Mambo kadhaa ya kufurahisha kuhusu the late Steve Jobs

Mambo kadhaa ya kufurahisha kuhusu the late Steve Jobs

Nafaka

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2015
Posts
12,154
Reaction score
31,246
Huyu jamaa alikuwa na akili nyingi sana. Ni mmoja kati ya waanzilishi wa kampuni ya apple. Yeye na Billgates walikuwa mahasimu wakubwa sana kila mmoja akimdharau mwenzake.

Mfano Steve Jobs alikuwa anasema Billgates hana taste ya vitu vizuri, hata OS yake ya ovyo tu, ila ni bahati tu business model yake imefanya kazi. Gates naye alikuwa anamdharau Steve anamuona kama ni kichaa tu.

Wakati apple inataka kumrudisha Jobs kazini, (Jobs japo alikuwa mwanzilishi wa apple, ila aliwahi kufukuzwa kazi na bodi ya wakurugenzi halafu wakamteua jamaa ambaye jobs ndiye alimleta mwenyewe apple).

Baada ya miaka mingi apple ikawa haifanyi vizuri wakaamua kumrudisha Jobs. Gates aliposikia alipiga simu apple akawambia hivi wamechanganyikiwa. Wanataka kumrudisha mtu ambaye hajui lolote kuhusu technology, wala hawezi kucode hata mstari mmoja wa program. Akasisitiza kwamba kama wataendelea kubisha watakuja kujuta mbeleni.

Jobs alimprove gates wrong baada ya kurudishwa aliiletea apple mafanikio makubwa kwa bidhaa safi, kama ipod, iphone, ipad, na piakubadili comp za mac kuwa bora sana.

Baadhi ya mambo ya kufurahisha kuhusu Jobs.
1. Jama alikuwa ana patent kila kitu hata ubunifu mdogo, mfano stair case zilizoko kwenye ofisi za apple zilizo tengenezwa kwa kioo, alizipatent. Staircase hizi uwa zinawavutia watu kuingia kwenye maduka yao kununua bidhaa.

2. Alikuwa anaamini katikaa kufanya vitu kwa usafi na umakini. Alikuwa akisema haifai kufanya kitu ovyo ovyo kwakuwa hakitaonekana. Mfano kabati kwakuwa upande wa nyuma utakuwa umetazama ukuta hivyo hakuna atakayeuoana, eti ndo utumie mbao mbovu mbovu na usipige rangi. Jobs hakuwa mtu wa hivyo.

3. Alikuwa akiendesha gari lisilokuwa na plate namba. Jobs alikuwa akiendesha gari aina ya Mercedes-Benz SL55 AMG. Sheria ya California inamruhusu mnunuzi wa gari kutumia gari kwa miezi sita pasipo kupachika plate number. Jobs alitumia hii nafasi kuwa ananunua gari na kuliendesha kwamiezi sita kisha anauza na kununua gari lingine same model same color.

4. Aliunda timu ya wataalamu kufanya research juu ya shauku (emotions) pale ambapo mteja anapokuwa akifungua box la bidhaa aliyonunua anajisikiaje. Ndiyo maana matokeo ya utafiti wao yakapelekea apple kutumia utaalamu mwingi katika kupack bidhaa zao. Hata box lazima liwe zuri na mpangilio bora.

5. Alikuwa akivaa simple sana. Alipendelea kuvaa jeans za levis na tisheti zenye collar ndefu. Inasemekana alikuwa na jeans zaidi ya 100 za levis ana sneaker.

6. Alitaka kubadili dini ya kuwa Mbudha baada ya kutembelea India. Na hii ilibadili mtazamo wake maisha yake yote.

Jobs amekuwa inspiration kwa wavumbuzi wadogo duniani kote. Amebadili mambo mengi. Alikuwa pia anajua marketing sana jamaa. Presentations zake wakati wa kuintroduce bidhaa ilikuwa za kipekee, ambapo naona makampuni mengi sasa yanafuata style hiyo.
 
Msipende kunizungumzia zungumzia mambo yangu, huwa sipendi.

Halafu kuhusu kurudishwa kazini na hao walio nifukuza si kweli. Hawakunirudisha kazini, waliponifukuza nilirudi kitaa nikasurubika sana baadaye nikaanzisha kampuni nyingine iliyotengeneza faida zaidi halafu nikaenda kuinunu apple sababu apple was my thing
 
Msipende kunizungumzia zungumzia mambo yangu, huwa sipendi.

Halafu kuhusu kurudishwa kazini na hao walio nifukuza si kweli. Hawakunirudisha kazini, waliponifukuza nilirudi kitaa nikasurubika sana baadaye nikaanzisha kampuni nyingine iliyotengeneza faida zaidi halafu nikaenda kuinunu apple sababu apple was my thing
Haukuinunua ulirudishwa kazini na makubaliano ikawa kwamba wata merge hizo kampuni mbili kwa kukupa hisa 1.5 million
 
Anayejua anajua tu, mjuba baada ya kuachishwa kazi aliunda kampuni ya kutengeneza animation jina pixar, ikaonyesha mafanikio.

