Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) yakamata Kilogramu 2,327,983.66 za Dawa za Kulevya 2024, idadi ambayo haijawahi kufikiwa

Ojuolegbha

JF-Expert Member
Joined
Sep 6, 2020
Posts
1,278
Reaction score
797
Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) yakamata Kilogramu 2,327,983.66 za Dawa za Kulevya 2024, idadi ambayo haijawahi kufikiwa tangu kuanza kwa mapambano haya nchini.

Dawa zilizokamatwa zilijumuisha bangi aina ya skanka na hashishi, methamphetamine, heroin, na dawa tiba zenye asili ya kulevya.

Pakua Samia App kupitia Play Store au App Store.

#samiaapp
#kaziiendelee
#tumejipatanamama
 

Attachments

  • VID-20250220-WA0061.mp4
    13.6 MB
Kwa Tanzania Itakuwa gundi za kunusa, makopo ya rangi, madumu ya petrol, mirungi, bangi na shisha.

Tanzania haiwezi kuwa kitovu cha madawa ya kulevya ya ukweli kama Colombia, Ecuador, Guatemala, Mexico, Afghanistan n.k
 
Hizi data Zina harufu ya upikwaji
Huoni hapo mwisho amempigia chapuo HAngaya na app yake?

Lengo lilikuwa kuitangaza hiyo app sasa alijua akiweka tangazo la app lenyewe kama lenyewe watu makini wasingeweza kufungua uzi wake so akaona achombeze na habari ya kuokoteza yenye mashiko ambayo kiuhalisia haina maana.
 
Wanatumia nguvu nyingi kumpamba hangaya lakini wapi
 
Dawa zinazokamatwa hazifiki hata theluthi ya zinazoingia mtaani.
 
Kilograms milioni 2.3 yaani tani 2300? Haya madawa yamehifadhiwa wapi? Lini yaliteketezwa? Yaani mzigo huu ni wa kubebwa na malori karibia 130 ya tani 15 kila moja. Huu ni uongo mkuu.

Watanzania wa Sasa siyo wajinga
Madawa ya Kulevya yana include Bangi na Mirungi, na sio "unga" pekee. Shamba moja tu la Bangi ama Basi likikamatwa na Mirungi mzigo unakua si wa kitoto.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…