Mambo yanayokuweka katika hatari ya kuugua ugonjwa wa Ini

Mambo yanayokuweka katika hatari ya kuugua ugonjwa wa Ini

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Liver_Cirrhosis.png
Virusi vya homa ya ini vipo vya aina 5 (A, B, C, D,E). Aina mbili za virusi (B Na C) zimetajwa kuwa ndio sababu kuu za ugonjwa wa homa ya ini ambayo husambaa kupitia damu na majimaji ya mwili.

Wataalamu wa afya wanasema virusi hivi vina uwezo wa kusambaa na kuambukiza mtu mara 100 zaidi ya Virusi vya UKIMWI.

Njia za maambukizi ya ugonjwa wa Ini
Kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto

Mama aliye na maambukizi anaweza kumuambukiza mtoto wakati wa kujifungua, iwapo hakuna juhudi za tiba za kuzuia maambukizi, kuna uwezekano hadi asilimia 90 kwa mama kumuambukiza mtoto.

Kufanya mapenzi na mtu mwenye maambukizi ya virusi vya homa ya ini

Kuchangia vifaa vyenye ncha kali kama sindano hasa kwa watumiaji wa madawa ya kulevya au wachora 'tattoo', miswaki etc

Kuongezewa damu ambayo ina maambukizi ya homa ya ini

Nani yuko katika hatari ya kuambukizwa

Watoto wachanga waliozaliwa na mama aliye na maambukizi ya virusi vya homa ya ini

Watu wanaofanya biashara ya ngono

Wanaume wanaofanya mapenzi na wanaume wenzao

Watu wanaojidunga dawa za kulevya

Mtu mwenye mpenzi ambaye anaishi na maambukizi ya

virusi vya homa ya ini

Wafanyakazi wa Sekta ya afya

Watu wa familia wenye ndugu anayeishi na maambukizi ya kudumu ya Virusi vya homa ya ini
Wagonjwa wa figo wanaotumia huduma za kusafisha damu (Dialysis)


Jinsi ya kujilinda
Dhibiti matumizi yako ya dawa

Tumia dawa ulizoandikiwa na mtaalamu wa afya, au daktari wa eneo lako. Usitumie dawa ulizoandikiwa pamoja na pombe au dawa za kulevya. Dawa zingine zikitumiwa kwa kipimo cha juu zinaweza kuwa sumu kwenye ini lako (kama vile paracetamol).

Punguza au acha kunywa pombe
Kadri unavyopunguza unywaji wa pombe, ndivyo unapunguza hatari ya kupata madhara yanayotokana na pombe ikiwemo magonjwa ya ini.

Acha kuvuta sigara, bangi au dawa zingine za kulevya
Sumu na kemikali zilizomo kwenye sigara zinaweza kudhuru ini lako. Matumizi ya kipimo cha juu cha bangi yanaweza kuongeza uharibifu wa ini. Kuna hatari ya kupata kansa ya ini ikiwa unatumia sigara au bangi.

Tumia mbinu salama ya kujidunga
Tumia kifaa safi na chako mwenyewe cha kujidunga, kuwa makini na kujichora chale au kujidunga mwilini. Chagua, kituo ambacho kinafuata njia salama za uzuiaji wa maambukizi, kamwe usishiriki kifaa cha kujidunga na mtu mwingine.

Shiriki ngono salama
Tumia kondomu wakati wa kushiriki ngono. Hatua hii itakulinda dhidi ya kupata maambukizi ya virusi kupitia majimaji ya ngono au damu.


----------------------------------------------


CHANZO CHA MAGONJWA YA INI

Magonjwa ya Ini yanavyanzo mbalimbali ambavyo asilimia kubwa yanatokana na mitindo ya maisha.

NAFLD_diagram-1764x700
  1. Matumizi ya vyakula au bidhaa zenye kemikali (Sumu).
  2. Matumizi makubwa ya vilezi na sigara
  3. Matumizi ya dawa zenye kemikali
  4. Virusi aina ya hepatitis A, hepatitis B, na hepatitis C
  5. Unene na uzito uliopitiliza (Obesity)
  6. Kwa Kurithi kama hemochromatosis na Wilson disease
  7. Kuto kula au kunywa vitoa sumu mwilini kama maji na vingine
  8. Tatoo au kutoboa mwili
  9. Kemikali nyingi zenye sumu (viuatilifu vingine, chemotherapeutics, mafuta ya peroxidised, aflatoxin, kaboni tetrachloride, acetaminophen, hidrokaboni zenye klorini, n.k.), chakula, pombe, maambukizo kama vile vimelea, virusi, fungi au bakteria na shida za mwili zinaweza kusababisha magonjwa ya ini kama vile hepatitis, ugonjwa wa ini wa uchochezi, homa ya manjano, hepatosis (ugonjwa wa ini ambao sio wa uchochezi, ugonjwa wa cirrhosis (ugonjwa wa mmeng’enyo ambao ni matokeo ya fibrosis ya ini), saratani ya ini, n.k.
 
WOTE TUTAKUFA TU, SASA UNATAKA UZIKWE NA INI JIPYA UKAMRINGISHIE NANI NA TULIAHIDIWA MIILI MIPYA TUKIFUFULIWA?
Halafu na hii kitu POMBE imewakosea nini hawa walinda afya wa mitandaoni?
Kila ugonjwa utasikia acha pombe, ezi ifu ukiacha pombe hautakufa. Wengine pombe ni tiba kwa tunayoyapitia.
Hawachelewi kusema pombe inamaliza hela, mbona na kwa Mwamposa bila hela hakuna kuteleza kwenye mafuta? Huko hela haziishi?
Siku ikifika ya kufa hakuna pa kukwepea, HAKIKA TUTAKUFA TU.
KUCHOSHANA TU...

#pombesiachinanitakufasaayanguikifika
 
Halafu na hii kitu POMBE imewakosea nini hawa walinda afya wa mitandaoni?
Kila ugonjwa utasikia acha pombe, ezi ifu ukiacha pombe hautakufa. Wengine pombe ni tiba kwa tunayoyapitia.
Hawachelewi kusema pombe inamaliza hela, mbona na kwa Mwamposa bila hela hakuna kuteleza kwenye mafuta? Huko hela haziishi?
Siku ikifika ya kufa hakuna pa kukwepea, HAKIKA TUTAKUFA TU.
KUCHOSHANA TU...

#pombesiachinanitakufasaayanguikifika
[emoji23][emoji23][emoji23]
Lakini pia pesa ya kodi ya pombe ndiyo inanunua dawa za magonjwa mbalimbali ikiwa ni pa1 dawa za kutibu ini na figo.

Na wakipandisha bei ya pombe simpigii kura chief Hangaya
 
[emoji23][emoji23][emoji23]
Lakini pia pesa ya kodi ya pombe ndiyo inanunua dawa za magonjwa mbalimbali ikiwa ni pa1 dawa za kutibu ini na figo.

Na wakipandisha bei ya pombe simpigii kura chief Hangaya
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Vitisho vingi sana kwenye pombe na bado kodi kwa kiasi kikubwa inatoka huko huko.
Watuache...
 
zinaa nayo ina uhatari mwingi ?🤔

jamani tupunguze kunyanduana ovyo maana starehe ya dakika 1 inakuharibia future dakika 0
 
Jamani tuongelee swala la hepatit b (homa ya ini) kuna aliyewahi kupona kabisa na alipima mara ngapi had kuja kupona?
 
Back
Top Bottom