Mambo ya kutatanisha katika jamii kuhusu watu wenye upungufu wa akili

Mambo ya kutatanisha katika jamii kuhusu watu wenye upungufu wa akili

Mkuu nadhani uliileta hii kama utani lakini nataka kuiunga mkono ifuatavyo.

(Miaka ya late 80s na early 90s kulikuwa na kundi kama hili - likiitwa Tanzanet, na nafikiri ndio chanzo cha hii JF. Katika kundi hilo nilitoa mada kama hii kuhusu ukichaa - katika mjadala wa death penalty. Wale tuliokuwa nao enzi zile kama wakipitia hapa wanaweza kuongeza. Lakini msitoe identity yangu)

Ukichaa ni scale.
Sisi sote tuna ukichaa wa aina fulani.

Tunaojiita sisi ni wa kawaida ni kwa kuwa ukichaa wetu ni wa kawaida au wa wastani. Wale ambao ukichaa wao ni chini ya wastani basi tunawaita "wapole, hawana ghadhabu, wala hawajikuzi, nk." Wale ambao ukichaa wao ni zaidi ya wastani tunasema wale "machachari, utamjua tu akiingia hapa, wamezidi ngebe, nk." Wale wenye ukichaa ulikubuhu basi saa nyingine inabidi wafungwe kamba au kupewa madawa watulie.

Tunachoita ukichaa ni chemical imbalance kwenye ubongo. Hawa watu hawana tofauti na sisi ("normal" people). Wakipatiwa matibabu muafaka wana hisia zote tulizokuwa nazo sisi "wazima".

Tatizo moja ni kuwa society is very cruel. Watu wakishakujua au kuelezwa kuwa wewe ni mkichaa basi huponi tena!

Kwa sababu, siku ukifurahi na kucheka sana watu wataangaliana na kuulizana "vipi anarudiwa nini?" Ukiwa mkimya siku hiyo watu wataulizana tena, "vipi amekunya dawa zake?"

Jamii ikishakuita wewe ni mkichaa kwa kweli huponi tena. Salama yako ni kuhama mji au nchi.


Disclaimer:
Mimi sio medical doctor. Wenye taaluma zao wanaweza kuja hapa na kunichana chana vipande. Ninachokielezea hapa ni experience yangu katika maisha.

Kama ukichaa ni 'scale', hiyo scale ikoje? Kama ni kama ile ya number line haswa kuanzia zero kwenda juu basi kuna wengine sio vichaa kabisa yaani wale ambao wataangukia kwenye zero kwenye hiyo scale.
 
Kama ukichaa ni 'scale', hiyo scale ikoje? Kama ni kama ile ya number line haswa kuanzia zero kwenda juu basi kuna wengine sio vichaa kabisa yaani wale ambao wataangukia kwenye zero kwenye hiyo scale.


Mkuu Mwanamayu hiyo picha hapo juu inaonesha mtawanyiko wa takwimu wa kawaida (kama wewe ni statistician naomba msamaha lakini hapa nitaandika kana kwamba hujajifunza takwimu).

Sasa hapo penye sifuri ndio wastani (mean). Kwa hiyo kama wewe ubongo wako (uwiano wa kemikali au chemichal balance) uko hapo kwenye sifuri basi wewe ni mtu wa kawaida. Lakini hata watu waliopo kati ya -10 na +10 bado tunajiita watu wa kawaida na wengi wetu tupo hapo.

Watu waliopo kati ya +10 na +20 tunasema wao ni machachari (hyper au eccentric), na wale ambao wapo 20+ tunasema ni vichaa au wanahitaji huduma maalumu kama vile madawa.

Kwa upande mwengine, wale waliopo kati ya -10 na -20 tunasema ni wapole au slow, na wale ambao ni chini ya -20 tunasema ni taahira.

Nikukumbushe tu kuwa mimi sio mtaalam wa tiba za hawa wagonjwa wa akili. Wenye taaluma zao wanaweza kuja hapa na kutupa darasa.

Ninachokielezea hapa ni a very simple statistical categorization ya hawa watu tunaowaita VICHAA!
 
Vichaa wanaumwa na wanakufa Kama watu wengine, ulishawahi kwenda kwa kichaa ukamuuliza Kama anaumwa au la? Vichaa wapo very few mkuu to notice kuumwa kwao, kwan Wewe unauhakika na kila unachokula kwamba ni kisafi (unless ur rich)



Ulishawahi kutembelea milembe hosp iliyoko Dodoma ukauliza statistics za vifo vya wagonjwa wao?
Usidhan kwamba utakaa ndani na mtu akakuletea taarifa za kifo cha kichaa! Vichaa wanakufa na wengi wao wanazikwa na manispaa kwasababu hakuna ndugu wanaotokea.

Mkuu vitu kama hasira, mapenzi, matamanio etc umeshasema akili zao zimechanganyikiwa atajuaje kama hili tako zuri au la kama hata ugali uliotupwa na msafi hawezi kutofautisha??

bora usingechangia.mtoa mada anazungumzia vichaa tulionao mitaani wewe unaleta habari za milembe.
 
