Mambo yote Polisi huwa wanasingiziwa tu. IGP Wambura anapaswa kupongezwa kwa amani tunayoifurahia

Mambo yote Polisi huwa wanasingiziwa tu. IGP Wambura anapaswa kupongezwa kwa amani tunayoifurahia

Don Gorgon

Member
Joined
Nov 21, 2024
Posts
35
Reaction score
68
Jeshi letu la Polisi ni jeshi zuri sana na huenda likawa ni lenye weledi na utashi kuliko yote Afrika Mashariki na Kati. IGP Wambura ni IGP Bora zaidi kuwahi kutokea katika historia ya nchi hii. Ana historia nzuri ya kushughulikia wahalifu na askari wakengeufu kila wanapojitokeza na ametengeneza Jeshi imara ambalo halisigani na wananchi. Ndiyo maana kila raia yupo huru katika kila kona za nchi hii. Hofu iliyokuwepo enzi na enzi haipo tena.

Hakuna mtu atatekwa au kunyanyaswa kwenye nchi hii kama kuna uwepo wa polisi maeneo hayo. Ni watetezi wetu tunaopaswa kuwakumbatia vema. Tunaona kila siku watu wanavyosafiri kwa amani toka maeneo mbalimbali na wanapata msaada wa polisi kila wanapouhitaji. Kwanini wasipate msaada wakati ni wananchi halali na watiifu kwa nchi yao?

Kesi zote kama za akina Mzee Ally Kibao, Deo Bonge, Soka, n.k zimeshafanyiwa uchunguzi wa kina na majibu ya uchunguzi tumepewa. Watuhumiwa wamechukuliwa hatua na kila Mtanzania anajua hilo. Jeshi lina uwazi sana. Hawakai kimya. Hata wale waliompiga Lissu risasi polisi wamefanikiwa kuwabaini na kama tunavyojua Watanzania wote, wameshahukumiwa vifungo vya maisha.

Hata hili la Abdul Nondo nalo linashughulikiwa kwa umakini kabisa. Jeshi lipo vizuri, tutarajie weledi wao. Wambura juu, juu zaidi!

Wapo washirikina fulani wanasema eti polisi wanakamata watu wakiwa hawajavaa sare za kazi. Jamani, wapi na lini umeona wakifanya hivyo? Hao ni wahuni tu wanaolenga kulisigina jina la jeshi letu. Kwa uzoefu wangu, hicho ni kitu hakiwezi kutokea. Polisi ni ndugu zetu, marafiki zetu na majirani zetu. Tunajua fika ni watu wema.

Jeshi hili huwezi kulifananisha na kitu chochote. Tukiwa barabarani na vyombo vya moto, hawa ni ndugu zetu na marafiki zetu wakubwa. Ni nadra sana kumbugudhi Mtanzania mwenzao. Rushwa kwao ni mwiko. Ukijichanganya ukataka kumhonga kwa utovu wako wa nidhamu, unaweza kuishia gerezani kihalali kabisa.

Kusema ukweli, nina miaka zaidi ya 53 kwenye nchi hii na sijawahi kushuhudia askari akipokea rushwa ya namna yoyote ile. Nimesikia baadhi ya watu wanafiki wakisema eti huko kwenye hiyo taasisi kumetamalaki rushwa. Rushwa ipi kama si unafiki tu? Peleka ushahidi uone kama huyo askari atabaki kazini. Acheni kuongelea vichochoroni.

Maneno ya kusema eti Jeshi la Polisi linaendeshwa kwa msukumo wa chama tawala ni porojo tu hizi. Wameshasingiziwa makamanda wengi kujihusisha na chama hiki. Hata Balozi Sirro ameshawahi kueleza kuwa hizi ni porojo tu. Kwanini tusiwaamini? Hatuoni hii amani jamani, mbona hatuna shukurani? Mnataka watupe huduma gani waungwana hawa?

Ushauri wangu ni kuwa, kama kuna cheo zaidi ya IGP kwenye jeshi hilo, basi Camillus Wambura akitunukiwe.

