Mambo ya kiroho!! Roho ni nini?

raslimali

JF-Expert Member
Joined
Nov 4, 2014
Posts
1,958
Reaction score
1,744
Wahubiri wa imani ya Kikristo, ni muhimu kutoa maelezo fasaha mnapozungumzia masuala ya ulimwengu wa roho. Mara nyingi, unamsikia mhubiri akisema, "Naona katika ulimwengu wa roho..." lakini ni vema tukajiuliza, roho ni nini? Je, ninyi pia mmekaririshwa tu kwamba roho siyo kitu chenye asili ya kimaada?

Mnasema ni kitu kisichoonekana, lakini wakati huo huo mnahubiri kuwa Roho wa Mungu anakaa ndani ya mtu, au kwamba ndani ya mtu kuna roho. Pia mnasema kuwa mambo ya kiroho ni mambo ambayo akili ya binadamu haiwezi kuyaelewa.

Kauli kama hizi zinaweza kuonekana kama njia ya kujificha ili kufanikisha ajenda za siri. Ikiwa huwezi kufafanua roho ni nini, ni vyema usihubiri jambo ambalo huwezi kulielezea kwa ufasaha. Inakuwa ni kama kuongoza watu kwenye barabara ya giza.

Acheni kuidhalilisha imani. Yesu ni mwanga, siyo giza.
 
tunapigwa tu mkuu

ni utapeli. mtu pekee anayeweza kuona kwenye huo ulimwengu wa roho ni nabii wa Mungu, sio hawa wanaojipachika unabii

mtu hajipi unabii, Mungu ndo anampa mtu unabii. tena ukiangalia manabii wa kweli hawakuipenda hiyo kazi . waliigomea kwanza
 
Roho ni roho tu mkuu...kwani kumetokea nini
 
Mtoa mada ukikata Roho utajua Roho ni Nini na maombi ya kiroho yapoje
 
Ni loophole ya kutupiga tu kwa sababu hayo mambo kikawaida jamii haina uelewa nayo. Hata mambo yasiyo na logic kama uchawi yana-operate huko huko.
 
Mkuu hata manabii wa shetwani nao wanaona katika Roho, ila chafu. Kumbuka Jesus mwenyewe aliambiwa anafanya miujiza kwa nguvu za belzebuli.

Belzebuli kwa wayahudi alikuwa ni mkuu wa mapepo wachafu
 
Roho ni uzima ulio nao ambao hauonekani, ukifa hiyo roho inaenda kuungana na roho nyingine katika ulimwengu wa roho. Wanaosema wanaona ni uwongo labda ndoto tu. Kuona inabidi ufe, nani atakubali kufa?
 
Umejibu vema kabisa. Unabii siyo kitu cha kukimbilia au kujipachika kama haya matapeli ya leo. Nashukuru mamlaka zimeanza kusikiliza. Kuna tapeli moja limekimbizwa juzi. Ni mwanzo mzuri. Ila bado wako wengi. Nao wamulikwe. Nimesikia nchi jirani wana mpango wa kuweka sheria hawa matapeli wa kuuza visaidizi vya imani kama maji,mafuta,keki,vitambaa n.k washughulikiwe.
 
Roho ni roho tu mkuu...kwani kumetokea nini
Swali ni roho ni nini? Ni kama nikikuuliza mwanga ni nini ukaniambia ni electromagnetic waves na ukanipa na properties zake. Ukisema mwanga ni mwanga ndio umejibu nini??
 
Swali ni roho ni nini? Ni kama nikikuuliza mwanga ni nini ukaniambia ni electromagnetic waves na ukanipa na properties zake. Ukisema mwanga ni mwanga ndio umejibu nini??
Kwani wewe unaitaka roho ya nini🤒
 
Ni loophole ya kutupiga tu kwa sababu hayo mambo kikawaida jamii haina uelewa nayo. Hata mambo yasiyo na logic kama uchawi yana-operate huko huko.
Ndiyo nia yangu ni kuwafumbua macho watu waachane na huu usanii. Leo nilikuwa naongea na mkristo jirani yangu nikamuuliza kuna kitabu kwenye biblia kinaitwa kitabu cha mtume Ernest umewahi kukisoma akasema bado ila atakipitia,,😁🤣. Yaani hawa wakristo wanaomiminika kwenye haya makanisa uchwara hata hiyo biblia hawaijui. Ni makondoo yanayopelekwa machinjoni tu.
 
Taasisi yenye nguvu ulimwenguni ni suhulishi ya mambo yote duniani
Ewe mwanamke kwanini uteseke duniani wakati msaada upo
Uwe na miaka 25 -45
Uwe mwanamke shupavu
Uwe na kazi yako binafsi au kipaji chako/ usiwe umeajiriwa uwe unajitegemea katika utafutaji wako mwenyewe.
Uwe tayari kuchinja mbuzi wakubwa 5 kama sehemu ya kiapo.
Utapewa bilioni 2.5 kama sehemu ya mtaji wako.
Njoo utajirike Sasa umaskini ni mbaya na unatesa.
 
Ni
Ni utapeli tu hawana tofauti na waganga.

Ukimuuliza huko ulimwengu wa roho ndio wapi anabaki kubabaika tu na bla bla nyingi
 
Utapeli
 
Wakija kushtuka ni too late.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…