Man City, PSG na Juventus ni timu zenye mikosi kwenye kombe la UCL

Hakuna cha matambiko wala nini, itoshe tu kusema kuwa Mwacity na kocha lake libaguzi likuu la rangi na utaifa "Pep Kipara" wasiendelee kuvimba mabichwa kuwa ni timu kubwa saaana la hasha! bali uzuzu wa pesa za Waarabu kwa fitina zao ndiyo unawasumbua tu.

Pep Kipara awaombe radhi Samuel Eto'o na Yaya Toure kuhusu ubaguzi wa rangi (uafrika) labda laana asilia ya ulimwengu itamkumbuka kumpatia kombe la UEFA champions league [emoji847]
 
Ametwaa Sana na Bercelona,bado Kwa Man City
 
Kwa kweli hizo timu hazina bahati kabisa heri hata man city huwa anajikongoja kidogo ila hao wengine ndo hawana bahati kabisa
 
Man City binafsi naona bado ni timu nzuri hata kaliba ya wachezaji walionao ni mapema kuwapima kwa mechi kubwa na timu kubwa duniani kama Real Madrid siku za usoni tutarajie makubwa kwao.

PSG hawana tofauti na Man City tofauti ni ndogo sana. Don Carlo Ancelotti akiwa kocha wa PSG aliwahi kuambiwa na Al Khelafi kama watatole na FC Porto basi hana kibarua. Don alishangazwa na kauli kwanza aliona hana umuhimu wa kuwa hapo isipokuwa mafanikio yananuliwa. Mpira na uwekezaji wake ni project inayohitaji muda mrefu hayapimwi na mchezaji mmoja mmoja kuwa na Messi, Mbappe na Neymar haitoshi unahitaji kuwa na watu zaidi ya timu.

Juventus kuna muda unashindwa kuwaelewa project yao nini ? Kibibi kizee cha Turin wakati wanafanya usajili wa Dusan Vlahovic , akiwa mfungaji anayeongoza kwa magoli kwenye ligi anashindwa kufunga kwa kukosa mtu anayeleta muungano kati yake na Dusan. CR7 akiwa Juventus wakicheza dhidi ya Ajax wakiwa na De Ligt, Ziyech na Tadic wanakufa 2-1 Turin unaona kabisa timu haichezi wote wanamuangalia CR7 unahitaji zaidi ya timu linapokuja suala la mashindano makubwa kama UEFA CL. Siku za usoni uwekezaji wao utawalipa kama watafanya mbadala wa Bonucci,Chiellini, Sandro, Dybala anahitaji changamoto mpya, Cuadrado pia si mbaya akapewa mkono wa kwa heri. Nakuruhu damu kama Demiral , Chiesa, Dusan na kina Locatteli nakuongeza sura mpya za wapamabanaji kama kina Scamacca.
 
Man city hapo walipo ni kwenye peak maana wachezaji wao wengi hodar umri umewatupa mtu kama KDB wa Sasa sio yule wa miaka miwili iliyopita unamuona anakimbia Kila sehemu mpaka uso unakuwa mwekundu.
 
Wote hao wamefika hatua za nusu fainali au fainali kwa kukutana na timu nzito zinazojua kucheza mechi kubwa na muhimu,hapo hakuna kukosa bahati bali ni suala la kuzidiwa uwezo na maarifa...huwezi kufungwa na timu Kariba ya real Madrid au Bayern munchen then ikasemwa ni bahati tu ndo hatuna,kila mmoja anafahamu namna timu Kariba Kama ya r.madrid inavyocheza katika hatua muhimu Kama hizi,kiasi ambacho hata ukishinda basi unajipongeza kuwa ww ni mwanaume...
 
Man city hapo walipo ni kwenye peak maana wachezaji wao wengi hodar umri umewatupa mtu kama KDB wa Sasa sio yule wa miaka miwili iliyopita unamuona anakimbia Kila sehemu mpaka uso unakuwa mwekundu.
Marco Polo:

😃😃 hakika, ila umri umeonekana ni namba angalia shughuli ya CR7 ,Messi, Luke Modric , Benzema n.k. Wana kina Foden, na kuna vijana wengi wamewandaa acha vijana kama kina Alvarez kutoka River Plate ambaye walimnunua kisha wakamuacha kwa mkopo. Ila falsafa ya Gurdiola siku zote inafahamika.

Cha kujiuliza ni kwamba Pep kweli ameshindwa kukifanya alipokuwa Barca ? Achilia watu aliokuwa nao Messi, Xavi na Iniesta. Maana tumeona pia Bayern Munchen mambo yalimuendea kombo ?
 
Wakati wewe mwafrika ukiendelea kuwaza porojo zinazoitwa laana mwenzako anaenda kujiuliza walipokosea mwakani anarudi tena kwenye mashindano.Hizi myth ni porojo tu zasisi tusioweza chochote au kua na fikra za mambo makubwa.Ndo maana tunaowawazia huo ujinga wao wala hawana huo muda.
 
Madrid ana kisimati akifika fainali sijui inatokea nini
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…