Mambo sita mapya niliyoyaona kwenye kikosi cha Simba kwa hivi karibuni

Mambo sita mapya niliyoyaona kwenye kikosi cha Simba kwa hivi karibuni

ToniXrated

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2022
Posts
1,134
Reaction score
2,993
Amani iwe nanyi

Katika siku za hivi karibuni mara baada ya Simba kumteua Master Guardiola Mgunda, nimeweza kugundua masuala kadhaa! Ungana nami uweze kuyajua mambo hayo.

1. Mzamiru amezaliwa upya, nikiri kuwa nilikuwa miongoni mwa watu waliokuwa wakikosoa sana uchezaji wa Mzamiru Yasin kutokana na mpira wake wa kupiga pasi fyongo, kurudisha mipira nyuma na kufanya mikimbio isiyokuwa na umuhimu. Toka Mgunda aingie Simba nimemuona mzamiru mpya.

Mzamiru wa sasa hana mambo mengi, anasafa uwanjani kukata umeme na pindi akiupata mpira amekuwa na maamuzi bora sana ya kuachia pasi zenye macho kwa mchezaji aliyekaribu naye. Hivi ndivyo kiungo mkabaji wa kati anatakuwa awe. Mzamiru ameongeza kujiamini uwanjani na kitete kimemtoka. Hongereni benchi la ufundi la simba kwa kumfanya mzamiru awe bora.

2. Kibu denis, licha ya kiwango chake cha kazi kuwa kikubwa uwanjani lakini bado anasumbuliwa sana na kutokuweza kufanya maamuzi sahihi anapokuwa na mpira. Hajui ni wakati gani anatakiwa akimbie na mpira na wakati gani anatakiwa atoe pasi na wakati gani apige shuti golini.

Kibu anatakiwa ajue kuwa Simba haimpi presha ya yeye kufunga kila mechi. Hivyo inampasa atulize mchecheto awapo uwanjani. Yote kwa yote nafurahishwa sana na uchezaji wake pindi anapokuwa hana mpira. Leo amemsaidia sana Israel Mwenda kwenye kukaba.

3. Safu ya ulinzi ikiwa chini ya kapteni Tshaba imetulia, hofu yangu ipo sana kwa Kennedy Juma, huyu jamaa sijui ni uzito wa mwili au nini, ila anaonekana anakosa kujiamini sana. Simba ilishatoka katika zama za butua butua. Tunataka tuweke boli chini ila kennedy akipata mpira huwa ni kubutua tu. Ajifunze utulivu na kujiamini kutoka kwa Kitasa Inonga Varane, Babu Onyango kama kawaida yake ni marufuku kucheka na nyau.

4. Putin kama Putin kwenye michezo mitatu iliyopita ameonesha kujiamini sana na utulivu umeongezeka kiwanjani, Nimependa ushirikiano wake na Mzamiru, leo walitawala dimba vilivyo.

5. Chama, Okrah na Generali Phiri waongezewe mikataba. Wana mengi ya kuisaidia Simba. Okrah ameziba pengo la Morison kabisa kiasi kwamba hatukumbuki kama tulikuwa na mchezaji anaitwa Bernard Morrison. Phiri na Chama sina haja ya kuwaelezea sana, wanayofanya uwanjani yanajieleza.

6. Israel Mwenda ni mchezaji anayeleta matumaini, kila siku anaendelea kukua bado ana muda wa kusahihisha makosa yake.


VAMOOOOOOOS SIMBAAAAAAAAA!!!
 
Natamani wachezaji wote wangeiga uchezaji wa Chama,chama anachezea nafasi yake vilivyo hana papara ya kufunga na ni mtoa pasi kwa wenzake yani ana moyo uliofunguka hana moyo wa uchoyo, lakini bado ni maarufu na ni mchezaji tegemezi.

Kuna wengine wabanizi wa pasi wanataka kufunga ili na wao waonekane hata kama hawako ktk angle nzuri mfano Kibu D.

