jerrytz
JF-Expert Member
- Oct 10, 2012
- 5,975
- 4,266
Mara kadhaa nimeona mijadala humu kuhusiana na single mothers, kwa wengi imekuwa ni ushujaa kuwasema vibaya hawa wanawake wenye mtoto ama watoto na kwa kweli walioamua kulea watoto wao bila uwepo wa baba.
Kuwa single mother sio kilema, sio upungufu wa akili ni matokeo tu ya maisha, kifo ama sababu nyingine yoyote.
Sahau kuhusu ulichosikia ama ulichoamini kuhusu single mothers, hawa ni wanawake kama walivyo wanawake wengine. Kama kiimani ama kwa jamii unayotoka hutakiwi kuwa na mahusiano na single mother basi hilo baki nalo moyoni lakini hakuna ushujaa katika kuwasema vibaya na kuwadharau.
Hii ni topic maalum kwa wanaume ambao wameingia kwenye mahusiano na single mothers ili waweze kujua mambo ya msingi wakati wanafurahia mapenzi motomoto kutoka kwa hawa viumbe.
Kuwa kwenye mahusiano na mwanamke mwenye mtoto inaleta uzoefu mpya wa kimahusiano - life experience na kwa kweli mara kadhaa hawa single mothers huwa partners bora kabisa.
Naomba kuweka wazi kwa mimi ni baba wa watoto wawili na mke niliyenaye sio single mother; naandika huu uzi kwa kuwa tu nimeona sasa jamii yetu inaona ni ushujaa kuwasema vibaya hawa single mothers.
Sasa wewe mwanaume, zingatia mambo yafuatayo:
1. Tambua kuwa itakuwa tofauti
Unapoingia kwenye mahusiano na single mother tambua kuwa mahusiano yenu hayatakuwa sawa na kuwa na mahusiano na mwanamke ambaye hana mtoto. Hata sisi wanaume wenye ndoa tunatambua kuwa mkeo baada ya kuzaa na kupata mtoto hawezi kuwa sawa na mwanamke huyohuyo kabla ya kuzaa.
Hapa sasa tarajia huyu mwanamke kuhusisha mahusiano yenu na mtoto wake, huyu ni mtoto wake na ni sehemu ya maisha yake lazima mara kadhaa atakuwa sehemu ya mahusiano yenu. Kwa mfano anaweza kukuomba kwenda naye shuleni kwa mtoto wakati wa visiting days ama siku nyingine.
Jambo lingine tofauti kwa single mothers ni kuwa wapo wazi sana kwa kitu wanachohitaji, yaani hawa hawana muda wa kusitasita, kama jambo analitaka atasema na kama kitu hakipendi pia atasema kwa sauti ya wazi kabisa. Hii ni moja ya attractive quality ya single mothers.
2. Kubali kwamba mtoto wake ni Her First Priority
Kwa single mothers, mtoto wake huwa ndio kipaumbele chake cha kwanza; na hakuna tatizo katika hilo. Ni human nature tu kukipa kipaumbele kitu ambacho unakiona ni cha thamani zaidi katika maisha.
Ni muhimu kwa mwanaume uelewe hili na ukubali kama unataka kufurahia maisha na single mother.
A parent's devotion to their children is admirable, and embracing it can help enrich the relationship and prevent you from becoming jealous.
Ni muhimu kwa mwanaume kuheshimu hilo na kuruhusu huyu mwanamke afanye maamuzi bila kuhisi kuwa hujali mtoto/watoto wake.
Ukimwachia uhuru wa namna hii yeye pamoja na mtoto wake watakuwa comfortable kukukaribisha katika maisha yao.
Ikiwa hauna uhakika wa aina ya mahusiano unayotaka kati yako na mtoto wake basi uwe na uwazi tangia mwanzoni. Hapa sio unaanza kumzoea mtoto kwa kasi ili upate nafasi ndani ya moyo wa mama yake halafu ukishapata nafasi unamsahau mtoto. Inawezekana mtoto anakuangalia kama father figure na kwa muda mfupi umeshamzoesha baadhi ya mambo na yeye amekuzoea.
Zingatia mwongozo wa single mother mwenyewe katika kuanzisha hayo mahusiano na watoto wake.
Ni muhimu sana kuzingatia kuyapa muda mahusiano yako na single mother ili yaende vizuri, usikimbilie kuwa mzazi mwenza wa watoto wake kwa kuchukua majukumu ya ubaba, usikurupuke kuhamia kwake au yeye kuhamia kwako wakati bado akili yako haijafanya maamuzi. Take it slow bother.
