Chikumba one
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 1,009
- 1,642
Umenifanya nicheke! Post yako ni namba 8 katika kuchangia! Yaani hupishani na mtu ambaye kakutana na mwenzie barabarani halafu anamlalamikia mwenzie kuwa mtembezi!Huyu binti anawaweka vijana bize ktk mitandao ya kijamii wanashindwa hata kufanya kazi na ninachosikitika hata magazeti yetu nayo yanamchukulia kama chanzo cha habari. Asilimia kubwa wanaomfuatilia huyu binti wengi wao wavivu wa kufikiri, hawapendi kujishughulisha kutwa kusubiri leo atapost nini,wengi wao ni low IQ. Haiwezakani kila kitu anajua yy siasa, uchumi mpaka maisha binafsi ya familia za watu yaani kwa kifupi chuki zimemjaa moyoni mpaka mungu anashindwa kumbariki na ashukuru ameolewa na mzungu lkn kama angeolewa na mbongo sasa angekuwa tayari kilema, kwa kauli zake mbovu. Ila ninachosikitika zaidi mdogo wangu ni mmoja wa wafuasi wake, yaani amekuwa mvivu, mmbeya kwa kifupi hana mda wa kuyatafakari maisha yake, yy kila sawa na simu mpaka najuta kumnunulia simu, kila mara yupo instagram kwa huyo mange, sasa sijui labda anatoaga ela au huo uzushi wake ndio anaupenda.Nitasikitika zaidi kama Kuna watoto wa kiume nao wanamfuatilia huyu binti, basi nitakuwa na wasi wasi na ulijali wao.
Wewe usingekuwa unapoteza muda wako mwingi kwenye mitandao ungekuwa namba 8 katika kuchangia hapa?
Suala la kupoteza muda hapa jukwaani halina msingi wowote... Usiwafanye Vijana wenzio hawana akili bali wewe unazo! Hakuna tofauti yoyote kati yako na hao Vijana!
Wewe unawezaje kuja jf huku unafanya kazi zako? Je, wenzio hawawezi? Unaweza kukuta mashabiki wa Mange wanakuzidi kipato maradufu! Wengine wana kazi za maana kuliko wewe...usiongozwe na hisia katika kuwanyooshea wengine kidole!
Nachokushauri ni kuacha kujiona una IQ ya juu wakati huna uwezo hata wa kujua tofauti yako na unaowashutumu!
Zingatia mantiki ya hoja wanazotoa, na sio muda wanaoutumia kutoa hizo hoja!