MANENO MENGINE!!... Nini maana na asili ya maneno haya??

MANENO MENGINE!!... Nini maana na asili ya maneno haya??

WomanOfSubstance

JF-Expert Member
Joined
May 30, 2008
Posts
5,457
Reaction score
963
Leo nilikuwa kwenye ibada, ikawepo haja ya kutafsiri neno "Ghost" basi mhubiri akasema "Mzuka"... mbona miguno na vicheko vilitawala!

Nikawa najiuliza mhubiri hajui kuwa "Mzuka" ina maana tofauti kabisa?

Nikazidi kujiuliza, kuna maneno mengi tu siku hizi ukiyatamka watu hupata maana tofauti.
Mfano mzuri ni tangazo la radio kuhusu utumiaji wa pombe.."ulevi noma!".... hili tangazo kuna siku lilizusha mjadala mkali sana.Vijana walikwa wanashangaa iweje tangazo la polisi kusifia pombe?...

Wajuzi hebu tuangalie baadhi ya maneno yenye maana zaidi ya moja tena maana zenye kukinzana.

1. Mzuka -inamaanisha mtu aliyekufa lakini pia lina maana nyingine kabisa ....
2. Noma - hebu tufafanulieni maana yake...
Ongezeeni na mengine.

Inawezekana kabisa kukawa na thread yenye kuzungumzia jambo hili.Kama ipo basi naomba mods muunganishe lakini tuendelee kupeana shule ya kiswahili.

Asanteni
 
Lakini hapo kwenye 'mzuka' mhubiri wala hajakosea. Huenda wanamaombi wengi ndo hawajui maana halisi ya hilo neno na wanachojua ni ile maana ya mtaani.
 
Waumini walichekelea ujinga wao coz hata kama utaondoa maana halisi ya kilugha ya mzuka wangepaswa kufahamu pia mtumiaji wa lugha husika ana fursa maalum ya kutumia lugha atakavyo kimazungumzo ambayo italenga maana nyengine tofauti anayoikusudia. mf. ninapomuita mtu shetani nini maana ya ndani ninayoikusudia.. hayo mahubiri yalikua vijijini nini?
 
Sijui kama nitakuwa nimechangia kwa mujibu wa mada, lakini nafikiri mara nyengine hiii husababishwa na tabia yetu ya kutafsiri dhana za Kiingereza katika Kiswahili chetu.
Fikiria maeneo au dhana hizi.
- Amehukumiwa "chini" ya kifungu cha Sheria Nambari XYZ ya makosa ya jinai. Hapa neno chini tumechukua toka Kiingereza under wakati kwa Kiswahili halileti maana yoyote. Neno lingefaa zaidi ni "kwa mujibu wa".
- "Mwisho wa siku" yeye ndiye atakaye athirika- tumekuwa tukitumia maneno at the end of the day pengine hata hatujui tunasema nini. Kwa nini basi tusitumie maneno kama mwisho wa wiki, mwezi na mwaka?. Neno mwisho peke yake lingetosha. Nakumbuka pia zamani, kabla ya "mwisho wa siku" watu walikuwa wanatumia "Mwiso wa yote/Baada ya yote" au "Mwisho wa habari".
 
Noma: (Ni neno la kiswahili) Uzuizi, Uzuivu, Upinzani, Pingamizi, Mkingamo, Mkinga, Mgogoro, Uzuio, Masumbuo, Sumbuo, uzuwiaji, Uzuiaji, Masumbulizi, Kipingamizi, Masumbufo, Makinzano, Mfungizo, Kizuio, Kizuizi, Kikwazo, Masubuko.

Ghost: Mzimu, Mzuka, Zuka, Zimwi, Njozi, Kizuka, Kivuli, Masuka, Pepo, Roho (kidini)
 
nini asili na maana ya neno "afande"

Afande (title of rank) Ni neno linalotokana na Lugha ya Kituruki (Turkish), Kiarabu (Afandī أفند&#1610😉 au Kiajemi آفندی effendi.

(efendi hutumiwa na askari na polisi au maafisa wenye vyeo vya juu serikalini na haswa likitumika sana enzi ya utawala (Dola) y/wa Ottoman Empire)
 
hivi hayakuwepo maneno mengine mpaka yatumike haya;
kibwebwezo=computer
kibaobonye=mouse
toweo=toilet paper
 
<font color="#000080"><font size="3"><b>Noma:</b></font></font><b><font size="1"> (Ni neno la kiswahili) </font></b>Uzuizi, Uzuivu, Upinzani, Pingamizi, Mkingamo, Mkinga, Mgogoro, Uzuio, Masumbuo, Sumbuo, uzuwiaji, Uzuiaji, Masumbulizi, Kipingamizi, Masumbufo, Makinzano, Mfungizo, Kizuio, Kizuizi, Kikwazo, Masubuko.<br />
<br />
<font size="3"><font color="#0000ff"><b>Ghost:</b></font></font> Mzimu, Mzuka, Zuka, Zimwi, Njozi, Kizuka, Kivuli, Masuka, Pepo, Roho (kidini)
<br />
<br />
kwel&#305; kab&#305;sa s&#305;ju&#305; hao mara&#305;a wamecheka n&#305;n&#305;?
 
hivi hayakuwepo maneno mengine mpaka yatumike haya;
kibwebwezo=computer
kibaobonye=mouse
toweo=toilet paper
Kwa vile haya maneno yalianza na ki-bwebwezo, baobonye; nilitarajia na linalofuata lianzie hivyo hivyo, yaani ki-toweo=toilet paper. (lolz!!)
Napendekeza "pauro llitwe pauro"; kwa hiyo "toilet paper=karatasi ya chooni".
 
Nadhani neno Kisetiri lilifaa sana kwa toiletpaper
 
Noma,nishai,au soo, nikufanya tendo la aibu...ila anayetenda haoni "noma" (aibu) bali anayemwangalia ndo anamsaidia kuona "noma"(aibu) kwa mfano, mimi nimeamua kukojoa stand ya daladala,palipo na wa2 kibao, nani mwenye "noma"/aibu kati yangu na nyie mnoniangalia? Nyie ndo mnaNOMA..kwa sababu mi nimeona poa tu nikakojoa. Kwa kuwa nyie mna "noma"/aibu basi mnanisaidia kuona noma. Lakini mi cma noma
 
Noma: (Ni neno la kiswahili) Uzuizi, Uzuivu, Upinzani, Pingamizi, Mkingamo, Mkinga, Mgogoro, Uzuio, Masumbuo, Sumbuo, uzuwiaji, Uzuiaji, Masumbulizi, Kipingamizi, Masumbufo, Makinzano, Mfungizo, Kizuio, Kizuizi, Kikwazo, Masubuko.

Ghost: Mzimu, Mzuka, Zuka, Zimwi, Njozi, Kizuka, Kivuli, Masuka, Pepo, Roho (kidini)

hapo nlipopigia mstari..kwa kiswahili cha kwetu..kizuka ni mwanamke aliyefiliwa na mumewe na wala si mzimu kwa maana ya ghost kwa kizungu.
 
Back
Top Bottom