1. Ni kawaida wenye dhambi mkiambiwa muache dhambi mnakimbilia kusema mnahukumiwa.
2. Mnakimbilia kusema hakuna mkalifu, Biblia hiyo hiyo inasema 'Watakatifu waliopo duniani, ndio nnaopendezwa nao'.
3. Kama kuambiwa uache dhambi kisa unaona kila mru ni mdhambi unajidanganya na wahubiri wa injili waliofanya mpaka leo tumjue Kristo walifanya kazi bure, wale walikuwa ni watakatifu na dhambi haikuonekana kwao.
4. Usipendeke kutumia maandiko na kuyafafanua kwa utashi wako.
Mkuu kwa taarifa yako mimi nimeokoka nampenda Bwana Yesu sana.Hata mimi nilikuwa na mawazo kama yako katika uchanga wangu wa kiroho,ila Mungu alinionya.Aliniambia hivi kama wewe huna dhambi,mimi kama dhabihu hunihusu,na nilikufa bure Msalabani.Alinikumbusha na kuniambia unahesabiwa haki bure,ndio maana Mungu akikuangalia hakuoni wewe,anamuona Yesu badala yako.Alinielekeza nisome Warumi 7:15-25
Inasema,
"15 Maana sijui nifanyalo, kwa sababu lile nilipendalo, silitendi; bali lile nilichukialo ndilo ninalolitenda.
Warumi 7:15
16 Lakini kama nikilitenda lile nisilolipenda, naikiri ile sheria ya kuwa ni njema.
Warumi 7:16
17 Basi sasa si mimi nafsi yangu ninayetenda hilo, bali ni ile dhambi ikaayo ndani yangu
Warumi 7:17
18 Kwa maana najua ya kuwa ndani yangu, yaani, ndani ya mwili wangu, halikai neno jema; kwa kuwa kutaka nataka, bali kutenda lililo jema sipati.
Warumi 7:18
19 Kwa maana lile jema nilipendalo, silitendi; bali lile baya nisilolipenda ndilo nilitendalo.
Warumi 7:19
20 Basi kama lile nisilolipenda ndilo nilitendalo, si mimi nafsi yangu nilitendaye, bali ni ile dhambi ikaayo ndani yangu.
Warumi 7:20
21 Basi nimeona sheria hii, ya kuwa kwangu mimi nitakaye kutenda lililo jema, lipo lililo baya.
Warumi 7:21
22 Kwa maana naifurahia sheria ya Mungu kwa utu wa ndani,
Warumi 7:22
23 lakini katika viungo vyangu naona sheria iliyo mbali, inapiga vita na ile sheria ya akili zangu, na kunifanya mateka ya ile sheria ya dhambi iliyo katika viungo vyangu.
Warumi 7:23
24 Ole wangu, maskini mimi! Ni nani atakayeniokoa na mwili huu wa mauti?
Warumi 7:24
25 Namshukuru Mungu, kwa Yesu Kristo Bwana wetu. Basi, kama ni hivyo, mimi mwenyewe kwa akili zangu naitumikia sheria ya Mungu, bali kwa mwili wangu sheria ya dhambi.
Warumi 7:25"
Mkuu hii ndio hali ya mwanafunzi wa Bwana Yesu was kweli,na kama wewe contradiction hiyo huioni,basi wewe sio mwanafunzi wa kweli Bwana Yesu,unajidanganya.Mtume Paulo aliiona contradiction hiyo katika maisha yake,sasa hatukuelewi wewe mwenzetu.
Mkuu ukweli unabaki kwamba kama wewe humkosei Mungu,basi Bwana Yesu hakuhusu.Kumbuka kwamba sisi ni Wana wa Mungu,kwa hiyo kama Wana tutamkosea Baba Yetu,yaani Mungu,tunamkosjjambo la kufanya ni kurudi Kwake kwa toba,na Yeye kama Baba yupo tayari kutusamehe.