Safi sana wewe ndiye unaewaza vyemaHili jambo limekaa kiimani zaidi,lakini watu si wanapona jamani,anyway wizara ya afya imeshaunda task force yenye technical personells,watachunguza kwa undani huduma ya babu kama ina viwango vinavyokidhi na itatuambia kama hii dawa ni curative kwa hiyo tusubiri saizi tutabishana kwa mitazamo ya kiimani zetu na ukweli hautapatikana.
tukumbuke huyu sio mtu wa kwanza tanzania kutamka kitu kama hicho.. kuna yule dada wa Kanyigo miaka ya 1990s katikati, James Brwn, Mzee wa Tegeta na NDUKAI.. where are they.....
Ingia ndani ya maandiko ya Mungu na uelewe nini maana ya karama! ukielewa maana ya karama hata hutasema karama hiyo! Kazi ya Mungu na zawadi zote za kiroho anazotupa Mungu zi wazi kwa watu wote na kwamba zinaweza kufanywa na mtu yeyote kama zimekubalika kwa Bwana! ndio maana mamlaka wapewa wote na formula iko wazi! Mungu ni mjinga hata aruhusu watu wafe wakiubiri mtu mmoja?? kama Mungu ametoa tiba kwanini asiongeze na wahudumu?? haoni??
wee acha kjidai unamfahamu Mungu acha ujuha bana! kwani kina Nuhu, Loti, si peke yao waliteuliwa? wee umeathirika na umangaribi naona!
Brikini nyuziiiiiiiiiiiiiiiiiiii za miaka ya Maisha bora kiboko,
Habari Za wandugu wa JF,
Nimeamini kuwa kilichosemwa na BIBLIA hakitabadilika hata kama ni kwanini.
1.WATU HAWA WANAMACHO LAKINI HAWAONI, WANAMASIKIO LAKINI HAWASIKII.
2. WENGI WATAKUJA KWA JINA LA MUNGU.
Tusibabaishwe na mganga wa Loliondo ukweli hakuna Mungu wa namna hiyo yeye angetumia tu jina la Mganga wa kienyeji sio Mungu unajua ni kwanini?
a. Dawa ya Mungu hainaga masharti, hata ukipewa sio masharti kama ya Loliondo eti hakuna mtu mwingine kukupa dawa hiyo ukanywa zaidi ya yeye peke yake swali: Watumishi wa Mungu Loliondo ni yeye peke yake? kama wengine wapo kwanini wasisaidiane? si kumpa tu mtu maji anakunywa??
b. Kwanini mti huo kama umefunuliwa na Mungu ukitumiwa na wengine usiponye?? Maana yake Mungu ameanza lini kutufundisha ubinafsi na uchoyo?
Nikomee hapa nitarudi! View attachment 24640
Kama watu wanapona it is ok.saa hii nauli ya laki na zaidi inatoka wapi jamani?kama watu wanapona it is gud
Unakumbuka yale aliyofanya Yesu je kila mtu aliweza kuyafanya. Pia soma kuhusu fimbo ya MUSA. Je kila mtu aliruhusiwa kuitumia na ikafanya kazi. Imani haitakiwi kuhojiwa kama ilivyo kwa sheria ni kuijua na kuifuata, ukipingana nayo utahukumiwa.
nakuomba uzikashifu na ARv's na za pressure , kisukari dawa zoote za kimangaribi, seems wewe ni limbukeni, issue hapo ni kupona! unajua ARV's zinawafanyia nini watu? bora miti shamba isiyotiwa midawa kabisa? tena ipo maporini hata moshi wa magari haikuwahi pata! so tulia kama unaumwa nda huko, na hiyo issue ya breaking news futa kabisa upupu wako!
Habari Za wandugu wa JF,
Nimeamini kuwa kilichosemwa na BIBLIA hakitabadilika hata kama ni kwanini.
1.WATU HAWA WANAMACHO LAKINI HAWAONI, WANAMASIKIO LAKINI HAWASIKII.
2. WENGI WATAKUJA KWA JINA LA MUNGU.
Tusibabaishwe na mganga wa Loliondo ukweli hakuna Mungu wa namna hiyo yeye angetumia tu jina la Mganga wa kienyeji sio Mungu unajua ni kwanini?
a. Dawa ya Mungu hainaga masharti, hata ukipewa sio masharti kama ya Loliondo eti hakuna mtu mwingine kukupa dawa hiyo ukanywa zaidi ya yeye peke yake swali: Watumishi wa Mungu Loliondo ni yeye peke yake? kama wengine wapo kwanini wasisaidiane? si kumpa tu mtu maji anakunywa??
b. Kwanini mti huo kama umefunuliwa na Mungu ukitumiwa na wengine usiponye?? Maana yake Mungu ameanza lini kutufundisha ubinafsi na uchoyo?
Nikomee hapa nitarudi! View attachment 24640
hapo kwenye bold tu nimechoka!!
muhimu kupona iwe imetoka kwa mungu ama la unachojua ni uizima kwanza. Imani bora kabisa hii!!
IS this a breaking news?
