Wakati naweka hii habari hapa, watu waliibeza, nadhani JF tujifunze uvumilivu. Na tujue kuwa humu JF kuna watu wa kila aina na mara nyingi JF imekuwa ya kwanza
i stand to be corrected,ina maana birthday yake ndo tarehe aliyofariki Mwalimu?Niliambiwa kwamba amekwenda South Africa kwa matibabu, lakini katika system za Mwalimu Nyerere International Aiport, jina la Yusuf Mehboob Manji, aliyezaliwa Oktoba 14, 1975, mwenye pasi namba AB 052416 ya Tanzania, halijaonekana, labda kama kasafiri kwa ndege ya kukodi na pasi yake ya Marekani ama kimoja wapo. Patamu hapo.
Pia huyu jamaa ni mfisadi lakini Watanzania sijui tumeumbwa vipi hivyo viji centi anavyotoa yanga vinatufanya tumuone kama Mungu vile na kusahau kuwa ni sawa na vibaka wanao iba cheni au simu na kuchomwa moto na raia wenye hasira kali.
....Kwani jamaa mnazi wa Simba??Mkuu fikiria angekuwa anaifadhiri SIMBA ungesema hivyo?
Kunya anye KUKU akinya BATA kahalisha.
Mkuu Fidel80,Mkuu fikiria angekuwa anaifadhiri SIMBA ungesema hivyo?
Kunya anye KUKU akinya BATA kahalisha.
HASWA nimetonywa ilikuwa mtu wa mwanzo kuwekwa korokoroni.nimetonywa kisha paa majuuLabda ndo staili yake ya kukwepa Rungu la JK kwa mafisadi wa EPA. Au Rungu la EPA ndo limemchanganya hadi akabwia dozi kubwa ya ungwa.
HASWA nimetonywa ilikuwa mtu wa mwanzo kuwekwa korokoroni.nimetonywa kisha paa majuu
Mkuu fikiria angekuwa anaifadhiri SIMBA ungesema hivyo?
Kunya anye KUKU akinya BATA kahalisha.
Mkuu Fidel80,
Kwanza nirudie kuwapo mkono wa pongezi wana Yanga kwa ushindi wenu 'finyu' dhidi yetu.
Mimi ni shabiki mkubwa wa Simba (kama spika Sitta 🙂 ) lakini naomba kuna mambo wakuu tukubaliane kuwa si ya kukumbatia.
Ufadhili wa Manji kwa Yanga usiwazibe macho mkasahau kuwa jamaa huyu anaitumia Yanga kujitangaza! Jamaa huyu habari nyingi ninazopata juu yake huwa haziridhishi, mara anajidunga madawa, mara anachapisha note fake, n.k. Kwakuwa zinakuwa zinakosa proof japo ni fununu toka kwa watanzania wengi nachelea kuzithibitisha.
Kikwetu wanasema "lisemwalo lipo... kama halipo linakuja".
Nitaingia mtaani kusaka data zaidi nikizinyaka nitawapa facts zaidi na zaidi juu ya mfadhili wenu huyu.
Hapa nashindwa kuamini, bila shaka huku kuchanganyikiwa kuna harufu ya EPA! Kama ni madawa angechanganyikiwa siku nyingi,iweje zibaki siku 3 tu kurudisha pesa za EPA ndio achanganyikiwe?Watanzania wa sasa si wavivu kufikiri kama wao wafikirilivyo.
Date::10/29/2008
Manji wa Yanga sasa alazwa chumba uangalizi maalum hospitalini
Na Mwandishi Wetu
HALI ya mfadhili Mkuu wa Yanga, Yusuf Manji bado haijaimarika na sasa amepelekwa chumba cha wagonjwa mahututi, ICU, katika Hospitali ya Aga Khan jijini Dar es Salaam.
Habari ambazo Mwananchi imezipata jana jioni kutoka hospitalini hapo, zinasema kuwa hali yake ilibadilika ghafla jana mchana na uamuzi uliofikiwa na madaktari ni kumpeleka katika chumba cha uangalizi maalum.
