Mangi Mkuu Thomas Marealle katika nyaraka za Sykes

Ingependeza sana kama ungeandika “History of Zanzibar before 1800” kama itawezekana lakini.
 
Ingependeza sana kama ungeandika “History of Zanzibar before 1800” kama itawezekana lakini.
Sheriff...
Historia hiyo ishaandikwa sana.
Prof. Abdul Sheriff amefanyakazi kubwa sana katika historia hiyo.

Lakini mimi nnilikuwa msaidizi wa Dr. Harith Ghassany wakati anatafiti kitabu chake, ''Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru.''

Naamini unakijua kitabu hiki kuhusu mapinduzi ya Zanzibar ya 1964.
 
huyu mzee Muhamedi Saidi ni mtu makini ambaye tutakuja kujuta kitu kimoja kwamba hatujathamini kazi yake ya kutupatia historia..... Sema tu udini huhusishwa sana kwenye mada zake.
 
huyu mzee Muhamedi Saidi ni mtu makini ambaye tutakuja kujuta kitu kimoja kwamba hatujathamini kazi yake ya kutupatia historia..... Sema tu udini huhusishwa sana kwenye mada zake.
Njemba,
Utasemaje ikiwa nitakuambia kuwa walioifuta na kuivuruga historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika walifanya hivyo kwa kusukumwa na udini wao?

Hawakutaka kuona jinsi Uislam ndani ya ukoloni ulivyotumika kuleta umoja wa kitaifa kwani hili lingeunyanyua Uislam juu sana.

Hii ndiyo sababu leo nakufunzeni upya historia ya TANU.
 
Father sina nia na wala siwezi kukujibu mtu mzima kama wewe na ninayesoma na kujifunza mambo mengi kutoka kwako..... nasoma sana maandishi yako na nakuheshimu na wewe hujui tu kwamba unasaidia sana sisi tusiojua mambo tujue kupitia uandishi wako wewe....kuna mengi unapaswa kutufundisha zaidi ya hilo..... UKABILA NA UDINI NI MAMBO NINAYOYACHUKIA SANA.
 
Njemba,
Basi mimi najua mengi sana katika dhulma walizofanyiwa Waislam wa nchi hii kiasi naweza kusimama na yeyote kwa ushahidi.

Suala la udini umelileta wewe na mimi nikawa sina khiyari ila kukueleza ukweli.

Waislam tungekuwa tuna udini Nyerere asingefika hapo alipofika na nchi hii isingekuwa hivi unavyoiona leo ilivyo.
 
Sasa Mkuu Pascall naona kama nawe pia unaungana na Mzee Said kutuchanganyia mambo, hizo mambo unayoyataja kama 'hearsay' kwa nini msiachane nayo tu?
 
Sasa Mkuu Pascall naona kama nawe pia unaungana na Mzee Said kutuchanganyia mambo, hizo mambo unayoyataja kama 'hearsay' kwa nini msiachane nayo tu?
Mkuu May Day, kwa vile kuna kila dalili ya tuhuma hizo kuwa ni kweli, then kunyamaza hakusaidii kutaendelea kufanya makabila fulani kuwa sidelined kwenye kugombea urais.
P
 
Mkuu May Day, kwa vile kuna kila dalili ya tuhuma hizo kuwa ni kweli, then kunyamaza hakusaidii kutaendelea kufanya makabila fulani kuwa sidelined kwenye kugombea urais.
P
Nakuelewa ila mambo kama haya ndio yaliyopelekea Wahenga kusema "yaliyopita si ndwele..."

Na vipi kuhusu nafasi ya Uwaziri Mkuu, maana kuna Mzee Msuya, au hii iliwalenga Wachaga tu?

Kiufupi mimi siuoni huo muelekeo wa kikabila kabisa, nafasi yenyewe ya uraisi ina upana gani wa accomodate kila kabila kwa nchi hii? ndio kwanza tupo na raisi wa tano.
 
Kuona sidelining, na marginalization ya makabila fulani fulani ni mpaka uvae miwani ya ukabila kuyaona hayo.
Its true tuna makabila mengi na rais ni mmoja tuu, haiwezekani kila kabila likatoa rais lakini pia it's not fair kwa makabila fulani kunyooshewa vidole kuwa hawatakiwi kutoa rais. Nb Wapare sio Wachagga japo wanapatikana Mkoa wa Kilimanjaro. Kama ilivyo Mwanza ni kwa Wasukuma, Wakerewe wako Mwanza na sio Wasukuma.
P
 

wewe pia unaleta maurongo. hebu tuthibitishie madai yako kuhusu Mangi Marealle. Na Nyerere angeweza kujiapiza hivyo unavyosema kama tayari angekuwa ni Raisi wa Tanganyika, na siyo wakati anapigania uhuru wa Tanganyika. Unadai Mwalimu hakuwataka watu wa North Province, sasa mbona ktk nyakati mbalimbali aliweza kuwapa majukumu mazito ya kuitetea nchi yetu? Je, unafahamu kwamba Idi Amini alipotuvamia na kukalia ardhi yetu Kamanda[ T N Kiwelu ] wa Jwtz mzaliwa wa North Province ndiye aliyekabidhiwa na Mwalimu Nyerere jukumu la kupiganisha vita vya kukomboa ardhi ya Tanzania? Kama Mwalimu Nyerere alikuwa akiona wazawa wa North Province hawafai kwanini aliwakabidhi majukumu mazito kama huyo niliyekutajia hapo juu? Mwalimu amewahi kuwa na Mpambe mzaliwa wa North Province, leo mnasema alikuwa hawataki?
 
Mkuu umetisha sana😂😂😂
Mkuu umetisha sana.
Umejiongeza.
Umekwepa kiutu uzima.
Vinginevyo ungekula 'vitasa'
vya haja kutoka kwa Mzee Mohamed Said
 
Anatamani sana kukukwamisha
Lakini masikini hana chochote
Katika historia ya nchi.

Tunasubiri kile kitabu
chao na wenzie walichoahidi
kuandika😂
Dos Santos,
Kumbe nawe umeliona hilo.
Kaibadili mada kabisa.
 
Anatamani sana kukukwamisha
Lakini masikini hana chochote
Katika historia ya nchi.

Tunasubiri kile kitabu
chao na wenzie walichoahidi
kuandika[emoji23]
Do Santos,
Wanaweza hakika wakajaribu kuandika historia ya TANU kama ilivyokuwa katika miji yao lakini hawawezi kuja na historia mfano wa historia ya Abdul Sykes.

Sababu ni kuwa Abdul Sykes ni mmoja na yale aliyofanya katika maisha yake ndiyo yaliyompambanua ndani ya TAA na ndani ya TANU.

Abdul kampokea Nyerere Dar es Salaam 1952 akasimama na Nyerere kwenye uchaguzi wa rais wa TAA 1953 na Nyerere "akashinda," uchaguzi ule.

Vipi Nyerere aliweza kushinda ni historia tosha ya kusisimua.

Vipi historia hii kwa miaka yote haikuwa inafahamika na Nyerere hakupata kuieleza popote ni kitu cha kumstaajabisha mtafiti yeyote yule.

Yako mengi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…