Mambo ya kuzingatia uwapo safarini

Mambo ya kuzingatia uwapo safarini

Ndo maana unamtetea ushoga kumbe na wewe ni nanii
Acha dharau hakuna unachojua kuhusu mimi,hizo ni hisia zako tu....mimi ni mwanaume tena baba wa familia na wanangu wanapata mahitaji kama katiba inavyotaka
 
Umenikumbusha one time kuna huyu binti kwenye basi la mkoa alileta huu uswahili. Amepanda kwenye basi amevaa jeans, sweater, na kablouse. Basi hana hata pochi yaani yupo kisela sana.

Kilichotokea ni period ilimuanza ghafla bila kujua. Kilichofanya nijue ni alivua sweater lake na kulitumia kama kujifunika sasa mimi nilikuwa na sweater na zile shuka za kimasai. Nikamuuliza mbona umevua sweeter na gari wamewasha AC haikutesi?!

Akajibu kama vile mtu mwenye mawazo na aibu fulani. Ilinichukua dakika chache kunotice kuwa hakuwa sawa na nikashajua huyu ametumia sweater kujificha. Nikamwambia kwa sauti ya chini sana unahitaji msaada. Hakunijibu zaidi ya kuinama kama anaona aibu halafu anaweka lile tabasamu la aibu fulani.

Nikamwambia niandikie kwenye sms unataka msaada gani. Nikampa simu yangu aandike namba yake nikamtext akaanza kuchat akanambia ameingia Period hapo hana uhakika na kinachoendelea ila anahisi amechafua siti sasa hajui pa kuanzia.


Aiseee ni MUNGU tu alisimamia ile situation maana gari lilikuwa na utingo mwanaume tu. So ikabidi nimfuate nimpange kuwa atusaidie wakiona hata kituo cha mafuta wasimame konda akanielewa. Tukasimama akasema abiria tuchimbe dawa kidogo. Watu wakaanza shuka. Akachukua sweta akaliweka pale kwenye siti halafu nikampa shuka langu la kimasai akajifunika mwili mzima so muda tunatoka nashuka nae hakuna mtu alishtukia chochote hadi tunafika chini. Nikamwambia atangulie chini me nakwenda tafuta pedi. Nikaenda mnunulia duka liko huko barabarani kipande kidogo toka pale kwenye sheri nikamletea.

Akajiweka sawa suruali yake ilikuwa imechafuka akaisuuza na maji akavaa hivyo hivyo nikamwambia valia na hilo shuka la kimasai. Tukarejea kwenye gari. Aisee ikawa kama ni mke wangu sasa namna tulivyorudi na kukaa kwenye gari alijiegemesha kwenye kioo me namwambia niegemee kama unataka kulala.

Tulishuka sote stand ya Moshi alikuwa anataka kwenda nikamwambia sidhani kama utakuwa katika hali nzuri kuendelea na safari katika hali hiyo na muda umekwenda twende nyumbani sio mbali na hapa ukaweke mambo sawa uwe safi kesho utaendelea na safari ndugu zako waelezee situation wakitaka watumie picha kabisa halafu tukimbie na huu msala wa kuchafua siti.

Akakubali. Tulishuka sote akafika nyumbani akatoa nguo zote akazifua na kuzianika. Ilibidi nimnunulie kufuri mpya na pedi zingine za brand nzuri.

Nilimpa risala sana ule usiku. Kwamba kwann mtoto wa kike unasafiri kirahisi vile huoni namna umejihatarisha. Yaani unasafiri haubebi kitenge hata viwili na hata pedi tatu za dharula maana hata usipopata wewe anaweza pata mwanamke mwenzako ukamsitiri. Nikamwambia sasa usingekutana na mimi leo si ungefedheheka sana.

Kesho yake nikamsindikiza jioni aende kwa kwao huko Arusha. Na baada ya hapo tuliendelea kuwasiliana she is someone very close to me now.
Hapo unachukua point zote 3 zaidi hata yule aliemnunulia huyo mtoto Marcedes
 
Hii ni muhimu mno. Nilikuwa nakwenda Morogoro na basi la Abood la mwisho kabisa kutoka Dar.

Nilipata siti ya mwanzo kabisa nyuma ya dereva. Nilikuta kuna binti tayari keshakaa jirani ya siti yangu. Kama ilivyo uungwana nikamsalimia. Binti alinishusha na kunipandisha akachuna.

