Tukiacha Yale mambo ya ujumla kama vile uhaba wa madaktari, dawa , vifaa n.k yafuatayo ni mambo nimejionea wakati namuuguza mdogo wangu aliyevunjika mguu
1. Vyoo vya wodini havina Maji
Yaani ni mpaka unashangaa kama upo hospitali ya Wilaya au zahanat ya Kijiji. Kama una mgonjwa inabidi uwe na ndoo na ukatafute Maji nje.. lakini hili linapelekea harufu kali wodini na uchafu chooni.
2. Kupata huduma weekend na wakati wa jioni ni changamoto..
Ni kama Magunga hospital wamekubaliana kwamba hakuna kuumwa wakati wa jioni au au siku za weekend!! Unaweza kuhangaika kutafuta daktari usimuone!
3. Mfumo wa mtandao kugawa dawa kwa baadhi ya manesi ni changamoto
Kuna mmoja alikuwa anagawa dawa hata kushika mouse inamsumbua! Mpaka unajiuliza nani kamuweka dukani!! Yaani watu wawili mnaweza kukaa masaa mawili au matatu kwa dawa chache tu!!
4. Huduma ya X-ray ni hadi utoe rushwa kidogo
Wanasema mtu wa x-ray ni mmoja tu hospital nzima kwa hiyo lazima 'kumlinda' na analindwa kweli!
5. Baadhi ya dawa unaweza tu kuambiwa hazipo ila mwingine akaambiwa zipo hususan ukiwa na bima!
6. Hakuna watu wanajua kulindana kama hawa jamaa wa Magunga!!
Unaweza kushuhudia kabisa dokta kapanda Bajaj au pikipiki kasepa lakini ukimuuliza nesi anakuambia yuko ofisini.
Nitaendelea
1. Vyoo vya wodini havina Maji
Yaani ni mpaka unashangaa kama upo hospitali ya Wilaya au zahanat ya Kijiji. Kama una mgonjwa inabidi uwe na ndoo na ukatafute Maji nje.. lakini hili linapelekea harufu kali wodini na uchafu chooni.
2. Kupata huduma weekend na wakati wa jioni ni changamoto..
Ni kama Magunga hospital wamekubaliana kwamba hakuna kuumwa wakati wa jioni au au siku za weekend!! Unaweza kuhangaika kutafuta daktari usimuone!
3. Mfumo wa mtandao kugawa dawa kwa baadhi ya manesi ni changamoto
Kuna mmoja alikuwa anagawa dawa hata kushika mouse inamsumbua! Mpaka unajiuliza nani kamuweka dukani!! Yaani watu wawili mnaweza kukaa masaa mawili au matatu kwa dawa chache tu!!
4. Huduma ya X-ray ni hadi utoe rushwa kidogo
Wanasema mtu wa x-ray ni mmoja tu hospital nzima kwa hiyo lazima 'kumlinda' na analindwa kweli!
5. Baadhi ya dawa unaweza tu kuambiwa hazipo ila mwingine akaambiwa zipo hususan ukiwa na bima!
6. Hakuna watu wanajua kulindana kama hawa jamaa wa Magunga!!
Unaweza kushuhudia kabisa dokta kapanda Bajaj au pikipiki kasepa lakini ukimuuliza nesi anakuambia yuko ofisini.
Nitaendelea