Kwa leo maua yangu ni hayo
 
Hoja zako ni za kipumbavu na kijinga kabisa, hilo jeshi kama halihusiki lingekuwa limesha chukua hatua stahiki kama ambavyo huwa wanachukua hatua kwa matukio mengine wasiyo husika nayo. Kuto kuchukua hatua na kutoa utetezi wakijinga kwenye matukio ya utekaji na uuaji ni kupigia mstari uhusika wao.
Ndugu yangu, huoni kesi za kina Kibao, Soka na Deo Bonge zimekuwa solved? Hujaona tukipewa taarifa za matokeo ya uchunguzi na Jeshi la Polisi? Polisi wanafanya kazi nzuri aisee. Kwenye maua wape kama yalivyo.
 
Jeshi letu la Polisi ni jeshi zuri sana na huenda likawa ni lenye weledi na utashi kuliko yote Afrika Mashariki na Kati. IGP Wambura ni IGP Bora zaidi kuwahi kutokea katika historia ya nchi hii. Ana historia nzuri ya kushughulikia wahalifu na askari wakengeufu kila wanapojitokeza na ametengeneza Jeshi imara ambalo halisigani na wananchi. Ndiyo maana kila raia yupo huru katika kila kona za nchi hii. Hofu iliyokuwepo enzi na enzi haipo tena.

Hakuna mtu atatekwa au kunyanyaswa kwenye nchi hii kama kuna uwepo wa polisi maeneo hayo. Ni watetezi wetu tunaopaswa kuwakumbatia vema. Tunaona kila siku watu wanavyosafiri kwa amani toka maeneo mbalimbali na wanapata msaada wa polisi kila wanapouhitaji. Kwanini wasipate msaada wakati ni wananchi halali na watiifu kwa nchi yao?

Wapo washirikina fulani wanasema eti polisi wanakamata watu wakiwa hawajavaa sare za kazi. Jamani, wapi na lini umeona wakifanya hivyo? Hao ni wahuni tu wanaolenga kulisigina jina la jeshi letu. Kwa uzoefu wangu, hicho ni kitu hakiwezi kutokea. Polisi ni ndugu zetu, marafiki zetu na majirani zetu. Tunajua fika ni watu wema.

Jeshi hili huwezi kulifananisha na kitu chochote. Tukiwa barabarani na vyombo vya moto, hawa ni ndugu zetu na marafiki zetu wakubwa. Ni nadra sana kumbugudhi Mtanzania mwenzao. Rushwa kwao ni mwiko. Ukijichanganya ukataka kumhonga kwa utovu wako wa nidhamu, unaweza kuishia gerezani kihalali kabisa.

Kusema ukweli, nina miaka zaidi ya 53 kwenye nchi hii na sijawahi kushuhudia askari akipokea rushwa ya namna yoyote ile. Nimesikia baadhi ya watu wanafiki wakisema eti huko kwenye hiyo taasisi kumetamalaki rushwa. Rushwa ipi kama si unafiki tu? Peleka ushahidi uone kama huyo askari atabaki kazini. Acheni kuongelea vichochoroni.

Maneno ya kusema eti Jeshi la Polisi linaendeshwa kwa msukumo wa chama tawala ni porojo tu hizi. Wameshasingiziwa makamanda wengi kujihusisha na chama hiki. Hata Balozi Sirro ameshawahi kueleza kuwa hizi ni porojo tu. Kwanini tusiwaamini? Hatuoni hii amani jamani, mbona hatuna shukurani? Mnataka watupe huduma gani waungwana hawa?

Ushauri wangu ni kuwa, kama kuna cheo zaidi ya IGP kwenye jeshi hilo, basi Camillus Wambura akitunukiwe.

Kwa leo maua yangu ni hayo
Nimekuelewa hii Ndio kina Lucas Mwashambwa wanaipenda.
Maua Yako yamefika
 
Jeshi letu la Polisi ni jeshi zuri sana na huenda likawa ni lenye weledi na utashi kuliko yote Afrika Mashariki na Kati. IGP Wambura ni IGP Bora zaidi kuwahi kutokea katika historia ya nchi hii. Ana historia nzuri ya kushughulikia wahalifu na askari wakengeufu kila wanapojitokeza na ametengeneza Jeshi imara ambalo halisigani na wananchi. Ndiyo maana kila raia yupo huru katika kila kona za nchi hii. Hofu iliyokuwepo enzi na enzi haipo tena.

