Hizi zote ni ishara za watu waliokata tamaa na maisha! We fail to invest in better infrastructures, health services, education, roads...etc for our children..na tunaanza kukimbilia Loliondo kutafuta dawa za kututibu ukimwi na kansa! Ama kweli! Umasikini ni kitu kibaya. Lakini ni kibaya zaidi kama ni umasikini wa fikra. I only wish tungekwenda Loliondo kukomboa mbuga yetu aliyogawiwa yule mwaraabu...perhaps angetupa kodi zaidi tukajenga ile barabara ya Arusha-Loliondo!
Kama mnabisha kwamba watanzania tumekata tamaa na maisha angalia vitu kama DECI vilipoingia hata wakubwa wa serikalini waliiba kodi zetu wakaenda 'kupanda mbegu' sijui leo DECI iko wapi...mifano ni mingi jamani
Ushauri wangu kwa watanzania wenzangu: Mafanikio hayana short cut. Huwezi kupata utajiri simply kwa kwenda kwa mganga! work hard and bit of 'luck' money will come. Ni kupenda hivi vitu vya mkato mkato ndo tunazidi kuwa masikini. Unalala..usiku asubuhi unataka uendeshe Lexus! Unless uibe utaipata wapi? Mwanafunzi anashindwa kusoma shule anataka mganga amsaidie kufaulu mtihani! Tunawanyima haki wanachi wetu na kupeleka hela zote uswisi huku wachache wakiishi maisha ya peponi...harafu unakuta hao hao wanasimama kwenye majukwaa wakitwambia twende kanisani kuombea amani ya nchi! Kuna watu wanatufanya tuone kwamba umasikini ni mapenzi ya Mungu kitu ambacho si kweli. Kikwete anaona kabisa DOWANS wanatuibia na wale wahusika kashindwa kuwawajibisha...they have swindled billions in our name....Kikwete huyo huyo anasimama mbele ya TV anatwambia kwamba matatizo ya umeme yanatokana na kazi ya 'Mungu' kwa sababu mvua haipatikani. Twende kanisani/msikitini tukaombe mvua inyeshe tupate umeme!
I Masanja, I refuse to believe in this! Hardwork, determination and discipline will liberate you! I say and I do! Amen!