MAN UTD VS MAN CITY: Somo jipya la uamzi.

Bila bila

JF-Expert Member
Joined
Dec 20, 2016
Posts
22,168
Reaction score
39,118
Siku zote Kwa watu Wenye busara tatizo huzaa Somo.

Jana Mwamuzi Stuart Antwel akishirikiana na Waamuzi wa VAR kwenye Mechi ya Mahasimu wa Manchester ameanzisha mtifuano wa hoja dunia nzima. Amewapa watunga sheria na kanuni kazi ya kufanya.

Mpaka Sasa Kila upande Una lake, Hakuna anayekubali kushindwa.

Mwamuzi mstaafu wa England Dermont Gallagher yeye kasema suala lile maamuzi yoyote ya mwamuzi yalikuwa sahihi.

Maamuzi kama haya ndo sehemu sahihi Kwa Waamuzi wetu kuingia darasani na kutuletea maoni sahihi ya "Ni offside au siyo offside?" Rashford anapewa pasi akiwa eneo la kuotea na mpinzani wake Akanji akiwa Mita 4 toka kwenywe mpira na 2 toka Kwa Rashford.

Mfukuzano huo unakwenda umbali wa zaidi ya Mita 20 bila yeyote Kati Yao kugusa mpira wala Akanji kimkaribia Rashford. Wanapokaribia eneo la 18 ghafla anatokea Fernandes na Kupiga mpira ule golini na kufunga.

Unazuka utata ni goli halali au haramu? Antwel anawasiliana na VAR officials kujiridhisha kama mpira uliguswa na Rashford au la? Wao pamoja na Mashika kibendera No. 2 wanasema Rashford hakugusa mpira Kwa umbali wote wa zaidi ya Mita 20 alizofukuzana na mpira ule.



Baada ya maelekezo hayo anaruhusu bao Kwa Man Uta lakini anapingwa vikali na Man City.

Watu wanarudi kwenye kanuni lakini nazo zinazidisha mkanganyiko tu maana Kila mmoja anazituzitumia kuvutia upande wake.

Nani atatutalia Fumbo hili? Ni Peluig Collina au Ramadhani Kayoko? Ni Athumani Kazi au Scars wa JF? Tusubiri huku tukiendelea kutoa maoni Kwa kutumia vielelezo na hoja jadidi.

 
Sasa hizo kanuni zinaleta mkanganyiko gani zaidi? Wakati ukizisoma ni wazi kabisa ilikuwa ni offside
 
Hapa Rashford alikuwa kwenye eneo la kuotea wakati mpira ukiwa unachezwa eneo la mbali kutoka kwake





Rashford hakuugusa ule mpira japo alionekana yupo jirani sana na mpira almost kuugusa


Tukija kwenye sheria za Offside

Sheria namba 11.2 kuhusu offside inasema

Mchezaji aliyepo katika nafasi ya kuotea wakati mpira upo katika umiliki wa wachezaji wa timu yake atahusika moja kwa moja kuwa ni offside offence iwapo

  • Kuingilia mchezo kwa kuucheza au kuugusa mpira uliopigwa na team mates wake (kitu ambacho sio kweli maana Rashford hakuugusa wala kuucheza mpira)
  • Kumuingilia mpinzani kwa
  1. kumzuia mpinzani asiucheze mpira au kumuwekea kizuizi cha wazi kinachoonesha lengo la kumzuia (Rashford hakuweka kizuizi)
  2. Kum challenge mpinzani kwa mpira au kufanya jaribio la wazi la kuucheza mpira ambao upo karibu wakati kitendo hiki kitaonekana kuwa na athari kwa mpinzani (Rashford hakuvunja sheria hii pia)
  3. Kufanya kitendo chochote ambacho kitakuwa na athari ya wazi kwenye uwezo wa mpinzani kuucheza mpira (Sheria hii inampa faida Rashford)
 
KWAMBA DUNIA NZIMA VILAZA ILA NI WEWE TU NDIO UNAJUA
Kwani dunia nzima imekubali, haijapinga? Hata kama wangekuwa wote wanakubali mie ningesimamia ninachokiamini
 

Attachments

  • 20230115_093856.jpg
    50.1 KB · Views: 6
Kwani dunia nzima imekubali, haijapinga? Hata kama wangekuwa wote wanakubali mie ningesimamia ninachokiamini
Kuna haka katafsiri ka natembea wenyewe walikuwa wanajadili wanasema "mshambuliaji aliye kwenye nafasi ya kuotea akiwa anakimbia kuelekea kwenye mpira uliopigwa yeye akiwa tupo kwenye nafasi ya kuotea, lakini akatokea mchezaji wa timu yake ambaye hayupo kwenye nafasi ya kuotea akaucheza huo mpira basi hiyo haitahesabiwa kama ni offside"

 
Ile ni offside uwepo wa Rashford ulizuia Akanji kuufikia mpira na kunufaisha timu yake,kweli sheria inasema kuwa katika eneo la kuotea sio dhambi dhambi ni timu yako kunufaika wewe mchezaji kuwa katika eneo hilo,na kweli Manure jana walinufaika kwa uwepo wa Rashford pale mbele kwani ali ugard mpira nahivyo kuipa advantage timu yake ile jana inafanana na shuti likipigwa mchezaji aliyeotea akaziba vision ya kipa kuuona mpira hata kama hajaugusa ila kwakua atamzuia kipa kuona mpira itatafsiriwa kuwa ameotea na jana Rashford alizuia mpira usipotee kwa kuu guard ivyo Akanji akashindwa kuuchukua mpira.

Sent from my SM-G9650 using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…