Mambo ya kwa Babu LOLIONDO

Jana liianzisha hii topic wakubwa wakaifunga naona leo nguvu ya umma inafanya kazi imeanzishwa tena.
 
Hivi bado watu wanaenda kwa kakobe
 
imani yako itakuponya ila kama una imani haba usiende kwa babu plez ni wastage of time.
 

Wewe unaelewa unajibu kuhusu nini? Watu wanaenda kupata matibabu kwa maradhi ambayo bado yanasumbua tiba yake. Wewe umeng'ang'ana na uvivu wa watu kufanya kazi. Au wewe ndio umekasirika kwa kuwa hiyo sio dawa ya kuleta utajiri? Elewa mada inayozungumziwa.
 

hii mada ina mantiki, haiwezekani watu wasafiri kutoka sehemu mbalimbali kukimbilia dawa ya mtu huyu, hii inaonesha dhahiri watu wamekata tamaa na huduma mbovu zitolewazo katika hospitali zetu
 
Gari mali ya Shirika la Umma ndani ya Loliondo, hatuna hakika hii gari ilikuwa na mahusiano gani na uwepo wake kule. Shirika linalomiliki hili gari linatakiwa kutoa maelezo. Pesa za walala hoi zinatumika kulihudumia hili gari lakini hiyo pesa haikupaswa kutumika kama inavyoonekana pichani. We need maelezo.

 
well,kwani hata msanii wa ukweli si alienda huko?kwani hujui?alijidai ameenda kukagua nyayo za watu wa kale!sasa cha kushangaza mbona hakwenda siku zote hizo?mama wa msanii wa ukweli akajiona mjanja kuvaa ijabu ila wajanja wakamwona!watu kibaooooo huko
 
people are so desperate towards their own created problems, and because of desperation no one who is taking any critical analysis of the event. why cant we take time and analyse the event in logical way that other can get the concept and understand rather than pouring brabra all the way
 
kunywa dawa arifu ka iman ipo kwel hapo nimewakubal
 
kama rais wa nec mwenyewe anasema mfumuko wa bei za vyakula utategemea na kudra za mwenyezi mungu kuleta mvua sasa ni kwanini mtawaliwa asitegemee kudra za babu kupona
 

utata wa watanzania wengi unakuja kwa kujidai ujuaji wa kila kitu!hawaheshimu profession.mgonjwa anaweza kukataa dawa kisa vipimo ni -ve bila kujua kwamba vipimo ni kipengele tu katika matibabu ya mgonjwa.nawashauri muwe mnauliza kwa nini mhudumu wa afya anakufanyia kitu flani na sio kujiamulia kivyakovyako.
'Ujuaji' huu unasababisha watu kuingizwa mkenge kama ule wa loliondo.
 
Naye (yule aliyekuwa Kipofu) akajibu: "Kama ni mwenye dhambi mimi sijui. Lakini kitu kimoja najua: Nilikuwa kipofu na sasa naona." I like it that way, but don't forget we're dealing with 'The Sword of Jesus' or in swahili: 'Panga la Yesu', sasa Yesu na Panga wapi na wapi? Au ni 'Mujaheedina wa Yesu'?
 
Amini usiamini sio kwamba wote wanaokwenda huko wako desparate coz ya huduma mbaya za hospitali zetu.

Sio vizuri kutaja majina lakini wamekwenda viongozi wakubwa wa nchi hii ambao hutibiwa nje kwa kodi zetu. Jamaa wamechagua
kwenda Loliondo baada ya USA, UK, India, Canada etc believe it. Inasemekana huyo mchungaji dawa yake inatibu hata magonjwa
sugu yasiyotibika kwa modern medicine kama UKIMWI, KISUKARI, Hupertension, Cancer etc. Wiazara ya afya sasa hivi imetuma
watalaamu wa National Institute for Medical Reserach (NIMR) kwenda kuifanyia utafiti dawa hiyo kwa kuanzia kwa ku-prove kama
kweli inaponyesha magonjwa hao.

It is really a serious thing kwa hapa Tanzania. Kuna wahindi kutoka India wapatao 200 wameombe VISA ya kuingia TZ kwaajili
ya kwenda Loliondo kupata hiyo miracle medicine, It is a medical panacea kama kweli inafanya kazi kama wanavyosema
wenyewe waliowahi kutibiwa na dawa hiyo.

Sasa hivi ukifika Loliondo kabla ya kumuona Mchungaji na kunywa hiyo dawa unaweza kuchukua kati ya weeks 3-4 kabla hajupata dawa.
Tatizo la dawa hiyo ni lazima uinywee hapo hapo ukiipeleka nje na hapo haiponeshi tena. Kuna wagonjwa kibao sasa wanatolewa mahospitalini
na kupelekwa Loliondo. Wengine wanakufa kabla ya kumuona na kunywa hiyo dawa kutokana na idadi kubwa ya wagonjwa walioko kwenye
foleni ya kusubiri.

Bei yake TSH 500/= TU
 
Mimi sidhani kama kuna tatizo kama watu wanapona, na inaonekana kabisa kweli kuna nguvu ya Mungu..
 
mhu jamani michuzi kaweka eti karibia watu saba wameshakufa sababu wamepelekwa wakiwa mahututi,pia msongamano ni mkubwa kupita kiasi,mi naona serekali ingeingilia kati kusaidia watu na huyo mzee,sasa wiki mbili hujamuona babu na watu wanazidi kwenda si balaa hilo,Mungu ambariki huyo babu azidi kusaidia watu,mi naona watu kama wamechelewa kweli iyo dawa sio kwamba kwasasa itabidi idairudiwe ili iweze kutosha?aya we... ya Dunia mengi mara mabomu, mara babu roliondo,story haziishi.......
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…