Mambo yanayonikasirisha Kanisani

Mambo yanayonikasirisha Kanisani

Hasa hapo kwenye kwaya, Wanaimba nyimbo zilizotungwa kisasa, ukutane mpiga kinanda anatacheza kinanda makelele yaani unapoteza utulivu kabisa.

Baraza la walei wapige marufuku kwaya zinazoimba nyimbo zisizokuwepo kwenye liturujia.maana wanakwaya wengine wanafikiri pale ni jukwaa la kuonyesha mbwe mbwe zao.

Waimbe nyinmbo za rohoni ambazo kila muumini anaweza kuimba zile zina uburudisha moyo na utukufu unakujieni.

Sent using Jamii Forums mobile app
I second
 
Ni kweli Bro. Sijui hilo linawashinda vp. Kamani mbwembwe si wangoje siku za harusi? Aidha Paroko/Padri, Baraza (Kamati tendaji)/kamati ya Liturjia ni kama wanaunga mkono jambo hilo kwa ukimya wao. Kwaya (Wengi ni vijana) hawajakulia malezi ya Sala -hata ile kauli isemayo Kuimba ni kusali mara mbili hawakumbushwi au hawaikumbuki au wanaipuuzia.
Wabinafsi sana
 
Bora wewe, mimi kinachoniuzi ni kutopata nafasi/kutoruhusiwa kumuuliza maswali/ kumkosoa padri juu ya anacho hubiri.
Jiunge na wakatekutumeni au omba kuonana na padri baada ya misa umuulize maswali.
Hakuna kanisa lolote la Kikristo/Uislamu wakati wa mahubiri maswali yanaulizwa.
Maswali uulizwa wakati wa mihadhara
 
Wasalaam wana JF,

Kesho jamii nzima ya kikristo au sisi wakatoliki tunaanza kwaresma siku 40 za kufunga na kufanya ibada nyingi.

Pamoja na zoezi hilo, naomba niorodheshe mambo yanayonikera kanisani kama yafuatayo:

1. Kwaya kuimba nyimbo ambazo waumini hawazijui. Yaani wanaimba wenyewe tu mavitu ambayo hatuelewi na hatushiriki;

2. Wingi wa matangazo, makanisa yanakua kama platforms za matangazo, yanapoteza muda na kurefusha ibada;

3. Urefu wa mahubiri, mapadre wanaongea sana, waongee kwa kiasi ujumbe utafika tu;

4. Sadaka za kushtukiza, watu wapewe taarifa mapema watatoa tu; na

5. Kushindwa kufuata ratiba za ibada. Hii ni mikoani zaidi, unakaa zaidi ya nusu saa ibada haijatoka tofauti na ilivyoandikwa kwenye time table.

Nawatakia kwaresma njema.
Ni ajabu kuchoka ibada. Toka huko katoliki ambako kuna akili akili tu, hakuna Roho Mtakatifu humo. Amua kuokoka, umwabudu Mungu katika Roho na kweli, kamwe hautoboreka. "Waabuduo halisi watamwabudu Mungu katika roho na kweli, na Mungu anawatafuta watu kama hao" YOHANA 4:

JESUS IS SAVIOR
 
Ni ajabu kuchoka ibada. Toka huko katoliki ambako kuna akili akili tu, hakuna Roho Mtakatifu humo. Amua kuokoka, umwabudu Mungu katika Roho na kweli, kamwe hautoboreka. "Waabuduo halisi watamwabudu Mungu katika roho na kweli, na Mungu anawatafuta watu kama hao" YOHANA 4:

JESUS IS SAVIOR
Kuhama hama dini ni umalaya wa kiimani. Yesu wa katoioki ni huyo huyo wa kirutheri au pentecoste
 
Kuhama hama dini ni umalaya wa kiimani. Yesu wa katoioki ni huyo huyo wa kirutheri au pentecoste
Wewe hujihurumii kuichoka ibada. Ibadani ni sehemu tunakopata ushirika na Mungu wetu, sio sehemu ya kuchosha. Hata sisi tulikuwa huko uliko tukapata neema ya kuzaliwa mara ya pili. Acha kung"ang"ania dini, njoo kwa Yesu akuokoe!


JESUS IS LORD
 
Back
Top Bottom