Nilikuwa nimechoka na mambo yangu, sikumtilia maanani nikauchuna na simu yangu. Tulipofika chalinze nilinunua maji na korosho, kama ilivyo uungwana nimkamkaribisha, demu, kimya. Hapo hapo na yeye alinunua maji akatoa noti ya 10,000. Jamaa akamwambia hana chenji na bus linataka kuondoka. Nikamwambia jamaa (ni wale wanaouza ndani ya bus) ampe nikamlipa. Kwa aibu akatoa asante ya chini chini. Sikumjibu.

Kufika Morogoro sasa, kumbe ilikuwa anaenda kukutana na mwanaume. Jamaa kila akipigiwa simu hapokei na mwisho akazima simu kabisa. Nililijua hili maana alianza kupiga simu toka tupo Mikese.

Nilipakia spare kwenye boot, hivyo tulipofika Moro ilibidi niwe mpole mpaka mizigo ya wengine iishe. Ndio bi dada ikabidi ajilete kipole kuuliza kama mimi ni mwenyeji Morogoro. Nikamwambia si mwenyeji nimekuja mara moja nageuza kesho yake.

Ikabidi sasa usister duu aweke pembeni aanze kufunguka ukweli. Kuwa alikuja kukutana na bwana 'ake na ndie aliemtumia nauli.
Ilikuwa ana Sh. 10,000 tu mfukoni na hajui pa kwenda maana mshkaji kaingia chaka.

Ikabidi nimwambie asubiri nichukue mizigo yangu halafu nitaona cha kumsaidia. Uzuri mwenye spare ilikuwa anazipokelea hapo hapo Msamvu. Nikaenda kuchukua chumba lodge na mgeni wangu nyuma. Baada ya hapo hatukutongozana tena. Alijuwa wajibu wake na maringo alitupa pembeni tena.

Msela wake alikuja kumtafuta asubuhi tukiwa tunajiandaa kuondoka akiomba samahani kuwa simu ili stuck touch akashindwa kupokea. Itoshe kusema kuwa jamaa alitukanwa kila tusi la duniani, mimi na cha maringo wangu tukarudi dar na kuendeleza libeneke kwa miezi kadhaa mbele mpaka nilipoamua kumpotezea kutokana na demu kuwa na shida za kila siku kuliko hata mkimbizi wa Sudan.
[emoji23][emoji23][emoji23] dah hatari sana
 
Umenikumbusha one time kuna huyu binti kwenye basi la mkoa alileta huu uswahili. Amepanda kwenye basi amevaa jeans, sweater, na kablouse. Basi hana hata pochi yaani yupo kisela sana.

Kilichotokea ni period ilimuanza ghafla bila kujua. Kilichofanya nijue ni alivua sweater lake na kulitumia kama kujifunika sasa mimi nilikuwa na sweater na zile shuka za kimasai. Nikamuuliza mbona umevua sweeter na gari wamewasha AC haikutesi?!

Akajibu kama vile mtu mwenye mawazo na aibu fulani. Ilinichukua dakika chache kunotice kuwa hakuwa sawa na nikashajua huyu ametumia sweater kujificha. Nikamwambia kwa sauti ya chini sana unahitaji msaada. Hakunijibu zaidi ya kuinama kama anaona aibu halafu anaweka lile tabasamu la aibu fulani.

Nikamwambia niandikie kwenye sms unataka msaada gani. Nikampa simu yangu aandike namba yake nikamtext akaanza kuchat akanambia ameingia Period hapo hana uhakika na kinachoendelea ila anahisi amechafua siti sasa hajui pa kuanzia.


Aiseee ni MUNGU tu alisimamia ile situation maana gari lilikuwa na utingo mwanaume tu. So ikabidi nimfuate nimpange kuwa atusaidie wakiona hata kituo cha mafuta wasimame konda akanielewa. Tukasimama akasema abiria tuchimbe dawa kidogo. Watu wakaanza shuka. Akachukua sweta akaliweka pale kwenye siti halafu nikampa shuka langu la kimasai akajifunika mwili mzima so muda tunatoka nashuka nae hakuna mtu alishtukia chochote hadi tunafika chini. Nikamwambia atangulie chini me nakwenda tafuta pedi. Nikaenda mnunulia duka liko huko barabarani kipande kidogo toka pale kwenye sheri nikamletea.

