Mambo ya kuzingatia kabla ya kupaka vipodozi

Mambo ya kuzingatia kabla ya kupaka vipodozi

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2009
Posts
42,872
Reaction score
34,363
KWA UFUPI

  • Hivyo, inakupasa kufanya utafiti ili kubaini ni make up ipi sahihi na haina madhara katika ngozi yako.



Vipodozi au ‘Makeups’ ni urembo unaopendwa zaidi na wanawake wengi, dhamira yao ikiwa kubadili mwonekano wao uliozoleleka ili wapendeze.

Mara nyingi watu wanapopaka make up tofauti hujitokeza usoni kutokana na kipodozi hicho kufanya kazi ya kung’arisha na kupendezesha uso.

Unapofika wakati wa kupaka make up, kwanza unapaswa kuchagua ni ipi itakufaa na kukupendeza. Swali la kama kipi kitafaa zaidi kati ya poda au cream, hilo linabaki kwa mhusika kwa kuwa kila mmoja anapendekezo lake, kutokanana namna anavyopata matokeo mazuri.

Mambo ya kuzingatia kabla hujapaka make up!

Kwanza jaribu kutafuta make up itakayoendana na ngozi yako na rangi ya mwili wako. Usipake aina yoyoe ya make up eti kwa sababu umeiona kwa mwenzio amepaka na amependeza kwani kila mmoja ana rangi yake na huenda anayotumia mwenzio ikawa na madhara katika ngozi yako.

Hivyo, inakupasa kufanya utafiti ili kubaini ni make up ipi sahihi na haina madhara katika ngozi yako. Watu wenye ngozi za mafuta wanashauriwa kupaka make up ya poda au ungaunga kwani cream inaweza kuziba vitundu vya hewa katika ngozi ya uso, hatimaye kusababisha chunusi kuonta.

Kwa walio na ngozi kavu wafahamu kuwa, make up ya cream haina uwezo wa kukaa muda mrefu katika ngozi, hivyo ikiwa unahitaji iendelee kuonekana kwa muda usiopungua saa nane ni vyema ukapaka make up ya poda iliyozeleka na wengi.

Jambo jingine la kutilia msisitizo ni namna ya kupaka aina zote mbili za make up, inashauriwa make up ya poda au unga ipakwe kwa brashi zake maalumu, siyo mikono wala kitambaa chochote ambacho hakijawekwa mahususi kwa kazi hiyo.

Ila kwa upande wa make up ya cream au majimaji, inapaswa kupakwa kwa mikono na kusambazwa katika uso wote, ili kuwe na ulinganifu katika eneo hili linalohusudiwa zaid na wanawake.

Imeandaliwa na Elizabeth Edward

lizzyedu@gmail.com

Chanzo.Mambo ya kuzingatia kabla ya kupaka vipodozi - Makala - mwananchi.co.tz
 
hii sasa ilipaswa iwe na ka sub forum kake.... Invisible unaona lakini......?
 
Last edited by a moderator:
Waangalie na expiry date pia kwenye hizo makeup!Na kawaida baada ya mwaka unatakiwa utupe vipodozi haswa vya macho,wanja,eyeshadow,eyeliner!!
 
Waangalie na expiry date pia kwenye hizo makeup!Na kawaida baada ya mwaka unatakiwa utupe vipodozi haswa vya macho,wanja,eyeshadow,eyeliner!!

Wacha bana......wanja wangu wa Rimmel unasema niutupe.......?...haya niambie kama unajua hapa bongo nitaununua wapi mwingine.........
 
Wacha bana......wanja wangu wa Rimmel unasema niutupe.......?...haya niambie kama unajua hapa bongo nitaununua wapi mwingine.........
Niko serious dadaangu uwe makini sana na vipodozi vya macho kwasababu hakuna preservatives zinazolast so long...Mfano mdogo dawa za macho zote ukitumia baada ya mwezi tu unatakiwa utupe kwasababu kutakuwa na growth of microorganisms!Na pia wengi wetu tunashare hivo vipodozi ni hatari sana!!Kitu kingine ni Mascara kama unatumia kila siku baada ya miezi 3-6 unatakiwa utupe au unaweza upate eyeinfection kama nilivyosema awali kunakuwa na growth of microorganisms(bacteria).
Mi sijui huo wanja utaupata wapi labda nimuulize Heaven on earth!!
 
Niko serious dadaangu uwe makini sana na vipodozi vya macho kwasababu hakuna preservatives zinazolast so long...Mfano mdogo dawa za macho zote ukitumia baada ya mwezi tu unatakiwa utupe kwasababu kutakuwa na growth of microorganisms!Na pia wengi wetu tunashare hivo vipodozi ni hatari sana!!Kitu kingine ni Mascara kama unatumia kila siku baada ya miezi 3-6 unatakiwa utupe au unaweza upate eyeinfection kama nilivyosema awali kunakuwa na growth of microorganisms(bacteria).
Mi sijui huo wanja utaupata wapi labda nimuulize Heaven on earth!!

hahaaa mimi49 kumbe haya mambo yako hivi!!!!!!!!!

akitaka aniambie ntamtafutia tu..........
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom