuri aliyeolewa na kigogo fulani akiliwa uroda na Mganga wa kienyeji kisa kutafuta kupendwa na Mume wake. Mwanamke huyu alikosa elimu ya Mungu ndio maana alibabaishwa hadi kufikia kuliwa uroda na mganga.
3. HATAPATA SHIDA KUMPATA MWENZA WAKE.
Hakuna mwanaume chini ya jua ambaye hataki mwanamke mwenye elimu ya Mungu, mwenye elimu, na mwenye kipato kizuri. Hayupo na hajawahi kutokea.
Binti yako akiwa bora kwenye maeneo hayo atawagaragaza wanaume vile atakavyo, na kumpata amtakaye.
Lakini kama atakosa yote hayo nakuhakikisha dunia hii itakuwa chungu sana kwake. Atajifunza ulozi lakini hautamsaidia kwani kipindi kinachokuja uchawi hautakuwa na nguvu kama ilivyo kwa maombi ya Mungu.
Dunia itakuwa inaendeshwa kwa asilimia kubwa na nguvu na akili ya mwanadamu tofauti na ilivyokuwa zamani ambapo dunia ilikuwa inaendeshwa na nguvu zisizoonekana kama Miungu, majini, mizimu na mashetani. Hivyo nguvu ya uchawi na nguvu ya Maombi inazidi kupungua kadiri nguvu ya mwanadamu katika kuutawala ulimwengu inavyoongezeka.
Palipo na nguvu na akili kubwa ya mwanadamu jua kuna nguvu ndogo ya Mungu au Uchawi
Palipo na nguvu na akili ndogo ya mwanadamu jua kuna nguvu na akili kubwa ya Mungu au uchawi.
Neno hili la Nabii Isaya linaenda kutimia
Isaya 4:1
Na siku hiyo wanawake saba watamshika mtu mume mmoja wakisema, Tutakula chakula chetu, na kuvaa nguo zetu wenyewe, lakini tuitwe tu kwa jina lako; utuondolee aibu yetu.
Safiri salama na binti yako, mfanye kuwa bora ili asije akawa kioja katika dunia hii yenye dhiki.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
Kwa sasa Morogoro
Kwa Mkono wa Robert Heriel
Andiko hili lamfaa mtu yeyote yule, hasa wazazi wenye watoto wakike. Bila shaka litakuwa msaada kwa sehemu kubwa ikiwa litazingatiwa.
Nilipokuwa mwaka wa pili pale UDSM nikiwa naishi Sinza Kwaremi, nilipata Rafiki jirani yangu ambaye alikuwa Fundi nguo. Huyu alikuwa kama kaka yangu, nikiwa sina vipindi chuoni nilikuwa nakaa ofisini kwake nakupiga stori za hapa na pale. Hata hivyo niliona kupiga stori pekee isingetosha hivyo nikamuomba anifundishe kushona nguo ili nami niweze kupata ujuzi wa kushona, na nimsaidie baadhi ya kazi ndogo ndogo.
Fundi alishangaa sana, akaniambia; Taikon acha utani bhana, wewe hutaweza kazi hizi, wewe ni msomi, kazi hii ya nini sasa.Wewe kazi zako ni kukaa ofisini na kushika kalamu tuu"
Kama alivyonishangaa ndivyo nami nilivyomshangaa kwa kauli yake. Hata hivyo baada ya kumsihi sana akakubali na safari yetu ya mafunzo ikaanza mara moja, mafunzo yaliboresha urafiki wetu na kufikia undugu kabisa.
Siku moja Fundi aliongea maneno ambayo leo ndio nimeona niyaeleze hapa baada ya mimi mwenyewe kufanya uchunguzi wangu kupitia wateja wengi wanaokuja pale ofisini.
Fundi akaongea; "Taikon, natamani watoto wangu wangekuwa na moyo wa kusoma angalau wafike hata chuo kikuu wawe na taaluma zao, lakini mabinti zangu shule imewashinda. Hata kushona kwenyewe hawataki, hivi watakuwa wageni wa nani kwa miaka ijayo? Wewe mwenyewe unaona wateja wetu wanaokuja hapa, si unaona lakini?"
Fundi aliongea kwa uchungu sana, nilimuelewa alikuwa anazungumzia nini. Fundi anawatoto wakike tuu.
Kwa ufupi wateja wetu waliokuwa wanakuja pale walikuwa ni wasomi wenye kazi zao, wengine walikuwa madaktari, waalimu, manesi, wahasibu, polisi, wanasheria ambao kwa sehemu kuja walikuja na magari yao. Hata hivyo kwenye stori zao baadhi yao walioonekana wao ndio wanaotunza familia, wanaohakikisha waume zao hawawatoroki kama manavyojua kwa sasa maeneo ya majiji makubwa vijana kwa sasa hawana kazi, hivyo wanawake wenye kazi wanaitumia fursa hiyo kuchagua mwanaume yeyote mzuri wamtakaye.