Hakuna mtu atatekwa au kunyanyaswa kwenye nchi hii kama kuna uwepo wa polisi maeneo hayo. Ni watetezi wetu tunaopaswa kuwakumbatia vema. Tunaona kila siku watu wanavyosafiri kwa amani toka maeneo mbalimbali na wanapata msaada wa polisi kila wanapouhitaji. Kwanini wasipate msaada wakati ni wananchi halali na watiifu kwa nchi yao?

Wapo washirikina fulani wanasema eti polisi wanakamata watu wakiwa hawajavaa sare za kazi. Jamani, wapi na lini umeona wakifanya hivyo? Hao ni wahuni tu wanaolenga kulisigina jina la jeshi letu. Kwa uzoefu wangu, hicho ni kitu hakiwezi kutokea. Polisi ni ndugu zetu, marafiki zetu na majirani zetu. Tunajua fika ni watu wema.

Jeshi hili huwezi kulifananisha na kitu chochote. Tukiwa barabarani na vyombo vya moto, hawa ni ndugu zetu na marafiki zetu wakubwa. Ni nadra sana kumbugudhi Mtanzania mwenzao. Rushwa kwao ni mwiko. Ukijichanganya ukataka kumhonga kwa utovu wako wa nidhamu, unaweza kuishia gerezani kihalali kabisa.

Kusema ukweli, nina miaka zaidi ya 53 kwenye nchi hii na sijawahi kushuhudia askari akipokea rushwa ya namna yoyote ile. Nimesikia baadhi ya watu wanafiki wakisema eti huko kwenye hiyo taasisi kumetamalaki rushwa. Rushwa ipi kama si unafiki tu? Peleka ushahidi uone kama huyo askari atabaki kazini. Acheni kuongelea vichochoroni.

Maneno ya kusema eti Jeshi la Polisi linaendeshwa kwa msukumo wa chama tawala ni porojo tu hizi. Wameshasingiziwa makamanda wengi kujihusisha na chama hiki. Hata Balozi Sirro ameshawahi kueleza kuwa hizi ni porojo tu. Kwanini tusiwaamini? Hatuoni hii amani jamani, mbona hatuna shukurani? Mnataka watupe huduma gani waungwana hawa?

Ushauri wangu ni kuwa, kama kuna cheo zaidi ya IGP kwenye jeshi hilo, basi Camillus Wambura akitunukiwe.

Kwa leo maua yangu ni hayo
Na haya uliyoandika ni porojo pia. Katika majeshi yaliyopo Tanzania Jeshi la Wananchi ndilo Jeshi lenye welding wa hali ya juu na wananchi wanajivunia Jeshi lao. Jeshi la polisi ni kinyume chake! IGP ana kazi kubwa ya kurejesha imani kwa wananchi.
 
Ndugu yangu, huoni kesi za kina Kibao, Soka na Deo Bonge zimekuwa solved? Hujaona tukipewa taarifa za matokeo ya uchunguzi na Jeshi la Polisi? Polisi wanafanya kazi nzuri aisee. Kwenye maua wape kama yalivyo.
Sarcastic kumbe, hatusomi miparagraph mirefu siku hizi hasa ikianza na heading zinazoelekea kwenye uchawa ati, sorry
 
Jeshi letu la Polisi ni jeshi zuri sana na huenda likawa ni lenye weledi na utashi kuliko yote Afrika Mashariki na Kati. IGP Wambura ni IGP Bora zaidi kuwahi kutokea katika historia ya nchi hii. Ana historia nzuri ya kushughulikia wahalifu na askari wakengeufu kila wanapojitokeza na ametengeneza Jeshi imara ambalo halisigani na wananchi. Ndiyo maana kila raia yupo huru katika kila kona za nchi hii. Hofu iliyokuwepo enzi na enzi haipo tena.

