Maneno mapya unayopaswa kuyatumia wakati wa kutongoza

Ben Zen Tarot

JF-Expert Member
Joined
Dec 13, 2014
Posts
4,298
Reaction score
7,612
Ili uweze kumpata kirahisi mwanamke unayemtaka unatakiwa kujifunza mbinu mpya za kutongoza. Wengi wanashindwa kuwapata watoto wanaowapenda kwa sababu ya kutumia maneno ya kawaida au ambayo yamepitwa na wakati.

Hivyo ili uweze kumpata mwanamke unayempenda kwa dhati basi unatakiwa kujifunza kutumia maneno yafuatayo;

1. Nipe makinikia ya moyo wako.

2. Naahidi kulipa mirahaba yako na kodi zote za mapenzi.

3. Sitakudanganya kiwango cha madini kilichoko kwenye mchanga wa madini ya mapenzi kama acacia.

4. Please usizuie contena la mchanga wa madini ya penzi langu kwenye bandari ya moyo wako.

5. Usiniundie kamati za marafiki zako kufanya uchunguzi wa makanikia ya upendo wangu.

6. Usinitangaze kuwa naiba utajiri wa mgodi wa moyo wako hadharini mbele ya vyombo vya habari.

7. Nitakuomba ukae kwenye meza ya mazungumzo ili uniruhusu kuchimba sukari ya moyo wako.

8. Usiwahusishe viongozi wastaafu ma X wako katika ombi langu sababu wengine watakuwa walikusainisha mikataba mibovu ikakuumiza na wengine wamepumzika baada ya kazi kubwa ya kulijenga taifa la moyo wako.
 
 
Mpenzi lenye kiwango cha makinikia
 
Nilivyokuja mbio nikajua kuna la maana kumbe [emoji706][emoji706][emoji706]
 
Daah me cjawah tongoza dem kwa maneno! Me nkimpend dem namchek namwambia naomba nkutoe out siku flan mfano weekend, tukiwa out namsoma kupitia maongezi yetu then baada ya hapo namwambia twende home ukapajue akikubali imeisha maan lazma nifanye harakati za kula mzigo!
 
Duh ngoja nikafanye practical kwa manzee
 
We jamaa lazima utakua ni mchimbaji mdogomdogo
 
Tafuta pesa, achana na mashairi yanapoteza muda na zama zake zishapita.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…