Mambo yaliyokuwa yanakuudhi nyumbani ulipokuwa mdogo...

Mambo yaliyokuwa yanakuudhi nyumbani ulipokuwa mdogo...

Wimbo wa Sabuni ya Mshindi halafu nasikia kawimbo ka Matukio Radio Free Africa, hapo najua muda wa shule. Bas Mama anaanza kutuamsha mimi na braza, asubuh baridiiii
 
Mimi nilikuwa nakereka kwa mambo haya:

1: Kurudi home mchana nakuta madha anachambua mboga halafua ananiambia nikawashe jiko na inabidi nirudie shule,

2: Anapita home msichana tunayesoma naye darasa moja hata sijamwongelesha, madha anaongea kwa sauti ya juu 'We hivi leo si ndio zamu yako kuosha vyombo’

Duuuh, nilikuwa nakasirika vibaya! Wewe je?
Hahahahaaaa.. Ukweli mtupu mzee baba
 
Wageni nilikuwa siwapendi hata kidogo !!kilicho kuwa kinaniuma siku akija mgeni wenyew hatuna dhamani -kuku - wali anakula mgeni sisi wenyewe maharagwe duuuh!niliumia sana
Hii tabia hata mii siipendi wageni wanaonekana wa maana kwelu hata vyombo vitatokewa vipya watumie wageni

Sent using Jamii Forums mobile app
 
mimi kulala mchana...nilikua sipendi na ilikua hamna kwenda kucheza hadi ulale mchana...basi nkifika room najilizaaaa hadi macho yawe mekundu af nachukua kitana nafunga kune paji la uso hadi alama itokee eti ndo mistari mistari ile ukitoka kuamka[emoji1]...af nakaa kidogo nasepa zangu kucheza...
Nilikuwa naliaa sanaa,eti lala ukue halaf nue unasikia wenzio wanacheza

Sent using Jamii Forums mobile app
 
We cheka tu enzi zile kazibyangu ilikuwa kutandikia kuku na mzoa mavi ya kuku arafu unamsikia mama anasema hawa kuku tuwatunze ili mgeni akija tusiumbuke.Aisee nilikuwa natukanaga kimoyo moyo kusikia vile.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hahahahahaha kwa hiyo nyie mlikula lini kuku sasa ,sikukuu tu au?hujawah mkumbusha mama hayo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom