Wasijemuwekea sumuLeo tarehe 10.9.2024 Mzee Butiku amezungumza na Waandishi wa habari kuhusu sintofahamu zinazoendelea hapa nchini.
Kwanza nikupongeze sana Mzee Butiku kwa busara, hekima zako kwa kuishauri Mamlaka kwa yanayoendelea kwa sasa hapa nchini kwetu.
Mzee ameshauri kwa Mamlaka ya juu ya nchi kuwa wale wote ambao wanasimamia vyombo vya usalama WAWAJIBIKE kwa tukio la aibu lililotokea hivi majuzi.
Watanzania tudumishe Amani, upendo na mshikamano.
PIA SOMA
- Joseph Butiku: Vyombo vya ulinzi na usalama visijifanye havijui mambo yanayoendelea nchini
Je alicho ongea leo hakina mantiki?Huyu Butiku ambaye hata taasisi ya Mwalimu Nyerere imemshinda? Imebaki kuvizia matukio, kaigeuza kikao cha kahawa, au cha matambiko ya wazanaki. Mimi mpaka leo sijui uongozi wa hii taasisi una nani na nani, na kwa nini Butiku haachii ngazi. Mfano bora ni Benjamin Mkapa Foundation. Butiku kabakiza kutumia jina la Nyerere kuomba hela kwa wachina tu halafu anaenda kuzificha, na pia kuomba skolaship za wqjukuu zake China, kasahau watanzania wengine
Ondoa majina ya hao wazee wengine wanaojali maslahi yao binafsi na siyo ya Taifa, labda bakiza la Mzee mmoja tu kati ya hao ambaye amenyooka na haogopi kutoa maoni yake katika kilitetea Taifa letu mama .Wazee wengine kina Warioba, Wasira, Msuya, Sumaye na Jakaye Kikwete wanasema je?