Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
NCAA katika taarifa yao hiyo, imesema kuwa, Watalii kutoka ndani na nje ya nchi wameendelea na safari zao za kushuhudia vivutio vya utalii ndani ya Hifadhi na Serikali inaendelea kuwahakikishia usalama wao.
"Maandamano yaliyoripotiwa kupitia baadhi ya mitandao ya kijamii yanaidhihirishia dunia na jumuiya za kimataifa, vyombo vya habari na asasi za kimataifa kwamba ndani ya Hifadhi hiyo hakuna ukiukwaji wa haki za binadamu na unyanyasaji wa wananchi.
Mamlaka inawahakikishia watalii wote waliopanga safari za kuja Ngorongoro kuwa Serikali itaendelea kusimamia usalama wao wakati wote watakapokuwa ndani ya hifadhi." Imebainisha taarifa hiyo iliyotolewa na Hamis Dambaya, Kaimu Meneja , Kitengo cha Uhusiano kwa Umma wa NCAA.
Pia soma ~ Wamasai Ngorongoro wamechoka kunyang’anywa ardhi yao na kupewa Mwarabu, Wameamua liwalo na liwe