Fundi aliwahi sema kwa hali hii, kama binti yako hana maisha atapata kweli mwanaume wa maana wa kumuoa, maana vijana wenyewe wa siku hizi ndio hawa ambao kazi wamewaachia wanaume. Pengine nisieleweke vyema lakini najaribu kueleza kuwa kizazi kinachokuja wanaume wengi watapwaya, watapenda wanawake wenye kazi na pesa, je umemuandaaje binti yako?
Je umemuandaaje binti yako kukabiliana na fujo ya huko mbele?
Maisha yamebadilika lazima nasi tubadilike.
Usipomuandaa binti yako akawa mwanamke shupavu anayejiweza kifikra, kiroho na kiuchumi hakika usije mlaaumu huko mbeleni kwa sababu lazima atie aibu na kukudhalilisha.
Asijekukudanganya mtu TAMAA ya mwanamke Ipo kwa mwanaume kama alivyosema MUNGU, kila mwanamke hutaka kupendwa na mume wake, sasa mchakato wa kupata mume kwa siku zijazo utakuwa mgumu kidogo kwa wanawake wasio na vipato vizuri, na wasio na uimara wa kimaisha.
Imezoeleka kuwa wanawake wengi mkombozi wao ni Waganga wa kienyeji, wengi hukimbilia huko kupata msaada wa kupata au kumtuliza mwanaume, lakini mambo ya uganga ni teknolojia ya kizamani sana ambayo karne hii nguvu yake inazidi kupungua kila uchwao.
Kama Uganga na ushirikina unaisha nguvu na watoto wako hawajasoma na hawana vipato unafikiri dunia hii ataishije?
Wazungu kwa kulitambua hili ndio maana wakaona watoe fursa kwa jinsia zote kupata haki za huduma za kijamii kama elimu, urithi, uongozi nk.
MAMBO AMBAYO UNAPASWA UMPE BINTI YAKO KATIKA KARNE HII YAKAYOMSAIDIA KATIKA MAISHA YAKE.
1. Mfunze habari za Mungu
Mfunze Mungu ni nani, mfunze yeye ni nani, mfunze mwaname ni nani. Kisha mfunze kwa mwanaume anatafuta nini, na atawezaje kuishi na mwanaume.
Ukishamfunza Mungu ni nani automatic atajua yeye ni nani, atajiheshimu na kujua nafasi yake kwenye jamii ni ipi. Kisha atamheshimu Mwanaume ambaye ndiye atakuwa Mume wake.
Kumfunza Mtoto habari za Mungu ni kumfunza utulivu katika maisha yake,
2. MPE ELIMU YA DUNIA.
Elimu ya Mungu haitoshi kabisa kwenye dunia hii. Hata ajue na akariri misahafu yote lakini kama hana elimu dunia bado ataonja joto la jiwe. Elimu ya Mungu inamsaidia mtu kuwa na utulivu na maadili, lakini haiamshi ari ya kufanikiwa kidunia. Elimu ya Dunia ni kichocheo cha maisha.
Mpe binti yako elimu ya kidunia ili awe kumudu maisha ya duniani, apate taaluma, aweze kuchanganua mambo na kuyachambua. Elimu ya kidunia hutumika pia kupata kazi za kidunia.
Binti asiye na elimu kwa wakati ujao atapata tabu sana. Na hii ni kutokana na ile dhana ya HAKI SAWA ambayo kimsingi itawaumiza wanawake wengi mno ambao hawatakuwa kwenye nafasi nzuri kiuchumi na kimaisha.
3. MUWEZESHE KIUCHUMI
Muwezeshe binti yako kiuchumi, mfundishe namna ya kutafuta pesa, kutunza pesa na kuzizalisha ziwe nyingi zaidi. 'Kizazi kinachokuja sifa namba moja ya mwanamke atakayetafutwa ni mwenye uchumi au kazi nzuri. Uzuri hautakuwa tena kipaombele namba moja.
Nguvu ya mwanamke itakuwa ni uchumi na pesa zake.
Hata sasa wanaume wengi wanatafuta mwanamke wa kusaidiana naye kwenye maisha, huu ni mwanzo tuu, tunapoelekea haitakuwa wakusaidizana naye bali atakayeweza kuisimamia yeye mwenyewe familia.