Apple wakashtuka, maana kwa upande wao waliishaanza kuonyesha kufail, wakamuita tena jamaa.baada ya hapo apple haikuwahi kurudi chini tena.
 
'Yeye na Billgates walikuwa mahasimu wakubwa sana kila mmoja akimdharau mwenzake.

Mfano Steve Jobs alikuwa anasema Billgates hana taste ya vitu vizuri, hata OS yake ya ovyo tu, ila ni bahati tu business model yake imefanya kazi. Gates naye alikuwa anamdharau Steve anamuona kama ni kichaa tu.'

Na mwaka 1997 wkt Apple ikienda kufilisika Bill Gates ndiye aliyeikoa kwa kutoa $mil 150.,la sivyo Co. Ilikua inaenda korongoni.
 
'Yeye na Billgates walikuwa mahasimu wakubwa sana kila mmoja akimdharau mwenzake.
Mfano Steve Jobs alikuwa anasema Billgates hana taste ya vitu vizuri, hata OS yake ya ovyo tu, ila ni bahati tu business model yake imefanya kazi. Gates naye alikuwa anamdharau Steve anamuona kama ni kichaa tu.'

Na mwaka 1997 wkt Apple ikienda kufilisika Bill Gates ndiye aliyeikoa kwa kutoa $mil 150.,la sivyo Co. Ilikua inaenda korongoni.
Alitoa pesa ili kuzima kesi yake ya monopoly, na baadae alirudishiwa pesa zake
 
Nini kilimuua

Sent from my itel S31 using JamiiForums mobile app
Duh Mkuu asante kwa kutushtua mapaka tukamtafuta huyu marehemu tuisngemjua
Jobs was diagnosed with a pancreatic neuroendocrine tumor in 2003. He died of respiratory arrest related to the tumor at age 56 on October 5, 2011.
1605040436698.png
1605040652940.png
 
Kuna movie inaitwa pirates of silicon valley, inazungumzia maisha ya Steve na Bill. Steve alikuwa mtu wa ovyo sana , mjivuni balaa.
 
Msipende kunizungumzia zungumzia mambo yangu, huwa sipendi.

Halafu kuhusu kurudishwa kazini na hao walio nifukuza si kweli. Hawakunirudisha kazini, waliponifukuza nilirudi kitaa nikasurubika sana baadaye nikaanzisha kampuni nyingine iliyotengeneza faida zaidi halafu nikaenda kuinunu apple sababu apple was my thing
Du umepata wapi ujasiri wa kutoka kaburini na kuja kupost humu bwana jobs
 
anayejua anajua tu,mjuba baada ya kuachishwa kazi aliunda kampuni ya kutengeneza animation jina pixar,ikaonyesha mafanikio.

apple wakashtuka,maana kwa upande wao waliishaanza kuonyesha kufail,wakamuita tena jamaa.baada ya hapo apple haikuwahi kurudi chini tena.
Hakuinzisha, ila aliinunua ilikuwa ikijulikana kama Graphics group, akalipa dollar milion tano na kuwa major share holder wa hiyo kampuni na CEO. Mwaka 2006, Disney alikuja kuinunua Pixar kwa 7.5 billion dollars, yani robo/nusu ya budget ya tz kwa mwaka. Animation iliyotisha sana na ya kwanza kuitoa ilikuwa inajulikana kama Toy Story. Disney hawakuamini walichokiona.

Kampuni aliyoanzisha baada ya kkufukuzwa apple inajulikana kama NeXT ambayo ilikuwa ikitengeneza computer softwares, na computer kwa ajili ya mashule na taasisi za kiuchunguzi.

Apple baada ya juhudi zao za kutengeneza Mac Os ya maana kufail ndipo wakamrudia jobs, wakakubaliana wainunue NeXT na wampe share 1.5 million arudi apple kama advisor. So software za NeXT zilitumika kuiupgrade Mac. Baadae wakamfanya Jobs kurudi kwenye UCEO kabisa.
 
Nini kilimuua

Sent from my itel S31 using JamiiForums mobile app
Kansa ya Kongosho. Jamaa alikuwa mbishi sana, allipogundulika ana kansa wakataka afanyiwe operation akagoma akasema atapona kwa kufuata diet za wale watu wa youtube wa kula matunda. Mpaka anakuja kukubali ilikuwa ishafika stage mbaya sana. Manneo yake ya mwisho kabla ya kukata roho ilikuwa ni "Ow Oh, Ow Oh"
 
'Yeye na Billgates walikuwa mahasimu wakubwa sana kila mmoja akimdharau mwenzake.
Mfano Steve Jobs alikuwa anasema Billgates hana taste ya vitu vizuri, hata OS yake ya ovyo tu, ila ni bahati tu business model yake imefanya kazi. Gates naye alikuwa anamdharau Steve anamuona kama ni kichaa tu.'

