Wild Flower
JF-Expert Member
- Jul 20, 2023
- 378
- 766
Fahamu mambo ya kuzingatia wakati unapoitwa kwa ajili ya Interview:
1. Fanya Utafiti kuhusu Kampuni iliyokuita kwa kufahamu Huduma na Maono yake ili majibu yako yalingane na malengo ya Kampuni
2. Elewa vizuri Majukumu ya nafasi uliyoiomba yaani (Job discription) ili uwe tayari kujadili jinsi uzoefu na ujuzi wako unavyolingana na Mahitaji ya Nafasi husika.
3. Chagua Mavazi yanayofaa kulingana na Kampuni husika. Hakikisha Nguo zako ni safi na zinakuwasilisha vizuri.
4. Fika Mapema eneo la Usaili angalau dakika 10-15 mapema kabla ya muda uliopangwa. Hii itaonesha Uadilifu na kukupa muda wa kupumzika na kuweka sawa fikra zako.
5. Jitayarishe kujibu Maswali ya Kawaida ya Usaili ikiwemo "Tuambie kuhusu wewe, Uwezo na udhaifu wako ni upi na Kwanini tukuajiri?"
6. Ikiwa umewahi kufanya Kazi awali, jiandae vizuri kuzungumzia Mafanikio ya majukumu yako ya awali. Toa mifano thabiti ya Ujuzi wako.
7. Si lazima sana kubeba Nyaraka za Vyeti vyako lakini ni muhimu kuwa navyo wakati huo, hasa kama uliambatisha nakala zake kwenye Maombi ya Kazi.
Muhimu zaidi: Usiongee vitu visivyohusiana na Maswali au Kujieleza kupita kiasi. Maelezo yako yawe mafupi, yenye kueleweka na yenye maana.
1. Fanya Utafiti kuhusu Kampuni iliyokuita kwa kufahamu Huduma na Maono yake ili majibu yako yalingane na malengo ya Kampuni
2. Elewa vizuri Majukumu ya nafasi uliyoiomba yaani (Job discription) ili uwe tayari kujadili jinsi uzoefu na ujuzi wako unavyolingana na Mahitaji ya Nafasi husika.
3. Chagua Mavazi yanayofaa kulingana na Kampuni husika. Hakikisha Nguo zako ni safi na zinakuwasilisha vizuri.
4. Fika Mapema eneo la Usaili angalau dakika 10-15 mapema kabla ya muda uliopangwa. Hii itaonesha Uadilifu na kukupa muda wa kupumzika na kuweka sawa fikra zako.
5. Jitayarishe kujibu Maswali ya Kawaida ya Usaili ikiwemo "Tuambie kuhusu wewe, Uwezo na udhaifu wako ni upi na Kwanini tukuajiri?"
6. Ikiwa umewahi kufanya Kazi awali, jiandae vizuri kuzungumzia Mafanikio ya majukumu yako ya awali. Toa mifano thabiti ya Ujuzi wako.
7. Si lazima sana kubeba Nyaraka za Vyeti vyako lakini ni muhimu kuwa navyo wakati huo, hasa kama uliambatisha nakala zake kwenye Maombi ya Kazi.
Muhimu zaidi: Usiongee vitu visivyohusiana na Maswali au Kujieleza kupita kiasi. Maelezo yako yawe mafupi, yenye kueleweka na yenye maana.