Hakuna mtu atatekwa au kunyanyaswa kwenye nchi hii kama kuna uwepo wa polisi maeneo hayo. Ni watetezi wetu tunaopaswa kuwakumbatia vema. Tunaona kila siku watu wanavyosafiri kwa amani toka maeneo mbalimbali na wanapata msaada wa polisi kila wanapouhitaji. Kwanini wasipate msaada wakati ni wananchi halali na watiifu kwa nchi yao?

Wapo washirikina fulani wanasema eti polisi wanakamata watu wakiwa hawajavaa sare za kazi. Jamani, wapi na lini umeona wakifanya hivyo? Hao ni wahuni tu wanaolenga kulisigina jina la jeshi letu. Kwa uzoefu wangu, hicho ni kitu hakiwezi kutokea. Polisi ni ndugu zetu, marafiki zetu na majirani zetu. Tunajua fika ni watu wema.

Jeshi hili huwezi kulifananisha na kitu chochote. Tukiwa barabarani na vyombo vya moto, hawa ni ndugu zetu na marafiki zetu wakubwa. Ni nadra sana kumbugudhi Mtanzania mwenzao. Rushwa kwao ni mwiko. Ukijichanganya ukataka kumhonga kwa utovu wako wa nidhamu, unaweza kuishia gerezani kihalali kabisa.

Kusema ukweli, nina miaka zaidi ya 53 kwenye nchi hii na sijawahi kushuhudia askari akipokea rushwa ya namna yoyote ile. Nimesikia baadhi ya watu wanafiki wakisema eti huko kwenye hiyo taasisi kumetamalaki rushwa. Rushwa ipi kama si unafiki tu? Peleka ushahidi uone kama huyo askari atabaki kazini. Acheni kuongelea vichochoroni.

Maneno ya kusema eti Jeshi la Polisi linaendeshwa kwa msukumo wa chama tawala ni porojo tu hizi. Wameshasingiziwa makamanda wengi kujihusisha na chama hiki. Hata Balozi Sirro ameshawahi kueleza kuwa hizi ni porojo tu. Kwanini tusiwaamini? Hatuoni hii amani jamani, mbona hatuna shukurani? Mnataka watupe huduma gani waungwana hawa?

Ushauri wangu ni kuwa, kama kuna cheo zaidi ya IGP kwenye jeshi hilo, basi Camillus Wambura akitunukiwe.

Kwa leo maua yangu ni hayo
Tatizo kubwa la CCM ni kupinga upinzani wakidhania wao wanayoyafanya yana haki ya kuungwa mkono na kila mtu.

Ukiiburuza nchi lazima zile sauti unazozinyima haki ya kuongea zitatafuta namna ya kusema hicho kinachotakiwa kusemwa hadharani.

Hilo ni kosa kubwa la CCM kuuchukulia upinzani kuwa ni uadui mbaya wakati ni haki ya kidemokrasia kwa jamii kuwa na makundi ya watu wenye akili zinazotofautiana.

Ukiunyima uhuru wa watu unainyima jamii nafasi ya kukua kimtazamo kwa ujumla. UK wanabadilisha serikali mara kwa mara na inawasaidia kwani hakuna serikali inayoingia madarakani ikaanza kubweteka kijinga tu.
 
Na haya uliyoandika ni porojo pia. Katika majeshi yaliyopo Tanzania Jeshi la Wananchi ndilo Jeshi lenye welding wa hali ya juu na wananchi wanajivunia Jeshi lao. Jeshi la polisi ni kinyume chake! IGP ana kazi kubwa ya kurejesha imani kwa wananchi.
IGP anatikiwa ashitakiwe yeye na Waziri wake pamoja na PM
 
Jeshi letu la Polisi ni jeshi zuri sana na huenda likawa ni lenye weledi na utashi kuliko yote Afrika Mashariki na Kati. IGP Wambura ni IGP Bora zaidi kuwahi kutokea katika historia ya nchi hii. Ana historia nzuri ya kushughulikia wahalifu na askari wakengeufu kila wanapojitokeza na ametengeneza Jeshi imara ambalo halisigani na wananchi. Ndiyo maana kila raia yupo huru katika kila kona za nchi hii. Hofu iliyokuwepo enzi na enzi haipo tena.

