Aleluyah!
Nimekuwa nikitafakari sana kuhusu huyu Babu wa Loliondo na nguvu alizo nazo za kuweza kuponya maradhi mbali mbali ambayo ni sugu hapa duniani. NIkianza kutafakari neno la Mungu ambalo linasema siku za Mwisho watakuja Manabii wa uongo soma Mathayo sura yote ya 24.
Nimeona watumishi wengi wa Mungu ambao wamekuwa wakitumia Neno la Mungu kufunika matendo yao magumu na ya kichawi tukiambiwa kuwa hawa ni watu wa Mungu. Lakini baada ya Muda imedihirika kuwa ni nguvu za kishirikiana zimekuwa zikitumika. Utakumbuka kuwa Paulo alimtoa pepo mama mmoja ambaye alikuwa ni mjakazi wa mtu ambaye kwa kutumia hilo pepo lake la utambuzi alikuwa akitumika kuagua watu na Mabosi wakewalifaidika sana kimapato kwa kumtumia yeye ingawa yeye alikuwa hafaidiki zaidi ya kuwa mjakazi, na pale paulo alipolikemea na kutoka ikawa ndo mwisho wa mambo ya utabibu wake.
NI kweli nina uhakika kuwa Huyu alikuwa ni Mchungaji kule Imiti babati na leo hii amepewa nguvu za kuweza kutibu magunjwa kwa kutumia dawa ya mizizi. Sasa swali langu ni kitu gani kinachozuia yeye kufanya kazi sehemu nyingine yoyote nje ya eneo lake, je ni kwaninini hiyo dawa lazima akupe yeye kwa mkono wake mwenyewe?
Hii inanipa nafasi ya Kumtafakari pia Mtumishi mwingine aliye kuwa Mchungaji na baada ya kwenda Huko NIgeria na kurudi alirudi na upako wa ajabu sana amabo akikunyooshea mkono tu unaanguka na aliponyesha watu wengi sana lakini siku za hivi karibuni amepoteza umaarufu wote baada ya kujulikana kuwa natumia nguvu za giza kutekeleza hayo yote.
Leo hii natafakari jinsi watu wanavyo kwenda kwa wingi kutoka mikoa yote ya Tanzania na nje ya Tanzania sehemu ambayo haina miundo mbinu na si ajabu leo ukasikia magonjwa ya mlipuko huko Loliondo. Jana nimepewa taarifa kuna Msafara wa magari km 50 wanasubiri huduma hiyo.
Mimi sitaki kumkani huyu babu kwamba yeye ni wa Mungu lakini Neno la Mungu linasema tuzipime hizo roho.
rai yangu watu wa Mungu nisaidieni niweze fahamu ninyi ambao mmesha zipima hizo roho je ni kweli huyu ni mtu wa mungu na siyo anasaidiwa na Mizimu ya mahalia na ndiyo sababu hawezi amishia huduma yake sehemu nyingine? Na hivyo mizimu hii imekuja kwa Sura ya Malaika wa Nuru.
Nisaidieni kwani mimi ni mchanga kwenye Imani nahitaji msaada. Wasi wasi wangu isije kuwa tunakwenda kwa Mganga wa Kienyeji tukuifikiri ni mtu wa Mungu, yaani nalataka ni watu wajue kuwa ile ni nguvu ya Mungu au la ingawa inaponya.
Nawasilisha
Mungu awabarikLi sana!
Sina maelezo ya kukusaidia zaidi ndugu yangu ingawa mie kama wewe nimeombea jambo hili ili kupata mafunuo zaidi usiku mmoja. Na Roho kwa namna ya ajabu usiku ule alinielekeza katika Zaburi 34 (please read na uamue). Unajua wanadamu tumeteseka sana na magonjwa ya kila aina na sasa baada ya Babu kutokea tunaona ndiyo pumziko limekuja kimsingi hakuna anayehoji sana kwani the driving force ni kupona na kuwa HURU. Ila neno linasema zijaribuni ROHO hiyo ndiyo caution yangu.