Mimi nadhani kila mtu acheze nafasi yake kwa ushirikiano mzuri na kufunga kuje kama zali tuu mpira umeukuta kwny angle nzuri ya kushoot sio mtu anakimbizana na mpira mwanzo mwisho ananyima pasi ili tuu akafunge yeye mfano Sakho.
 
Yaani mashabiki wa SIMBA FC leo wote tuna raha isiyo na kifani. Kuna jamaa shabiki wa utopolo baada ya goli la 3 la Israel kwa hasira kaipiga ngumi chupa ya bia vidole vimechanika damu kama yote na bia zilizokuwa mezani zimemwagika, aliokaa nao wakamkomalia anunue bia alizomwaga bila kujali kuumia kwake. Kucheza acheze mwengine hasira awenazo utopolo hahaha
 
Yaani mashabiki wa SIMBA FC leo wote tuna raha isiyo na kifani. Kuna jamaa shabiki wa utopolo baada ya goli la 3 la Israel kwa hasira kaipiga ngumi chupa ya bia vidole vimechanika damu kama yote na bia zilizokuwa mezani zimemwagika, aliokaa nao wakamkomalia anunue bia alizomwaga bila kujali kuumia kwake. Kucheza acheze mwengine hasira awenazo utopolo hahaha

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]duh mwana kawaingiza hasara
 
Kwa kazi aliyoifanyaga Israel Patrick Mwenda kwenye mechi ya marudiano kati ya Simba na Holando pirates huko South, ni wazi nilijua Simba tumeshapata mbadala wa Shomari Kapombe huyu dogo kwa sasa ni beki bora sana, anakaba vizur anapandisha timu na anapiga Cross zenye macho.

Kinachoniuma ni kuwa akifanya makosa kidogo mashibiki wengi huwa wanamshukia kama mwewe hii tabia ni ya hovyo sana.
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]duh mwana kawaingiza hasara
Hahaha angelipa kama chupa isingempasua, tulimuonea huruma zaidi tulimcheka tu nakumwahisha dispensary ya jirani
 
Kwa ujumla wachezaji walicheza kitimu na mapungufu ni machache .
 
Kwa kazi aliyoifanyaga Israel Patrick Mwenda kwenye mechi ya marudiano kati ya Simba na Holando pirates huko South, ni wazi nilijua Simba tumeshapata mbadala wa Shomari Kapombe huyu dogo kwa sasa ni beki bora sana, anakaba vizur anapandisha timu na anapiga Cross zenye macho.

Kinachoniuma ni kuwa akifanya makosa kidogo mashibiki wengi huwa wanamshukia kama mwewe hii tabia ni ya hovyo sana.
Bila kumshukia angeendeleza ujinga wake.
Kwa kumsema sana ndio anakuwa makini sasa.

Na ole wake aharibu tena.
 
Natamani wachezaji wote wangeiga uchezaji wa Chama,chama anachezea nafasi yake vilivyo hana papara ya kufunga na ni mtoa pasi kwa wenzake yani ana moyo uliofunguka hana moyo wa uchoyo, lakini bado ni maarufu na ni mchezaji tegemezi. Kuna wengine wabanizi wa pasi wanataka kufunga ili na wao waonekane hata kama hawako ktk angle nzuri mfano Kibu D. Mimi nadhani kila mtu acheze nafasi yake kwa ushirikiano mzuri na kufunga kuje kama zali tuu mpira umeukuta kwny angle nzuri ya kushoot sio mtu anakimbizana na mpira mwanzo mwisho ananyima pasi ili tuu akafunge yeye mfano Sakho.
Watu wanadhani ili uimbwe ni lazima ufunge, kumbe hata ukitmiza tu majukumu ni lazima uonekane. Pela Simba Sc hakuna wa kuuchallange ufalme aliojiwekea CHANA labda kidogo Miquisonne aliyeondoka ambaye pila, misingi ya umaarufu wake ni kutimiza majukumu yake ya u-Winga, yule jamaa alikuwa ni winga asiyewaza kufunga kabisa.
 
Simba hii dirisha Dogo January atoke okwa aingie zemanga soze alaf nafasi ya dejan aingie lobi manzoki,.... aaaaah ubingwa Wa Africa huu hapa kabisa.
 
Back
Top Bottom