KWAMBA NI KUTOKA KWA MUNGU AU KWA SHETANI SIJUI, NINACHOJUA MIMI NI KWAMBA NILIKUWA MGONJWA NA SASA NIMEPONA
pole sana ndg yangu, je ukipona sasa hutakufa??????????????? "there is no free meal" aliye nyuma ya huo uponyaji lazima atavuna anachopanda , watu wakiona mambo yalivyo ovyo duniani kwa sasa wanakiri dunia imekwisha lakini ukiwaeleza ishara za mwisho wa dunia kama lisemavyo neno la Mungu" siku za mwisho kutakuwa maajabu na ishara nyingi za uongo kutoka kwa roho ya mpinga kristo" somo hilo linakuwa gumu sana. Sikiliza mwisho wa huyo babu.
Hebu ngoja tuone, hivi kumbe Mfalme Naamani yeye hakupewa masharti? Sijui bana haya mambo mie, kikubwa matendo yangu tu, the rest are details
mimi ninachotaka angetibu tu kwa jina la mafumba ng'wana ngikili siyo kutumia jina la mungu.wewe bado mchanga kiroho na upeo wako wa bible ni mdogo sana inawezekana una husuda binafsi au una sali kwa kakobe.
Nikuulize maswali yafuatayo ukinijibu basi argument zako ni sahii:
1. Walikuwepo yesu wangapi? Na kwa nini hawakuletwa wengi ? likuwepo yesu mmoja ndiyo maana aliongeza na wanafunzi 12 wa kumsaidia! Hata pale alipotenda miujiza ya kulisha watu 5000 waliogawa chakula walikuwa wanafunzi wake! Why not loliondo to have another asisitance people?? aliletwa mmoja kwa ajili ya ukombozi na ununuzi wa dhambi kwasababu alitosha kuleta uzima katika ulimwengu wote na ndicho kilichofanyika wokovu u tele hata sasa hata ulipo sio wakusubiri kama wanavyosubiri loliondo.
2. Ni kwa nini only kwa jina la yesu unafika mbinguni au unapona au kuokoka na siyo kwa jina linginelo kama la petro, paul, yohana au watume wengine? kwasababu yesu ndiye ukombozi swali hili ni sawa na la kwanza! Lakini jina hilo la yesu linaletwa na watumishi wake akina wewe na wengine ndipo mtu anapookoka na kulielewa! Ingekuwa yesu aseme kuokoka ni mpaka ahubiri yeye tu tungepata wokovu ?? Ingetokea yesu angesema wagonjwa watapona kwa kuombewa na yesu peke yake msululu ungekuwaje??
kama unasema dawa ya mungu haina masharti kasome habari za naaman alipoambiwa akajizamishe mto yordani mara saba ndo apone ukoma au soma habari za kipofu aliyepakwa matope akapona. angalia masharti vizuri (masharti yote ya mungu hayafungi na hayaleti madhara, mtu huyo asingeenda kuchovya kwenye bahari hiyo asingepona na asingekufa ila angebaki alivyo! Sasa loliondo masharti hayo tayari yameanza kupeleka wengine peponi kwa kusubiri matibabu wasiyapate kwa urahisi! Na bado patakuwa makaburini!
mungu hana fomula anapotaka kumponya mtu kwani anaweza tumia mbinu yoyote kama aliyotumia jangwani kumwambia musa amtundike nyoka wa shaba juu ya mti na atakayemwangalia ndiye atakaye pona. Sasa jiulize je ni wote waliweza kumwangalia wakati walikuwa mahututi? tofautisha adhabu na matibabu! Wanaoenda kutibiwa siyo wanamakosa tofauti na wale waliowekewa nyoka kwa sababu maalum hebu kua kiroho basi.jibu ni hapana kwani kuna wana wa israel walikuwa na hali mbaya na hawakuweza kumwangalia nyoka na wali kufa. usijipe jibu la hapana jiulize swali kwanini mungu alitoa matibabu ya kumwangalia nyoka au njia ya kumangalia nyoka?? Tofautisha na adhabu bana na maswali yako yanajirudiarudia sana.
unaweza kujiuliza kwa nini nyoka wa shaba wakati kuna dawa? naomba usome chanzo cha kuwekewa nyoka wa shaba! Na uelewe siyo nyoka wa shaba tu kulikuwa na nyoka wengine wakiwauma na the same time wanaambiwa wamwangilie huyo nyoka kwa uponyaji wao! Huu mfano ulionukuuu hata hauwezi kufaa hapa! Go read it again.. Hili swali litajibiwa kwa swali la kwa nini tu huyu babu wa loliondo, na kwa nini huo mti tu? hayo mimi siyakatai, kinachoshangaza huduma yake imeanza kuleta madhara tayari it means mungu ameita watu waje lakini hana vitendea kazi vya kuwatibu hadi wanasubiri huyo babu tu nakufa!
wewe kama unahitaji kupona kanywe dawa acha ubishi ambao kwa sasa hautakusaidia na hili ndilo tatizo la watanzania mtabaki ku doubt kila kitu wakati wenzenu kutoka kenya , uganda, rwanda na ulaya wanapona . Mungu ameangalia uadilifu hapa kwani wangepewa watu wengine hiyo dawa ingekuwa imefika milioni.
Mwache babu wa watu aendelee na kazi yake hata bibilia haijasema wakenya wala wanyarwanda wala wazungu imesema watatokei wengi kwa jina langu na watesema mungu yuko kule lakini msiamini.