Chukua muda wako kutengeneza penzi na kujenga imani kabla ya kuyapeleka hayo mahaba yenu kwenda next level.
Unataka nini kwenye mahuasiano yako na huyu single mother? Je unataka mahusiano ya muda mfupi au mrefu na huyu mwanamke? Je kichwani kwako unaona ndoa?
Je unajiona ukiwa baba mwenye upendo kwa mtoto/watoto wa huyu mwanamke? Je upo tayari kushiriki malezi ya mtoto wa huyu mwanamke?
Wanawake wengi wenye watoto huwa wanataka kujua ni commotment gani utatoa kwenye mahusiano yako na wao.
Vyovyote ilivyo ni muhimu sana kuwa mkweli na muwazi mwamzoni kabisa wa mahusiano hayo ili kila mmoja ajue mlengo wa mahusiano yenu.
Uwazi na ukweli utakupa faida ya kufurahia penzi na huyu mwanamke bila kuwa na mawazo.
Sasa hapa wewe mwanaume uwe mtu wa kusikiliza na kutoa emotional support. Sio wewe ni mtu wa kuuliza tu kama ana nafasi ili ukajilie tunda, uwe na muda wa kumsikiliza na walau kutatua changamoto anazokabiliana nazo katika maisha.
Mfanye kuwa huru kuongea na wewe katika mambo ambayo yanahitaji mawazo ya mwanaume. Sikiliza zaidi, mtiwe moyo na mfanye maamuzi pamoja.
Embu pandisha viwango vyako kwa kuamua kuwa trustworthy kwa huyu mwanamke.
Uaminifu ni msingi muhimu katika kila aina ya mahusiano. Unaweza ukajenga msingi huu kwa kuwa reliable partner na kwa kutunza ahadi huku ukizingatia ustawi wa penzi lenu.
Mambo ya kuzingatia yapo nane; kwa leo tuishie hapa.
Tutaendelea kesho..
Kuwa single mother sio kilema, sio upungufu wa akili ni matokeo tu ya maisha, kifo ama sababu nyingine yoyote.
Sahau kuhusu ulichosikia ama ulichoamini kuhusu single mothers, hawa ni wanawake kama walivyo wanawake wengine. Kama kiimani ama kwa jamii unayotoka hutakiwi kuwa na mahusiano na single mother basi hilo baki nalo moyoni lakini hakuna ushujaa katika kuwasema vibaya na kuwadharau.
Hii ni topic maalum kwa wanaume ambao wameingia kwenye mahusiano na single mothers ili waweze kujua mambo ya msingi wakati wanafurahia mapenzi motomoto kutoka kwa hawa viumbe.
Kuwa kwenye mahusiano na mwanamke mwenye mtoto inaleta uzoefu mpya wa kimahusiano - life experience na kwa kweli mara kadhaa hawa single mothers huwa partners bora kabisa.
Naomba kuweka wazi kwa mimi ni baba wa watoto wawili na mke niliyenaye sio single mother; naandika huu uzi kwa kuwa tu nimeona sasa jamii yetu inaona ni ushujaa kuwasema vibaya hawa single mothers.
Sasa wewe mwanaume, zingatia mambo yafuatayo:
1. Tambua kuwa itakuwa tofauti
Unapoingia kwenye mahusiano na single mother tambua kuwa mahusiano yenu hayatakuwa sawa na kuwa na mahusiano na mwanamke ambaye hana mtoto. Hata sisi wanaume wenye ndoa tunatambua kuwa mkeo baada ya kuzaa na kupata mtoto hawezi kuwa sawa na mwanamke huyohuyo kabla ya kuzaa.
Hapa sasa tarajia huyu mwanamke kuhusisha mahusiano yenu na mtoto wake, huyu ni mtoto wake na ni sehemu ya maisha yake lazima mara kadhaa atakuwa sehemu ya mahusiano yenu. Kwa mfano anaweza kukuomba kwenda naye shuleni kwa mtoto wakati wa visiting days ama siku nyingine.
Jambo lingine tofauti kwa single mothers ni kuwa wapo wazi sana kwa kitu wanachohitaji, yaani hawa hawana muda wa kusitasita, kama jambo analitaka atasema na kama kitu hakipendi pia atasema kwa sauti ya wazi kabisa. Hii ni moja ya attractive quality ya single mothers.
2. Kubali kwamba mtoto wake ni Her First Priority
Kwa single mothers, mtoto wake huwa ndio kipaumbele chake cha kwanza; na hakuna tatizo katika hilo. Ni human nature tu kukipa kipaumbele kitu ambacho unakiona ni cha thamani zaidi katika maisha.