Kama ilivyosasa kuwa wanawake wanapenda wanaume wenye vipato vizuri ndivyo itakavyokuwa baadaye kuwa wanaume nao watapenda zaidi wanawake wenye vipato.
Kama ilivyosasa wanaume wenye pesa huweza kumnyang'anya mke mwanaume asiye na pesa, ndivyo itakavyokuwa siku zijazo kuwa mwanamke mwenye pesa atanyang'anya mume wa mtu, ambaye mke wake ni hohehahe.
Usije ukajidanganya kuwa sijui wajibu wa mwanaume ni kulisha familia, hilo halitakuwepo huko tuendako.
FAIDA YA KUMUINUA BINTI YAKO NA KUMFANYA KUWA NA MAISHA BORA
1. Ataweza kuitunza familia yake.
Siku hizi wanaume wengi huzitelekeza familia zao kutokana na sababu mbalimbali. Ikiwa binti yako atatelekezwa basi atakuwa na uwezo wa kuimudu na kuitunza familia yake, yaani watoto wake. Hii pia inaenda sambamba na kama binti yako atafiwa na mume wake bado atakuwa na uwezo wa kuitunza familia yake kwa vile anakazi yake au kiuchumi yuko fit
Lakini ikiwa hautamfanya binti yako awe imara kiuchumi basi majina yote mabaya ya kumdhihaki yatamhusu, atadanga(kufanya umalaya), ataitwa single Mother na majina mengine yatakayozuka wakati huo.
Binti yako ukimfanya kuwa bora nakuhakikishia wajukuu zako lazima wawe bora, kwani mama ndiye kashikilia malezi ya watoto
2. HATABABAISHWA NA MWANAUME MPUMBAVU
Binti ukishamfundisha mambo hayo matatu, nayo ni elimu ya Mungu, elimu dunia, na kujitafutia kipato akamaster yote kamwe hawezi babaishwa na wanaume wapumbavu ati kisa mapenzi. Mwanamke anayejitambua hawezi babaishwa na mwanaume asiye na akili.
Wanawake wengi wa siku hizi hubabaishwa kwa sababu ya kukosa mafunzo yaliyojitosheleza, unakuta binti anapesa na kazi nzuri lakini hana elimu ya Mungu, au anaelimu ya MUNGU lakini hana pesa, au anaelimu ya dunia na pesa lakini hana Elimu ya Mungu, huyu lazima ababaishwe tuu kivyovyote.
Niliwahi kumuona mwanamke mmoja msomi mwenye kipato kizuri aliyeolewa na kigogo fulani akiliwa uroda na Mganga wa kienyeji kisa kutafuta kupendwa na Mume wake. Mwanamke huyu alikosa elimu ya Mungu ndio maana alibabaishwa hadi kufikia kuliwa uroda na mganga.
3. HATAPATA SHIDA KUMPATA MWENZA WAKE.
Hakuna mwanaume chini ya jua ambaye hataki mwanamke mwenye elimu ya Mungu, mwenye elimu, na mwenye kipato kizuri. Hayupo na hajawahi kutokea.
Binti yako akiwa bora kwenye maeneo hayo atawagaragaza wanaume vile atakavyo, na kumpata amtakaye.
Lakini kama atakosa yote hayo nakuhakikisha dunia hii itakuwa chungu sana kwake. Atajifunza ulozi lakini hautamsaidia kwani kipindi kinachokuja uchawi hautakuwa na nguvu kama ilivyo kwa maombi ya Mungu.
Dunia itakuwa inaendeshwa kwa asilimia kubwa na nguvu na akili ya mwanadamu tofauti na ilivyokuwa zamani ambapo dunia ilikuwa inaendeshwa na nguvu zisizoonekana kama Miungu, majini, mizimu na mashetani. Hivyo nguvu ya uchawi na nguvu ya Maombi inazidi kupungua kadiri nguvu ya mwanadamu katika kuutawala ulimwengu inavyoongezeka.
Palipo na nguvu na akili kubwa ya mwanadamu jua kuna nguvu ndogo ya Mungu au Uchawi
Palipo na nguvu na akili ndogo ya mwanadamu jua kuna nguvu na akili kubwa ya Mungu au uchawi.
Neno hili la Nabii Isaya linaenda kutimia
Isaya 4:1
Na siku hiyo wanawake saba watamshika mtu mume mmoja wakisema, Tutakula chakula chetu, na kuvaa nguo zetu wenyewe, lakini tuitwe tu kwa jina lako; utuondolee aibu yetu.
Safiri salama na binti yako, mfanye kuwa bora ili asije akawa kioja katika dunia hii yenye dhiki.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
Kwa sasa Morogoro