Akajiweka sawa suruali yake ilikuwa imechafuka akaisuuza na maji akavaa hivyo hivyo nikamwambia valia na hilo shuka la kimasai. Tukarejea kwenye gari. Aisee ikawa kama ni mke wangu sasa namna tulivyorudi na kukaa kwenye gari alijiegemesha kwenye kioo me namwambia niegemee kama unataka kulala.

Tulishuka sote stand ya Moshi alikuwa anataka kwenda nikamwambia sidhani kama utakuwa katika hali nzuri kuendelea na safari katika hali hiyo na muda umekwenda twende nyumbani sio mbali na hapa ukaweke mambo sawa uwe safi kesho utaendelea na safari ndugu zako waelezee situation wakitaka watumie picha kabisa halafu tukimbie na huu msala wa kuchafua siti.

Akakubali. Tulishuka sote akafika nyumbani akatoa nguo zote akazifua na kuzianika. Ilibidi nimnunulie kufuri mpya na pedi zingine za brand nzuri.

Nilimpa risala sana ule usiku. Kwamba kwann mtoto wa kike unasafiri kirahisi vile huoni namna umejihatarisha. Yaani unasafiri haubebi kitenge hata viwili na hata pedi tatu za dharula maana hata usipopata wewe anaweza pata mwanamke mwenzako ukamsitiri. Nikamwambia sasa usingekutana na mimi leo si ungefedheheka sana.

Kesho yake nikamsindikiza jioni aende kwa kwao huko Arusha. Na baada ya hapo tuliendelea kuwasiliana she is someone very close to me now.
Dah! Umenifurahisha kwa ukarimu wako! Hiyo hali inatesa sana.

Wewe ni mume bora kwa mkeo[emoji2935]
 
1. Salimia unayemkuta kwenye siti maana hujui ya baadae. Inakera hukusalimia halafu baadae unaanza kuuliza "Eti hapa tumefika wapi?" [emoji849][emoji849][emoji849]

2. Kuwa mstaarabu unapoingia kwenye basi hasa kama tayari unajua siti yako haina haja ya kugombania mlangoni.

3. Sikiliza nyimbo na video za kwenye simu yako kwa kutumia earphones kwani kinachokufurahisha wewe kwa mwingine yawezekana ni kero.

4. Usiongee na simu kwa sauti kubwa hasa mambo yako binafsi kwani hakuna anayehitaji kujua mambo yako.

5. Kuwa mwangalifu unaposinzia epuka kumlalia jirani yako unaposinzia. Sambamba na hilo soma gazeti lako kwa uangalifu sio unalitandaza hadi linagusa pua ya mwenzako.

6. Usilazimishe kuchungulia dirishani kila mara wakati umekaa siti ya katikati, hiyo ni kero kwa aliyekaa dirishani.

7. Kama unasafiri na watoto wakatie siti yao isiwe kero kwa jirani yako. Unasafiri na watoto watatu kwenye siti moja ni kero kwa jirani yako na kwa watoto.

8. Usipake pafyumu kali za kukereketa wenzio. Sambamba na hilo piga mswaki vizuri ni kero kukaa na abiria anayenuka mdomo hasa anapokusemesha.

9. Msome abiria uliyekaa naye kama hapendi kusemeshwa usimsemeshe semeshe, mwache, wengine wana mambo yao kichwani, wengine wanaenda kwenye misiba, wengine wamefukuzwa na waume zao huko walikotoka, sio kila mtu anapenda kuongea safarini.

10. Kama unajijua una tatizo la kutapika safarini jiandae mapema kwa kuwa na vifaa vya kukusaidia kwenye hali hiyo.

Ongezea la kwako hapo kama unalo.
#5 noma sana[emoji23]
 
Yani ndio Bus linatoka mule Mbezi Louis kuitafuta Morogoro road, mama na mtoto waliokaa pembeni yangu wote kwa pamoja wakaanza kutapika. Dakika sifuri tu nimepakwa matapishi dadek.

Sijawahi kusafiri kwa raha mimi.

Enzi za Mohammed trans, natoka kanda ya ziwa kuitafuta Dar. Kuna wabibi ndani ya bus wanasafiri na wajukuu wao wadogo sana kiumri. Mmoja kati yao akaachia uharo kwenye corridor zile za katikati ya siti. Bus zima tulitafutana kwa hiyo harufu yake!