Mkuu nadhani uliileta hii kama utani lakini nataka kuiunga mkono ifuatavyo.

(Miaka ya late 80s na early 90s kulikuwa na kundi kama hili - likiitwa Tanzanet, na nafikiri ndio chanzo cha hii JF. Katika kundi hilo nilitoa mada kama hii kuhusu ukichaa - katika mjadala wa death penalty. Wale tuliokuwa nao enzi zile kama wakipitia hapa wanaweza kuongeza. Lakini msitoe identity yangu)

Ukichaa ni scale.
Sisi sote tuna ukichaa wa aina fulani.

Tunaojiita sisi ni wa kawaida ni kwa kuwa ukichaa wetu ni wa kawaida au wa wastani. Wale ambao ukichaa wao ni chini ya wastani basi tunawaita "wapole, hawana ghadhabu, wala hawajikuzi, nk." Wale ambao ukichaa wao ni zaidi ya wastani tunasema wale "machachari, utamjua tu akiingia hapa, wamezidi ngebe, nk." Wale wenye ukichaa ulikubuhu basi saa nyingine inabidi wafungwe kamba au kupewa madawa watulie.

Tunachoita ukichaa ni chemical imbalance kwenye ubongo. Hawa watu hawana tofauti na sisi ("normal" people). Wakipatiwa matibabu muafaka wana hisia zote tulizokuwa nazo sisi "wazima".

Tatizo moja ni kuwa society is very cruel. Watu wakishakujua au kuelezwa kuwa wewe ni mkichaa basi huponi tena!

Kwa sababu, siku ukifurahi na kucheka sana watu wataangaliana na kuulizana "vipi anarudiwa nini?" Ukiwa mkimya siku hiyo watu wataulizana tena, "vipi amekunya dawa zake?"

Jamii ikishakuita wewe ni mkichaa kwa kweli huponi tena. Salama yako ni kuhama mji au nchi.


Disclaimer:
Mimi sio medical doctor. Wenye taaluma zao wanaweza kuja hapa na kunichana chana vipande. Ninachokielezea hapa ni experience yangu katika maisha.

kweli tumepata uzoefu wako alichojifunza ktk maisha bt ni irrelevant na mada kwani mtoa mada ame specify kabisa kichaa wa aina gani!
 
Tofauti yao ni nini? wa milembe Dodoma wanatokea wapi?? Ukichaa ni ugonjwa kama ugonjwa mwingine, ni imani potofu kuanza kuamini kwamba huwa wanavanish ilhali haupo interested nao.

ww jamaa unaanza kuwa kichaa bado kuokota makopo uelewa wako mfinyu sana.
 
Hakuna tofauti ya kichaa Wa Milembe na yule Wa mitaani

utofauti upo wa mtaani sometime analala nje na anakula chakula kichafu ila wa milembe anakula chakula kizur na analala pazuri.
Wa milembe wanatumia dawa,wa mitaani hawatumi dawa.
Aliye maliza diploma na mwingine degree wote wanaitwa wasomi tofauti ni kwenye level ipi ya usomi.
 
kweli tumepata uzoefu wako alichojifunza ktk maisha bt ni irrelevant na mada kwani mtoa mada ame specify kabisa kichaa wa aina gani!


Nafikiri ni relevant. Fikiria hivi:

Chukua kila swali alilouliza muweka mada halafu uliulize kwa sisi watu wa "kawaida au wasio vichaa" na uone kama halina relevance. Nitayarudia maswali yake hapa chini:

1. Ni kwanini hawapati magonjwa hasa kama kipindupindu; hii ni kutokana na mazingira waishio kuwa machafu na hata vyakula wanavyookota na kula.

2. Sijawahi kusikia kichaa kafa kwa kuumwa zaidi ya kusikia labda kauliwa, zaidi ni kuwa huwa wanapotea tu ghafla na pengine asirudi tena na akipotea ni vigumu kuja kumuona mkoa mwingine.

3. Ningepnda kufahamu, je kutokana na hali zao inawezekana kuwa kuna hali fulani hawahisi kama watu wa kawaida? mfano njaa, hasira, huruma, uchungu na mengineyo.

4. Je, wanapata hamu ya kufanya mapenzi? Hapa nieleweke kuwa kuna vishawishi pengine kwa kumuona mtu na kuvutiwa kufanya nae hilo tendo.


Swali la kwanza: Tunaweza kuuliza "ni kwa nini watu wa kawaida wengine (ambao sio vichaa lakini ni homeless) hawapati magonjwa kama kipindupindu?" nk.

Kila swali hapa tunaweza kuliuliza kwa watu kama sisi tunaojiita wa "kawaida au sio vichaa".

Kwa mfano swali la nne, unafikiri kwa nini VIAGRA ina soko kubwa sana kwa sisi tunaojiita sio "vichaa"?

(Nafikiri umekwisha sikia wale vichaa wa ngono au sex maniacs. Tafakari, je wao ni tofauti na sisi "wazima" katika maswala ya mapenzi?)
 
Back
Top Bottom