Hakuna mtu atatekwa au kunyanyaswa kwenye nchi hii kama kuna uwepo wa polisi maeneo hayo. Ni watetezi wetu tunaopaswa kuwakumbatia vema. Tunaona kila siku watu wanavyosafiri kwa amani toka maeneo mbalimbali na wanapata msaada wa polisi kila wanapouhitaji. Kwanini wasipate msaada wakati ni wananchi halali na watiifu kwa nchi yao?

Wapo washirikina fulani wanasema eti polisi wanakamata watu wakiwa hawajavaa sare za kazi. Jamani, wapi na lini umeona wakifanya hivyo? Hao ni wahuni tu wanaolenga kulisigina jina la jeshi letu. Kwa uzoefu wangu, hicho ni kitu hakiwezi kutokea. Polisi ni ndugu zetu, marafiki zetu na majirani zetu. Tunajua fika ni watu wema.

Jeshi hili huwezi kulifananisha na kitu chochote. Tukiwa barabarani na vyombo vya moto, hawa ni ndugu zetu na marafiki zetu wakubwa. Ni nadra sana kumbugudhi Mtanzania mwenzao. Rushwa kwao ni mwiko. Ukijichanganya ukataka kumhonga kwa utovu wako wa nidhamu, unaweza kuishia gerezani kihalali kabisa.

Kusema ukweli, nina miaka zaidi ya 53 kwenye nchi hii na sijawahi kushuhudia askari akipokea rushwa ya namna yoyote ile. Nimesikia baadhi ya watu wanafiki wakisema eti huko kwenye hiyo taasisi kumetamalaki rushwa. Rushwa ipi kama si unafiki tu? Peleka ushahidi uone kama huyo askari atabaki kazini. Acheni kuongelea vichochoroni.

Maneno ya kusema eti Jeshi la Polisi linaendeshwa kwa msukumo wa chama tawala ni porojo tu hizi. Wameshasingiziwa makamanda wengi kujihusisha na chama hiki. Hata Balozi Sirro ameshawahi kueleza kuwa hizi ni porojo tu. Kwanini tusiwaamini? Hatuoni hii amani jamani, mbona hatuna shukurani? Mnataka watupe huduma gani waungwana hawa?

Ushauri wangu ni kuwa, kama kuna cheo zaidi ya IGP kwenye jeshi hilo, basi Camillus Wambura akitunukiwe.

Kwa leo maua yangu ni hayo
Nimesoma mahali eti una miaka 53 na hujawahi kuona polisi wakipokea rushwa. Bila shaka wewe kama siyo mnafiki basi siyo mzima kichwani.
Hivi wakati wale wachimba madini wa Ulanga wanauawa na timu ya akina Zombe,ulikuwa Mirembe? Wale askari waliotajwa kuhusika na kifo cha kijana mchimba madini Songea bado ulikuwa haujapona?
Shambulizi la aibu dhidi ya Lisu, ambalo hata huyo Wambura wako anaogopa kulizungumzia, bado unajiona ni mzima wewe!!! Mzee Kibao je!! Umesikia nani kakamatwa!!
 
Na haya uliyoandika ni porojo pia. Katika majeshi yaliyopo Tanzania Jeshi la Wananchi ndilo Jeshi lenye welding wa hali ya juu na wananchi wanajivunia Jeshi lao. Jeshi la polisi ni kinyume chake! IGP ana kazi kubwa ya kurejesha imani kwa wananchi.
IGP hajarejesha tu, bali pia ameikuza amani. Umesikia kuna mtu anatekwa akiwa anapata mvinyo wake baa? Umewahi kuona hilo likitokea? Umewahi kuona mtu anasafiri zake anashushwa kwenye gari na kukutwa amekufa baadaye? Kama kuna sehemu umeona au kusikia mambo hayo, basi si Tanzania. Na kama imewahi kutokea Tanzania, basi lazima uchunguzi umefanyika na watuhumiwa tayari wanakabiliwa na mkono wa sheria. Nchi imetulia hii.
 
Igp na vijana wake wanafanya vyema KAZI waliyosomea.
 
