Maneno yaliyoandikwa kwenye geti la kuingia Chuo Kikuu cha Cape Town, yana funzo kubwa!

Word...!?
 
Code:
Kwenye geti la chuo kikuu cha Cape Town nchini Afrika kusini kuna maandishi yasemayo;

 "Ukitaka kuangamiza taifa lolote duniani huhitaji kutumia silaha za nyuklia wala mabomu ya atomic. Njia nzuri ya kuangamiza taifa ni kuharibu mfumo wa elimu. Ruhusu "mbumbumbu" waonekane wamefaulu na wasonge mbele.

Matokeo yake yatajionesha baada ya muda, "mbumbumbu" hao wakishahitimu. Wagonjwa watafia mikononi mwa madaktari, majengo yataanguka mikononi mwa wahandisi, pesa zitapotelea mikononi mwa wachumi, utu utapotea mikononi mwa viongozi wa dini, na haki itapotelea mikononi mwa mahakimu. Kuchezea elimu ni kuangamiza taifa"

#nguzabullet%
 
Ni kweli.
Tukatae umbumbu
Tukatae uchawa
Tukatae Uozo 2025
 
Sasa ukitaka kujua nchi iliyokwisha angamizwa na kukosa elimu ni pale hoja ya umuhimu wa elimu haipati mchango kabisa kutoka kwa waliopata elimu lakini hoja za uchawa, hoja za kubeti ndizo zinapata michango lukuki. Kamanda ukitaka kupata michango humu wewe anzisha hoja za kishenzi , mapenzi, kuachana, kucheat, kubet, ligi ya budesliga, ligi ya ulaya, simba na yanga. Lakini ukiweka mambo ya critical thinking, mambo ya kufikilisha utaambulia wachangiaji wachache kama sisi ambao hatujaenda shule,
 
Elimu ambayo ni bora ndo silaha sio hii mliosoma hapa Tz

Nyie Tz hampewi Elimu Ila mnakaririshwa mambo tu ambayo yanwafanya kuwa watu ambao hamna impact yoyote .

Mimi maarifa yangu mengi 90% nimepata baada ya kuwa msomaji wa vitabu vya kiingereza .
 
ni kwasababu wengi ni mbumbumbu na elimu za kanjanja na kumpa uchi mwalimu,
Matokeo yake taifa linaongozwa na wapumbavu wasiojua nchi na wananchi wanahitaji nini.

Na hao mbumbumbu kila wakipata nafasi wanawaza mbinu za kuiba kodi za wananchi wakiamini ni haki yao.

Tena kuna kiziwi anawaambia wale kwa urefu wa kamba zao.

Nchi inakera hadi unatamani kulia.
 
Afu kweli, ila lands kupitia hoja hoi wapo watakaobadili mtazamo naamini wanaona hili ila ni jeuri, kiburi na dharau zao tu
 
Sasa hapo ndipo umeniacha hoi, kuna wanazuoni walikuwa wakisisitiza ni wakati sasa masomo yooote kuanzia primary mpaka secondari yafundishwe kwa kiswahili tena wakapata mashabiki lukuki humuhumu jamii forums. Nikajiuliza hivi tuko seriou
 
Ndiyo yanayotukuta sasa
 
Haswaa.
 
Y
Siasa katika elimu ni mbaya sana,nimeshuhudia watu wajinga sana wakiwa vyuoni hadi nikaanza kujiuliza kama walifikaje vyuoni,ni wajinga ajabu,chakushangaza wanakariri nakufaulu mitihani na mwishowe kusubiri ajira waende makazini.
Yaani na mimi nilipataga nafasi ya kufundisha chuo kikuu kikubwa sana cha afya nchini miaka fulani, ilibidi niwaulize hivi nyie ndio mabest students wa PCB nchini wenye ma-division one ya 7-10 kwani ndio ilikuwa criteria ya selection kwa wale wanafunzi, pathetic.

Lakini nilichokuja kugundua shule nyingi wanawashindilia watoto maswali na majibu, yaani mtoto mpaka anakuwa amekalili sana kufikia uwezo wa kufanya hesabu fulani kichwani kwa kukalili tu . Ni hakuna cha jumapili au jumamosi ni kuingia darasani asubuhi mpaka usiku wa manane. Huyu mtoto anarudia ma-past papers na kufundishwa namna ya kujibu scernario mbalimbali za maswali na ndio style ya ufundishaji wa walimu hata kabla ya kipindi cha mitiani.

Sasa ishu inakuja university ni lecturer/professor anakuja,, anawapatia refference na kuwapitisha kwenye core concepts au frameworks ya issues, then wanafunzi wanatakiwa waende wakachimbe kivyao. Kwa bahati nzuri nilikuwa nawaandalia notice nzuri sana kwenye power point ila niliwapa angalizo kuanzia siku ya kwanza kwamba hata ukikalili line by line kinachotakiwa ni kuelewa mada. Maswali yangu yatakuwa yanahusu application of the concept kwenye reali life scernarios au ni kwa jinsi gani unaweza kutumia concepts/constructs/principles/ modals/theories etc kutengeneza strategies na activities za miradi au kutengeneza evaluation approaches etc.

Sasa semister ya kwanza kilikuwa kilio ni baadae tu yaani semister za mwisho ndipo walipoelewa nini maana ya kumuelewa mwalimu. Mpaka leo nikikutana nao wananishukuru sana kwani zile concept ndizo wanazitumia kama ma-coordinators wa afya wa mikoa, wilaya au waganga wakuu wa wilaya. Kwa hiyo sio suala la ufundishaji tu lina shida kuanzia msingi mpaka chuo kikuu pia tuna tatizo namna tunavyowapima knowledge ,skills aand competence.
 
Umenena vema kabisa.
 
True na ndicho kilichopo hapa kwetu Tanzania hivi sasa. Viongozi wetu karibia ya wote ni wa aina hiyo, mambumbumbu na ndiyo maana hawaelewi nini wanafanya, wanafikiria kuiba tu kila kukicha na kumpongeza Mama kwa kuboronga ili wao waendelee kuiba huku wakimcheka.
 
Dr. Mwigulu Nchemba Na PhD yake ya kimagumashi
 
Hiyo mbona ni tafsiri yako, ungeweka maneno halisi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…