Mara nyingine tena natoka Dar kwenda Kanda ya Ziwa, ndani kuna familia ya hawa ndugu zetu wasukuma. Yani mmoja amekaa siti ya nyuma kabisa, anapiga story na mwenzie aliekaa siti ya katikati ya Bus. Walipanda na ndoo ndogo ya maji ya kunywa, wanachota kwa kikombe then wanapasiana kutoka nyuma mpaka katikati. Siku hiyo kabila lote la wasukuma lilinikwaza!

Mara ya mwisho nimepanda Bus, siti ya pembeni akakaa mzee mmoja hivi. Asee mzee alikua ananuka tumbaku sijawahi ona. Kila watu wakishuka kula na kuchimba dawa, yeye anashuka kuvuta tumbaku zake. Nilifika kwa tabu sana wakuu!
 
Unakutana na mtu ana constipated au ana halitosis kubabake. Unaweza omba kubadilishiwa siti. Halafu watu wanaonuka midomo wanapenda sana kuleta story sijui kwann. Nikama wanakuwa wameshahisi kuwa midomo yao inatema ila wao wapo busy kulazimisha kuwa haitemi.
🤣🤣🤣🤣🤣🤣
 
Kuna wengine wanapenda kuongea jmn tena usiombee awe anasoma gazeti ndio atataka kila habari adiscuss na wew, iwe siasa, iwe michezo ili mradi ni kuongea mwanzo mwisho...[emoji847]
Mwambie masikio yangu hayapendi disturbances ambazo haziambatani na cash. Yee nwenyewe atakaa kimya
 
Mara nyingine tena natoka Dar kwenda Kanda ya Ziwa, ndani kuna familia ya hawa ndugu zetu wasukuma. Yani mmoja amekaa siti ya nyuma kabisa, anapiga story na mwenzie aliekaa siti ya katikati ya Bus. Walipanda na ndoo ndogo ya maji ya kunywa, wanachota kwa kikombe then wanapasiana kutoka nyuma mpaka katikati. Siku hiyo kabila lote la wasukuma lilinikwaza
Wasukuma noma sana aisee
 
1. Salimia unayemkuta kwenye siti maana hujui ya baadae. Inakera hukusalimia halafu baadae unaanza kuuliza "Eti hapa tumefika wapi?" [emoji849][emoji849][emoji849]

2. Kuwa mstaarabu unapoingia kwenye basi hasa kama tayari unajua siti yako haina haja ya kugombania mlangoni.

3. Sikiliza nyimbo na video za kwenye simu yako kwa kutumia earphones kwani kinachokufurahisha wewe kwa mwingine yawezekana ni kero.

4. Usiongee na simu kwa sauti kubwa hasa mambo yako binafsi kwani hakuna anayehitaji kujua mambo yako.

5. Kuwa mwangalifu unaposinzia epuka kumlalia jirani yako unaposinzia. Sambamba na hilo soma gazeti lako kwa uangalifu sio unalitandaza hadi linagusa pua ya mwenzako.

6. Usilazimishe kuchungulia dirishani kila mara wakati umekaa siti ya katikati, hiyo ni kero kwa aliyekaa dirishani.

7. Kama unasafiri na watoto wakatie siti yao isiwe kero kwa jirani yako. Unasafiri na watoto watatu kwenye siti moja ni kero kwa jirani yako na kwa watoto.

8. Usipake pafyumu kali za kukereketa wenzio. Sambamba na hilo piga mswaki vizuri ni kero kukaa na abiria anayenuka mdomo hasa anapokusemesha.

9. Msome abiria uliyekaa naye kama hapendi kusemeshwa usimsemeshe semeshe, mwache, wengine wana mambo yao kichwani, wengine wanaenda kwenye misiba, wengine wamefukuzwa na waume zao huko walikotoka, sio kila mtu anapenda kuongea safarini.

10. Kama unajijua una tatizo la kutapika safarini jiandae mapema kwa kuwa na vifaa vya kukusaidia kwenye hali hiyo.

Ongezea la kwako hapo kama unalo.
11. Usile hovyo hovyo njiani hasa vyakula vyenye harufu kali kama mayai na chips.

12. Ukipishana kauli na abiria mwenzako usitumie lugha za matusi, heshimu watu usiowajua.

13. Ukikaa na binti mzuri jitahidi basi kumliwaza kwa stori nzuri na mwisho wa safari omba namba.
 
Back
Top Bottom