“Manji hajarejea katika hali ya kawaida, amekuwa akizungumza maneno yasiyoeleweka, lakini inawezekana ni malaria kali iliyopanda kichwani…bado hali haijatengemaa, wasiwasi umekuwa mkubwa lakini tunaimani atapata nafuu,” kilisema chanzo cha habari.
Mwananchi iliwasiliana na Mwenyekiti wa Yanga, Iman Madega kutaka kufahamu hali ilivyo kwa mfadhili huyo, na kusema hali yake bado haijaimarika. Hata hivyo Madega hakutaka kuzungumza zaidi suala hilo.
“Nimepata taarifa kuwa hali yake bado haijatengemaa, nilikwenda hospitali lakini sikuweza kumuona na nilizungumza na msaidizi wake, Sabas Kiwango mambo ya Yanga na baadaye nikaondoka hospitali…kwa kweli siwezi kulisemea zaidi, lakini hali ndiyo hiyo,” alisema Madega.
Habari zaidi kutoka hospitalini hapo zinasema kuwa hakuna mtu yeyote anayeruhusiwa kumwangalia Manji isipokuwa watu wa karibu tu na tayari yuko katika chumba hicho cha wagonjwa mahututi.
Manji alipatwa na kilichoelezwa kuwa ni malaria kali siku moja baada ya timu yake kuichapa Simba bao 1-0, katika mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom, mchezo uliofanyika kwenye Uwanja Mkuu wa Tanzania. Baada ya kuugua na kuanguka ghafla, alikimbizwa Hospitali ya Aga Khan kwa matibabu.
Ilielezwa kuwa Manji alipatwa maradhi hayo juzi wakati akijitayarisha kwenda kazini majira ya saa tatu asubuhi lakini ghafla alianguka. “Unajua inawezekana ni furaha za ushindi na kuwa bize inawezekana kulimfanya apatwe na hali hiyo…inawezekana alikuwa na malaria ya muda mrefu na kutokana na kuwa bize na mchezo ndipo ikaibuka.
"Baada ya kufanyiwa vipimo Aga Khan aligundulika kuwa na malaria kali na uchovu, mwili ulikuwa umechoka kwa mawazo akapewa dawa na kumpumzika nyumbani, lakini baadaye majira ya saa 11 alfajiri akatoka nyumbani bila ya kueleweka akielekea maeneo ya Viwanja vya Gymkhana, lakini walinzi wake walimfuata na kumrudisha tena hospitali," alisema Madega alipozungumza na gazeti hili juzi.
Madega alisema hali ya mfadhili huyo ilikuwa inaendelea vizuri baada ya kuchomwa sindano ya kumtuliza lakini baadaye hali yake ilibadilika ghafla.
Juzi Madega aliwataka Wanayanga kutulia katika kipindi hiki ambacho mfadhili wao anasumbuliwa na maradhi na kumuombea aendelee vema na matibabu.
Hi ya kulazwa ICU nimeiona. lakini does this make us believe that he is that serious? au baada ya masaa kuwa machache. And also remember he is in Aga Khan Hosp. another indian Institution!
Mod, baada ya kuona hii sasa inanukia harufu ya EPA ama ufisadi mwingine, ingehamishiwa katika siasa ili watu wajadili zaidi
Mod, baada ya kuona hii sasa inanukia harufu ya EPA ama ufisadi mwingine, ingehamishiwa katika siasa ili watu wajadili zaidi
Manji ana hela za EPA na ndo kama mweka hazina wa CCM na anafanya biashara kwa niaba ya chama cha mafisadi(CCM)na kikwete alimwomba Manji aisadie yanga kwasababu Yanga ni ya CCM na ndio ya Serikali na pia Manji now anawajengea uwanja utaochukua watu kama 20,000 na hoteli ya 4 star,huu ni ufala wa hali ya juu kikwete anafanya maana itakuwa vp kama wapenzi wa simba wakiamua kukipigia kura chama kingine???na ndo mana ata TBL walidhamini both Simba na yanga koz walijua simba hawatakunywa bia zao!!!lakini kwasababu kikwete kazungukwa na washauri wabovu ili hawezi lijua ata kidogo!!kama mbwai ni mbwai basi mwambie Rostam nae aidhamini Simba mana yule ni mpenzi wa simba na ana hela za EPA...