tc_edo
Senior Member
- Apr 9, 2021
- 123
- 98
Baada ya kumaliza msimu (2020 /2021) bila kombe na kupoteza mchezo wa fainali, jumatano 26 mei 2021 dhidi ya Villareal; Manchester United inategemea kumwongezea Koche Ole Gunnar mkataba wa miaka mitatu na kumuunga mkono kusajili wachezaji hadi wanne. Tokea achukue majukumu ya ukocha 2019 Solskjaer amepambana na kufanikiwa katika kukijenga kikosi cha Mashetani wekendu na bado hajakata tamaa.
"Tangu Ole aingie kulikua na project na wachezaji wanaamini katika mfumo huo na huu sio mwisho wa mfumo huo maana kila mfumo una milima na mabonde. Nawaahidi mashabiki hatutokata tamaaa ingawaje tumepoteza fainali." Marcus Rashford akiongea baada ya mchezo wa Fainali.
Upana wa kikosi kwa Manchester United umekua tatizo hasa wachezaji wa pembeni, beki ya kati, mshambuliaji na kiungo hivyo kufanya uhitaji wa usajili wa hadi wachezaji wanne. Nyota wa Borussia Dortmund, Jadon Sancho ni miongoni mwa wachezaji wanaowindwa na Manchester United.
Beki wa kati wa Villareal, Pau Torres nae yupo kwenye rada ya Manchester United. Pia tetesi zinaonesha Declan Rice mchezaji wa kati wa West Ham na Ruben Neves wa Wolves ni viungo wanaoweza sajiliwa na United. Erling Haaland ni mshambuliaji ambae United imekua ikimuangalia kwa muda kidogo na kuona akifaa kama straika wako, pia Harry Kane anaondoka Tottenham hivyo yupo sokoni.
"Tangu Ole aingie kulikua na project na wachezaji wanaamini katika mfumo huo na huu sio mwisho wa mfumo huo maana kila mfumo una milima na mabonde. Nawaahidi mashabiki hatutokata tamaaa ingawaje tumepoteza fainali." Marcus Rashford akiongea baada ya mchezo wa Fainali.
Upana wa kikosi kwa Manchester United umekua tatizo hasa wachezaji wa pembeni, beki ya kati, mshambuliaji na kiungo hivyo kufanya uhitaji wa usajili wa hadi wachezaji wanne. Nyota wa Borussia Dortmund, Jadon Sancho ni miongoni mwa wachezaji wanaowindwa na Manchester United.
Beki wa kati wa Villareal, Pau Torres nae yupo kwenye rada ya Manchester United. Pia tetesi zinaonesha Declan Rice mchezaji wa kati wa West Ham na Ruben Neves wa Wolves ni viungo wanaoweza sajiliwa na United. Erling Haaland ni mshambuliaji ambae United imekua ikimuangalia kwa muda kidogo na kuona akifaa kama straika wako, pia Harry Kane anaondoka Tottenham hivyo yupo sokoni.