Na mwaka 1997 wkt Apple ikienda kufilisika Bill Gates ndiye aliyeikoa kwa kutoa $mil 150.,la sivyo Co. Ilikua inaenda korongoni.
Hata Bilgates na Jobs pamojja na wa fanyakazi wa microsoft na apple walishirikiana kudevelope Office softwares kwa ajili ya Mac Os
 
Kuna movie inaitwa pirates of silicon valley, inazungumzia maisha ya Steve na Bill. Steve alikuwa mtu wa ovyo sana , mjivuni balaa.
Alikuwa ana kiburi sana na rude sana. Wafanyakazi walikuwa wanamuogopa na alikuwa ana watreat vibaya. We fikiria kwenye launch ya iphone ya kwanza alifire wafanyakazi tena waliotumia muda wao hawalali kuitengeneza iPhone.

Akiwa stejini akawa eti anaeleza, "Ukitaka kufuta majina kwenye phonnebook ni simple. Unaingia hapa unabonyeza hapa unafuta, akafanya hivyo mara tatu." kwa watazamaji walidhani anawaonyesha jinsi kutumia iPhone kulivyo simple, yale yalikuwa majina ya engineers wa apple, na hayo aliyofuta ilikuwa na maana they were fired.

Pia akiwa chuo alikuwa na maisha magumu, ila kuna manzi alimzimikia na akamkubari steve na maisha yake magumu ya kutooga na sometimes kutembea miguu peku. Alipompiga mimba akamkataa. Mpaka akiwa tajiri bado aliendelea hadi kumkataa mtoto wa la kumsaidia huyo mama mtoto wake. Na akawa anagoma kuwa yule si mtoto wake na aligoma hata kupima DNA.
 
Hata Bilgates na Jobs pamojja na wa fanyakazi wa microsoft na apple walishirikiana kudevelope Office softwares kwa ajili ya Mac Os
Hawakushirikiana ku-develop Ms Office kwa ajili ya MAC ila kilichotokea ni Gates kutoa $150mil akapewa Non-voting stocks na akaruhusu free access ya MS Os kwny apples na hii aliifanya baada ya kua ana kesi ya kufanya monopolization(kesi kama hizi hata facebook,google,Amazon wanazo) kitu ambacho kinakatazwa na sheria za US na baada ya kuwapa hio access Apple kesi zake zikafutwa baada ya muda kidogo maana ilionekana ha-monopolize soko tena.
 
Hawakushirikiana ku-develop Ms Office kwa ajili ya MAC ila kilichotokea ni Gates kutoa $150mil akapewa Non-voting stocks na akaruhusu free access ya MS Os kwny apples na hii aliifanya baada ya kua ana kesi ya kufanya monopolization(kesi kama hizi hata facebook,google,Amazon wanazo) kitu ambacho kinakatazwa na sheria za US na baada ya kuwapa hio access Apple kesi zake zikafutwa baada ya muda kidogo maana ilionekana ha-monopolize soko tena.
Mwaka 1997, Apple na microsoft waliingia deal la kushirikiana kutengeneza office kwa ajili ya Mac computers. Siongelei hiyo kesi bali naongelea kuwa kuna vitu waliwahi kushirikiana.
 
Alikuwa ana kiburi sana na rude sana. Wafanyakazi walikuwa wanamuogopa na alikuwa ana watreat vibaya. We fikiria kwenye launch ya iphone ya kwanza alifire wafanyakazi tena waliotumia muda wao hawalali kuitengeneza iPhone. Akiwa stejini akawa eti anaeleza, "Ukitaka kufuta majina kwenye phonnebook ni simple. Unaingia hapa unabonyeza hapa unafuta, akafanya hivyo mara tatu." kwa watazamaji walidhani anawaonyesha jinsi kutumia iPhone kulivyo simple, yale yalikuwa majina ya engineers wa apple, na hayo aliyofuta ilikuwa na maana they were fired.
Pia akiwa chuo alikuwa na maisha magumu, ila kuna manzi alimzimikia na akamkubari steve na maisha yake magumu ya kutooga na sometimes kutembea miguu peku. Alipompiga mimba akamkataa. Mpaka akiwa tajiri bado aliendelea hadi kumkataa mtoto wa la kumsaidia huyo mama mtoto wake. Na akawa anagoma kuwa yule si mtoto wake na aligoma hata kupima DNA.
Hii dark side yake inakua muted ila hakua na social capital kabisa.
 
Back
Top Bottom