Manji aanza mkakati wa ujenzi wa uwanja yanga

saaa safi sna kakak nimekupenda ukweli uliotwambia hasa hii timu ya maharage ndo imejaza washabiki
mimi mwenyewe simba damu lakini yule alshhabab hana lolote analojua, kwenye siasa anapanda na bastola utafikiri ameyaona majeshi ya kenya.yaani vululu mimi nilimwona mwehu pale aliposema ataitoa timu kwenye ligi mashabiki wangemkeketa yey na familia yake chezea yanga na simba eeh.
 

mi alipo kula rambirambi ya mafisango ndo nilichoka afu hakuna mtu wa kumuliza, afu kwenye ishu za yanga mashabiki wa simba ndio wanajifanya waongeaji, wakati alshababu kawashika wakashikika
 
manji hana iyo pesa............gharama za huo uwanja zitamgharimu hadi kijiko cha jikoni kwake............anapesa lakini sio wa kujenga uwanja wenye hadhi kama iyo hapo pichani
 
Ni hatari kwa klabu kubwa kutegemea ufadhili wa mtu mmoja, labda angekuwa ni mmiliki. Hivi mapenzi gani haya kwa timu? Mwisho wa siku utasikia fedha iliyojenga uwanja ameikopesha Yanga, na utakuwa mikononi mwake mpaka deni liishe. Vibabu, I mean, wazee, klabu ndio inabinafsishwa hivyo!!!!
 

soka biashara mjomba hiyo ndo tunaitaka, sio timu kila siku kuendeshwa kienyeji enyeji hata manchester yenyewe inamilikiwa
 
hii thread ipo humu ndani ,ni copy and past...nilidhani tayari ni official report
 
Waswahili kwa kupenda bure mi sijui wakoje...sasa timu kama Yanga hivi kweli ya kujengewa uwanja na mtu kweli?!!
 
Waswahili kwa kupenda bure mi sijui wakoje...sasa timu kama Yanga hivi kweli ya kujengewa uwanja na mtu kweli?!!
hata mimi nashangaa.mbona sisi simba tumejenga uawanja wetu wenyewe na unakaribia kuisha,tumebakiza kuweka vitasa vya milango tu.
 
Picha za boda la Kaunda zimenirudisha nyuma saaaana tu.
 

No wonder hata mawazo yako yamekaa ki'mfu-mfu,unataka kujua Wanachama hai tutachangia shing'api subiri mchakato uanze na hisa zianze kuuzwa ndo utamjua Anselm ni Mbia wa aina gani kwa team yake aipendayo,hapa nilipo hata siku 1 sikumbushwi ada yangu ya uanachama,always huwa na'clear ada yangu ya mwaka mzima miezi mi'3 kabla haijamalizika,ushirikishwaji mbaya ulitufanya tukose kumsajili Ngassa but I was ready to pay the difference iliyokuwa ina persist kati ya dau la Simba na lile la Yanga(Million 5 kitu gani),nataka kukuambia usione tunaandika sana hapa kuhusu Yanga wengine hii team tunaipenda kufa,get it right!
 
wabongo tunapenda vibaya hadi hatuoni! Yanga kujenga uwanja inawezekana sana ila siyo kwa stail hii ya kuzogoa kwenye media, alafu mwandishi mwenyewe zubeiry ambaye yanga ikifungwa anaweza hata kuzimia! Ingia kwenye blog yake ndo utamuelewa vizur. Kabla ya kuandika habari hii, kuna habari aliandika kuhusu uchakavu wa samani katika jengo la yanga na kufananisha vitanda vyake kama vya gest za uwanja wa fisi na anashangazwa na uwezo wa kifedha walionao viongozi huku hali jengoni ni mbaya, akafikia kumtaja hadi katabaro kuwa peke yake alikuwa na uwezo wa kushughulikia samani mara moja! Kama samani ni hivyo je uwanja? Zubeiry alichofanya ni kumuuliza manji kuhusu uwanja naye akajibu atajenga, na naamini mwenyekiti yeyote angetoa jibu kama lake.kwa kifupi habari zake mh...! Kuna kipindi aliandika kuwa ngasa amesajili yanga kabla ya simba na alimnukuu clement sanga bila kujua kuwa anamchongea mzee wa watu!(tembelea blog yake ili uchanganyikiwe vizuri). Viongozi wote(simba & yanga) ngoma droo, wanachofanya kuwachezea wanachama kama midoli tu kwakuwa wanajua shida yetu ni moja tu na roho zetu zitapona "ni yanga kumfunga simba au simba kumfunga yanga!" tuzinduke tufanye mapinduzi ya kweli. Moise Katumbi bongo bado hajazaliwa, wanachofanya hao ni marudio ya yale yaliyofanywa na kina marehem Gulamali(roho yake ipumzike kwa amani), Murtaza Dewj na Mohamed Viran Babu "Vimto" kwa yanga na Dewj(Azim, Kasim na mohamed) F. Amijee n.k kwa simba.
 
