Pre GE2025 Manara: Utani wa Simba na Yanga umesaidia kuleta Utulivu nchini, utakuta Maji, Sukari na Umeme hakuna lakini Media zinajadili Simba na Yanga!

Pre GE2025 Manara: Utani wa Simba na Yanga umesaidia kuleta Utulivu nchini, utakuta Maji, Sukari na Umeme hakuna lakini Media zinajadili Simba na Yanga!

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Katibu Uenezi wa CCM mkoa wa DSM mstaafu Alhaj Hajji Manara amesema Utani wa Simba na Yanga umesaidia kuleta Utulivu nchini na Serikali inauunga mkono 100%

Manara amesema unaweza kukuta Maji hakuna, Umeme hakuna, Sukari hakuna lakini Wananchi kwenye mitandao ya Kijamii wako busy kuwajadili Pacome na Chama nani mkali

Manara amesema Utani wa Simba na Yanga umefanya Siasa za Tanzania kuwa nyepesi na rahisi sana

Credit: Mfanyakazi Online

Baadae Mlale Unono 😀😀🔥

======

Utani wa Simba na Yanga umesaidia kuleta utulivu katika Siasa za Tanzania na Serikali inauunga mkono kwa asilimia mia kwa sababu kuna wakati ajenda inakuwa Simba na Yanga lakini huku umeme hakuna, maji yamekatika huku sukari hamna lakini watu wanafocus na Pacome na Chama nani zaidi, umeme hakuna, maji hakuna, sukari iko juu lakini ajenda kwenye Social media watu Pacome na Chama nani zaidi.

Pia soma:Mahakama yaamuru Eng. Hersi aachie ngazi Yanga!
 
Ofcoz Simba na Yanga zinatumuka. Ndio maana leo stori ya Magoma na Yanga imetengenezwa ili kufanya diversion ya stori ya Nape anavyotuibiaga kura.

Na kwasababu watanzania hawajui kinachoendelea huku duniani, kila kitu kwao poa tu na ndo maana Nape sio mara ya kwanza wala ya mwisho kutuambia hivyo kwasababu anajua hata atuambie nini, hatuwezi mfanya chochote. Safi sana Nape
 
Mpaka uwe na Akili kubwa ndiyo utajua kauli hii ya manara... Angalia Leo watanzania wote wamehamishwa kutoka Kwa NAPE Hadi YANGA.
Nchi hii ni UJINGA mtupu watu wanajadili kutoka asubuhi vipindi vyote redioni ni michezo,udaku na michezo tena usiku. CCM wamafanikiwa pakubwa Sana kuwaingiza watu wake kwenye UJINGA
 
Inasikitisha ila ndo ukweli.

Vijiwe ambavyo vingekua vya vijana kupeana ushauri na madili vimegeuka vya ubishani wa simba na Yanga
 
Hii video inaeleza/fafanua mambo mengi sana yanayotrend..

NB zingatia na hukumu ya kina mzee magoma tangu august 2023 na kukamata trend sasa hivi.[URL

======
Utani wa Simba na Yanga umesaidia kuleta utulivu katika Siasa za Tanzania na Serikali inauunga mkono kwa asilimia mia kwa sababu kuna wakati ajenda inakuwa Simba na Yanga lakini huku umeme hakuna, maji yamekatika huku sukari hamna lakini watu wanafocus na Pacome na Chama nani zaidi, umeme hakuna, maji hakuna, sukari iko juu lakini ajenda kwenye Social media watu Pacome na Chama nani zaidi.
 
Mbona saivi ccm wameanza kuongea ukweli Kuna nn? Juzi nape kasema wanaibaga kura, Leo huyu kasema hivyo. Hii naona na dalili njema sana.
Hahaha imani ya wao kwa wao imeisha kila mmoja anamuangalia mwenzake kwa jicho la macho kumchuzi
 
Siasa ni trust, hakuna hao wanasiasa wenye nguvu hiyo ya ushawishi Tanzania (demagogue politics, Magufuli kidogo ndio alifanya watu kuwa interested).

Ndio maana wananchi hawajali sio kwamba wanafurahia shida. Akitokea mtu wa kuaamsha wataamka tu.

Vinginevyo jaribu kutafuta sports radio za wazungu usikilize povu la team zao siku ikifungwa, kuna mashabiki wanasafiri na team msimu mzima.

Ushabiki wa mpira uingereza ni kama dini ndio maana makocha hawadumu; na siasa ina nafasi vilevile. Wanasiasa waache kulaumu raia ambao hawajui haki zao kwa kushindwa kazi kuelemisha jamii.
 
Mambo haya tumekuwa tukiyaongelea sana humu JF sasa yamedhihirika.
 
Manara apuuzwe tu.....! Huko alipo Wote Mazuzu watupu isipokuwa Baba yake na JK tu
 
Katibu Uenezi wa CCM mkoa wa DSM mstaafu Alhaj Hajji Manara amesema Utani wa Simba na Yanga umesaidia kuleta Utulivu nchini na Serikali inauunga mkono 100%

Manara amesema unaweza kukuta Maji hakuna, Umeme hakuna, Sukari hakuna lakini Wananchi kwenye mitandao ya Kijamii wako busy kuwajadili Pacome na Chama nani mkali

Manara amesema Utani wa Simba na Yanga umefanya Siasa za Tanzania kuwa nyepesi na rahisi sana

Credit: Mfanyakazi Online

Baadae Mlale Unono 😀😀🔥
Na huo ndio uzezeta wa wabongo,kwani kwenye uchafuzi huu anachukua jimbo gani?
 
Manara yupo sahihi,niliwahi kulisema hili miaka kadhaa nyuma.

 
Back
Top Bottom