Maneno ya Rais Samia, yamenifanya nitafakari sana hekima yake kuu

Maneno ya Rais Samia, yamenifanya nitafakari sana hekima yake kuu

Abuka

JF-Expert Member
Joined
Sep 17, 2013
Posts
248
Reaction score
242
Kwa masaa kadhaa nimetafakari uwezo mkubwa na busara alizonazo Mama yetu, Rais wetu, Mama wa Vitendo, Mhe Samia Suluhu Hassan, Rais wa Tanzania alipokuwa akiwaapisha viongozi mbalimbali leo.

Rais Samia ametumia miezi 6 kuwasoma viongozi wasaidizi wake, miezi 6 Amiri Jeshi Mkuu mwenye mamlaka kamili hajatumia nguvu bali hekima kujua aina ya viongozi wanaomsaidia katika majukumu.

Yaani ni kama kuchezea Sharubu za Simba akiwa amekaa tu anakuangalia bila kukufanya kitu, hii imetokea Tanzania ni nadra sana kupata viongozi wenye utulivu namna hii.

Hiyo ni busara ya viwango vya juu sana, tunajua watu wakishapata dola wanatumia nguvu badala ya akili, wengi wanajikuta wamekurupuka au wameingizwa chaka. Hekima ya aina hii inatoka kwa Mungu pekee.

Muda wa majaribio umekwisha, sasa Kazi imeanza. Baragumu limelia ni muda wa kuzinduka. Rais Samia ametangaza rasmi kwa wateule wote kwamba tunaenda pamoja kwa wananchi, ni mwendo wa kuwahudumia kwa vitendo vikali badala ya maneno.

Wale waliolala usingizi, chonde chonde muamke sasa, Mama amesema vitendo vikali ni zoezi endelevu.

Hekima aliyokuwa nayo Mfalme Suleiman hakika hata leo inaishi.

Watanzania tujifunze kupitia tunu tulizopewa kama Rais Samia Suluhu Hassan.

Mungu aendelee kukulinda, tunakupenda Rais wetu.

#TwendePamoja na Rais Samia
 
Kisha atulie Tena awaze na kuwazua la Mbowe linamjenga au linambomoa? Kisha akimaliza atatuambia!
 
IMG-20210913-WA0016.jpg
 
Umetumwa kuandika haya? Mwenye akili timamu angetafakari kidogo juu zaidi ya haya.
 
Mama Rais kasema atafoka kwa kalamu sio mdomo. Kufoka ni kufoka tu iwe kwa mdomo ama kalamu mwisho wa siku titajua tu.
#tag stick and carrote.
 
uongozi sio kuongea huku umekunja sura na kushupaza mishipa ya shingo huku umechongoa kidevu na komwe.....siku hizi hatufokean wala hatutmbei na vitambaa kujikinga na mate.
Kabisa mkuu!

Siku hizi tunapigwa huku tunageiwa na soda.

Hata magaidi yanakamatwa kimya kimya na sasa yako ukonga pale
 
Mwenyewe alituambia macho yake na sauti yake ndio silaha yake, nashangaa leo anatuambia kalamu nyekundu ndio silaha yake.
 
Huyu Rais anafanya kazi yake vizuri tu hadi sasa hakuna tatizo lolote zaidi ya utulivu na amani kwenye mioyo ya watu hata kama mtu huna kitu lakini unapambana bila kutukanwa wala kukashifiwa tofauti na awamu iliyopita watu waliolalamikia hali ngumu waliishia kubezwa na kutukanwa tu eti wamezoea dili.

Wasaidizi wa rais wengi walikuwa wakijinufaisha binafsi na kutisha na kuonea wengine mara waweke watu ndani, mara wachalaze viboko kwa kisingizio cha kufundisha uzalendo basi ili mradi kila mmoja alitaka kuonesha umwamba wake kumfurahisha mfalme.
 
Mwambie bila utawala bora wa sheria na kuheshimu haki za binadamu ni kazi bure. Kazi kubwa ya rais ni kuwainganisha watanzania na si kuwaumganisha wana CCM.

Vyama hivi vya kisiasa vipo kwa mujibu kisheria na katiba ya nchi , leo kavigeuza kuwa ni vya ugaidi...vijana wanafanya makongamano ya kisiasa tena ya ndani anataka kuwavunja miguu - what a shame. Mama gani ananataka kuwavunja watoto wake miguu kisa tu hawaafikiani na mawazo yake.
 
Mwenyewe alituambia macho yake na sauti yake ndio silaha yake, nashangaa leo anatuambia kalamu nyekundu ndio silaha yake.
Slow slow alishasema madaraka yakishatekwa unakuwa kama mwanasesere. Yaani utaongea au kuyatenda yale wanayotaka wao. Yaani wale waliokuteka.
 
Kwa masaa kadhaa nimetafakari uwezo mkubwa na busara alizonazo Mama yetu, Rais wetu, Mama wa Vitendo, Mhe Samia Suluhu Hassan, Rais wa Tanzania alipokuwa akiwaapisha viongozi mbalimbali leo...
Sifa kubwa ya kiongozi, katika nyanja yoyote ya maisha (nyumbani, ofisini, katika jamii, mahusiano, nk) ni kusimamia maamuzi (kuishi katika kauli).

Rais SSH, kama mama, itakuwa maajabu akiongoza kwa jinsi ya baba. Lakini, aliyoyasema leo yatakuwa na maana akiyaishi, kwa sababu wanaofanya kazi kwa niaba yake (viongozi) ni watu wa hulka na tabia tofauti.

Kwa kauli anayopenda kuirudirudia kuwa yeye ni Rais wa jinsi ya kike, hakika yajayo YANAFIKIRISHA
 
Back
Top Bottom