Kelele tu.. yanga wana kaeneo kadogo tu pale pembeni! Kifupi pale hakuna nafasi ya kujenga uwanja mkubwa kiasi hicho! Watu 40-60,000 watapitia wapi? Watafikaje? Magari yatapaki wapi?
 
timu zote viongozi longolongo tu. Kweli simba inakosa pesa za kulipia uwanja!? Ingawa nawapongeza wanachama kwa kupitisha mchango kwenye mkutano mkuu, tofauti na wenzao ambao wanataka walipiwe hadi mchango wa kadi za uwanachama ndo waende mkutanoni! Hivi pesa za samata, ochan, mrwanda na henry joseph ambazo zingetosha hata kwa uwanja wa mazoezi zimeenda wapi?na fedha za rambirambi je? Na yanga nao wanafukuza kocha bila kutathmini hasara watakayopata! Haya milioni 200 hizooo mtakatifu wenu tomasi anaondoka nazo! Klabu inamradi gani wakupata pesa zote izo?(kuna taarifa kuwa wamekopa, tayari deni ilo!), huku papic naye huyooo kakinukisha! Bila kusahau Njoroge yuko kwenye foleni anasubiri kukinga chake! Alaf ujengwe uwanja! What a hell is this!? Klabu imekua kama muembe wa uwani kila mtu anajitingishia tu! Eti kisa yeye ni Baniani! Mbona kuna kipindi aliitelekeza timu ikawa ina haha hadi wachezaji wakatoroka hotelini Arusha sababu ya deni! Huyo ameingia klabuni kufidia hasara alizopata kipindi kileee...amkeniiii! Baada ya mechi na JKT kuna watu wa yanga waKaanza kumuimbia na wengine kutaka hadi kumbusu...!! Bahati nzur aliwahi kupanda gari( alafu kuna jamaa anasema eti yanga hakuna watindiga! Hawa tuwaiteje? Mapoyoyooo au michelee!!?) maskini ya Mungu bado wamelala!
 

Wewee Yanga hakuna Watindiga wewe,ulishawahi kuona Yanga imesajili kwa kuonyesha picha ya Mwenyekiti amemshika bega mchezaji tajwa msajiliwa halafu wakashangilia,umeshawahi kusikia katika mkutano wa Yanga taarifa ya mapato na matumizi ikasomwa kisanii na wana Yanga wakashangilia,umeshawahi kuona wana Yanga wamechangia rambirambi za mpendwa wao zikaliwa na Viongozi wao na wao wakakaa kimya,umeshawahi kuona Yanga imeuza wachezaji nje wana Yanga wasihoji fedha iliyopatikana imetumikaje badala yake wakazidi kukamuliwa kwa kuchangishwa kwenye mkutano mkuu....hivi unafahamu kuwa kupata taarifa ya mapato na matumizi hata kwa wewe mshabiki njaa wa huko madongo kuporomoka kwako unakoishi ni haki yako? halafu unajisifia kwa kuchangishwa,kama kuchangishwa pasipo kupata maelezo ya kina ya sababu za kuchangishwa au mapato yaliyopatika katika mwaka wa fedha uliotangulia yametumikaje ni ujanja basi mimi binafsi nitakuwa Mtindiga namba 1 kwani siwezi kukubali hata siku 1.
 
Nimependa kuonda juhudi za kiongozi Mkuu wa Young Africans Mwenyekiti Yusuph Manji anataka kufanya pale Jangwani lakini naungana na washabiki wenzangu wawe wa Simba au Yanga au mpenzi wa timu yoyote haya yasiwe maneno ya kujisifia tu kwani maneno yanayohusu Uwanja huo wa KAUNDA yamekuwa ni Hadithi za (Esopo ) inakera sana hata kama wanayanga hawana uwezo wa kujenga uwanja huo basi tupunguze tambo za uwanja huo kwani zimekuwa ni za muda mrefu sana Tangu enzi za Ramesh Patwa, Abbas Gulamali, na viongozi wengi waliofuatia hapo hahadi nyingi ya kujenga Uwanja huo zimebaki ni Hadithi tena magazetini.. hiyo ni kwa upande wa Yanga upande wa pili wa shilingi wenzetu tulisikia zimepungua shilingi milioni 90tu uwanja utakuwa tayali umepatikana ukweli unabaki pale viongozi wote wanababaisha lugha wanapokutana na wanachama wao,Rage umepata milioni 30m na kutapeliwa na Mbuyu Twite utakosa milioni 60m zilizobaki kutoka Bungeni na kwa washirika wenzako kujenga uwanja uliowahahidi ndani ya siku 100 sasa ni mwaka 2 hakuna kitu fixxxxxxxxxx tu
 
baada ya kushinda ndio mkakati unazungumziwa tushaanza na tv show toa maoni yako kwa maandeleo ya azam fc 123 - YouTube
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…