Ni muhimu kwa mwanaume uelewe hili na ukubali kama unataka kufurahia maisha na single mother.
A parent's devotion to their children is admirable, and embracing it can help enrich the relationship and prevent you from becoming jealous.
Ni muhimu kwa mwanaume kuheshimu hilo na kuruhusu huyu mwanamke afanye maamuzi bila kuhisi kuwa hujali mtoto/watoto wake.
Ukimwachia uhuru wa namna hii yeye pamoja na mtoto wake watakuwa comfortable kukukaribisha katika maisha yao.
3. Peleka mambo taratibu
Unapoanza mahusiano na single mother usiwe na haraka wala papara kwake wala kwa watoto wake.Ikiwa hauna uhakika wa aina ya mahusiano unayotaka kati yako na mtoto wake basi uwe na uwazi tangia mwanzoni. Hapa sio unaanza kumzoea mtoto kwa kasi ili upate nafasi ndani ya moyo wa mama yake halafu ukishapata nafasi unamsahau mtoto. Inawezekana mtoto anakuangalia kama father figure na kwa muda mfupi umeshamzoesha baadhi ya mambo na yeye amekuzoea.
Zingatia mwongozo wa single mother mwenyewe katika kuanzisha hayo mahusiano na watoto wake.
Ni muhimu sana kuzingatia kuyapa muda mahusiano yako na single mother ili yaende vizuri, usikimbilie kuwa mzazi mwenza wa watoto wake kwa kuchukua majukumu ya ubaba, usikurupuke kuhamia kwake au yeye kuhamia kwako wakati bado akili yako haijafanya maamuzi. Take it slow bother.
Chukua muda wako kutengeneza penzi na kujenga imani kabla ya kuyapeleka hayo mahaba yenu kwenda next level.
4. Kuwa mkweli na muwazi
Kuwa mkweli na muwazi ni jambo la muhimu sana.Unataka nini kwenye mahuasiano yako na huyu single mother? Je unataka mahusiano ya muda mfupi au mrefu na huyu mwanamke? Je kichwani kwako unaona ndoa?
Je unajiona ukiwa baba mwenye upendo kwa mtoto/watoto wa huyu mwanamke? Je upo tayari kushiriki malezi ya mtoto wa huyu mwanamke?
Wanawake wengi wenye watoto huwa wanataka kujua ni commotment gani utatoa kwenye mahusiano yako na wao.
Vyovyote ilivyo ni muhimu sana kuwa mkweli na muwazi mwamzoni kabisa wa mahusiano hayo ili kila mmoja ajue mlengo wa mahusiano yenu.
Uwazi na ukweli utakupa faida ya kufurahia penzi na huyu mwanamke bila kuwa na mawazo.
5. Uwe mtu wa kutoa Emotional support
Single moms wanapitia au wamewahi kupitia stress ama pressure kwenye malezi, na ukweli ni kwamba wanadamu wote tunapitia stress na presure mara kadhaa katika safari ya maisha yetu.Sasa hapa wewe mwanaume uwe mtu wa kusikiliza na kutoa emotional support. Sio wewe ni mtu wa kuuliza tu kama ana nafasi ili ukajilie tunda, uwe na muda wa kumsikiliza na walau kutatua changamoto anazokabiliana nazo katika maisha.
Mfanye kuwa huru kuongea na wewe katika mambo ambayo yanahitaji mawazo ya mwanaume. Sikiliza zaidi, mtiwe moyo na mfanye maamuzi pamoja.
6. Kuwa mtu Mwaminifu
Hawa wanawake wengi huko nyuma wamepitia uzoefu wa kukutana na watu ambao sio waaminifu, na kwa wengi hata kulea mtoto mwenyewe kama single parent ni kwa sababu ya kukutana na mtu ambaye hakuwa mwaminifu. Huna sababu ya kumkumbusha jinamizi kwa kutokuwa mwaminifu, kuwa mwaminifu kwake ili ajue kuwa bado kuna wanaume waaminifu.Embu pandisha viwango vyako kwa kuamua kuwa trustworthy kwa huyu mwanamke.
Uaminifu ni msingi muhimu katika kila aina ya mahusiano. Unaweza ukajenga msingi huu kwa kuwa reliable partner na kwa kutunza ahadi huku ukizingatia ustawi wa penzi lenu.
Mambo ya kuzingatia yapo nane; kwa leo tuishie hapa.
Tutaendelea kesho..