Jeshi letu la Polisi ni jeshi zuri sana na huenda likawa ni lenye weledi na utashi kuliko yote Afrika Mashariki na Kati. IGP Wambura ni IGP Bora zaidi kuwahi kutokea katika historia ya nchi hii. Ana historia nzuri ya kushughulikia wahalifu na askari wakengeufu kila wanapojitokeza na ametengeneza Jeshi imara ambalo halisigani na wananchi. Ndiyo maana kila raia yupo huru katika kila kona za nchi hii. Hofu iliyokuwepo enzi na enzi haipo tena.

Hakuna mtu atatekwa au kunyanyaswa kwenye nchi hii kama kuna uwepo wa polisi maeneo hayo. Ni watetezi wetu tunaopaswa kuwakumbatia vema. Tunaona kila siku watu wanavyosafiri kwa amani toka maeneo mbalimbali na wanapata msaada wa polisi kila wanapouhitaji. Kwanini wasipate msaada wakati ni wananchi halali na watiifu kwa nchi yao?

Wapo washirikina fulani wanasema eti polisi wanakamata watu wakiwa hawajavaa sare za kazi. Jamani, wapi na lini umeona wakifanya hivyo? Hao ni wahuni tu wanaolenga kulisigina jina la jeshi letu. Kwa uzoefu wangu, hicho ni kitu hakiwezi kutokea. Polisi ni ndugu zetu, marafiki zetu na majirani zetu. Tunajua fika ni watu wema.

Jeshi hili huwezi kulifananisha na kitu chochote. Tukiwa barabarani na vyombo vya moto, hawa ni ndugu zetu na marafiki zetu wakubwa. Ni nadra sana kumbugudhi Mtanzania mwenzao. Rushwa kwao ni mwiko. Ukijichanganya ukataka kumhonga kwa utovu wako wa nidhamu, unaweza kuishia gerezani kihalali kabisa.

Kusema ukweli, nina miaka zaidi ya 53 kwenye nchi hii na sijawahi kushuhudia askari akipokea rushwa ya namna yoyote ile. Nimesikia baadhi ya watu wanafiki wakisema eti huko kwenye hiyo taasisi kumetamalaki rushwa. Rushwa ipi kama si unafiki tu? Peleka ushahidi uone kama huyo askari atabaki kazini. Acheni kuongelea vichochoroni.

Maneno ya kusema eti Jeshi la Polisi linaendeshwa kwa msukumo wa chama tawala ni porojo tu hizi. Wameshasingiziwa makamanda wengi kujihusisha na chama hiki. Hata Balozi Sirro ameshawahi kueleza kuwa hizi ni porojo tu. Kwanini tusiwaamini? Hatuoni hii amani jamani, mbona hatuna shukurani? Mnataka watupe huduma gani waungwana hawa?

Ushauri wangu ni kuwa, kama kuna cheo zaidi ya IGP kwenye jeshi hilo, basi Camillus Wambura akitunukiwe.

Kwa leo maua yangu ni hayo
Umesema kwel ila sehem zingine haukusema kwel hasa kweny suala la rushwa ungesema kwel tu,, mbona wenyew Kwa wenyew wamefukuzana Kwa rushwa iweje ww ukate hakuna?
 
Huwezi kupongeza ujinga, ni sahihi watu wanavyotekwa na kuuawa na wengine kupotezwa mazima wanaacha familia zao zikiwa masikini na yatima? Kuna mtu anaweza kupata ujasiri wa kuteka mtu mbele ya Stand ya Magufuli live na huku kuna CCTV camera? wengine kushushwa kwenye mabasi? kama polisi wana nia njema kwanini wasipige marufuku polisi kukamata mtu bila uniform na kitambulisho na watoe taarifa kwa VEO/WEO/Mwenyekiti au diwani? ili watekaji wasitumie mwanya huo!
Bw. Benja nashindwa niseme nini unielewe. Hizi zote ni hila tu za kulichafua Jeshi. Hata hili la Nondo watalishughulikia na wahalifu watakamatwa. Huoni wahalifu waliomuua Mzee Kibao tayari tumekamata? Huoni wale vijana waliomteka Deo Bonge wameshafunguliwa kesi mahakamani? Usiniambie una upofu wa kiasi hicho, Benja.
 
Tesla Robots zikiamriwa zikumalize umekwisha.
images (5).jpeg
 
Back
Top Bottom