Manji kuzikwa Marekani kumedhihirisha kiwango kikubwa cha ujinga. Tuna safari ndefu kama nchi katika katiba na elimu ya uraia

Manji kuzikwa Marekani kumedhihirisha kiwango kikubwa cha ujinga. Tuna safari ndefu kama nchi katika katiba na elimu ya uraia

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Nimeangalia comments za ukurasa mmojawapo wa mitando ya kijamii kuhusu Manji kuzikwa Florida Marekani nimeshangaa kuona kundi kubwa sana la raia Watanzania hawana elimu kabisa kuhusu vigezo vya kuwa raia wa nchi hii au kuna ubaguzi mkubwa sana kwa raia walio wengi.

Wengi katika ukurasa huo wameshangazwa sana na kuuliza maswali kwamba kumbe Manji hakuwa Mtanzania?! Yani tuna raia wengi wanaojua kwamba Mtanzania hawezi kuzikwa nje ya Tanzania akifariki! Kwamba kigezo kimojawapo cha kuthibitisha Utanzania wako ni kuzikiwa katika ardhi ya Tanzania!

Sasa kama mtu amefikia kumiliki smartphone na hajui hata vigezo vya uraia wa nchi yake hao wengine watakuwa anafahamu nini katika masuala ya haki za uraia na mambo mazito ya katiba kwa ujumla?!

Itoshe kusema tuna safari ndefu kama nchi kuhusu katiba na elimu ya uraia.
 
Nimeangalia comments za ukurasa mmojawapo wa mitando ya kijamii kuhusu Manji kuzikwa Florida Marekani nimeshangaa kuona kundi kubwa sana la raia Watanzania hawana elimu kabisa kuhusu vigezo vya kuwa raia wa nchi hii au kuna ubaguzi mkubwa sana kwa raia walio wengi.

Wengi katika ukurasa huo wameshangazwa sana na kuuliza maswali kwamba kumbe Manji hakuwa Mtanzania?! Yani tuna raia wengi wanaojua kwamba Mtanzania hawezi kuzikwa nje ya Tanzania akifariki! Kwamba kigezo kimojawapo cha kuthibitisha Utanzania wako ni kuzikiwa katika ardhi ya Tanzania!

Sasa kama mtu amefikia kumiliki smartphone na hajui hata vigezo vya uraia wa nchi yake hao wengine watakuwa anafahamu nini katika masuala ya haki za uraia na mambo mazito ya katiba kwa ujumla?!

Itoshe kusema tuna safari ndefu kama nchi kuhusu katiba na elimu ya uraia.
Ungetoa elimu kidogo kuhusu mazishi ya Yusuph Manji huko USA ili wengi wajifunze.
 
Wana hoja wahindi wengi sio wazalendo,wako huku kuchuma tu ila wana passport au nasaba ,mapenzi na nchi zingine,wahindi sio watu wa kuwaamini
Kwa sababu hata Tanzania sio nchi ya kuaminika mkuu, hata sisi ni vile tumezaliwa hapa na ni wazawa wa ngozi nyeusi, wengi tungeshatafuta namna ya kuishi na hata kuukana utaifa wetu.
 
Wana hoja wahindi wengi sio wazalendo,wako huku kuchuma tu ila wana passport au nasaba ,mapenzi na nchi zingine,wahindi sio watu wa kuwaamini
Kunaweza kuwa na ukweli katika hilo.Lakini,nimeona wengi wanaozikwa huko(nchi walizofarikia) huwa ni wa dini ya kiislamu.Nikaelezwa sababu mojawapo ni kwamba,kwa taratibu za dini ya kiislamu,mtu akifariki anatakiwa kuzikwa siku hiyohiyo(kuna muda mchache wa kukaa na maiti)bila kujali nchi yake ya kuzaliwa.Na ninaamini yawezekana kukawa na sababu zingine.
 
Wana hoja wahindi wengi sio wazalendo,wako huku kuchuma tu ila wana passport au nasaba ,mapenzi na nchi zingine,wahindi sio watu wa kuwaamini
Kwani kuwa na nasaba, mapenzi au mahaba na nchi nyingine kunaondoa vipi uraia wa mtu?? Yani Utanzania wa mtu unaondoka kivipi kwa yeye kuwa na mapenzi na Israel, Russia, Kenya au Marekani??
 
Hivi Tanzania kuna makaburi au madampo ya kutupia watu? Hayana usimamizi mzuri, watu wanazikwa zigzag, hayapaliliwi wala kusafishwa, i hope atatokea mtu na idea ya kununua ardhi, inakuwa chini ya Manispaa ila yeye anaendesha usimamizi na matunzo ya hilo eneo. Hata kama itagharimu milioni moja kuzika, lakini pawe safi miaka yote. Pawekwe maua na nyasi na wazikwe kwa mstari ulionyooka
 
Hivi Tanzania kuna makaburi au madampo ya kutupia watu? Hayana usimamizi mzuri, watu wanazikwa zigzag, hayapaliliwi wala kusafishwa, i hope atatokea mtu na idea ya kununua ardhi, inakuwa chini ya Manispaa ila yeye anaendesha usimamizi na matunzo ya hilo eneo. Hata kama itagharimu milioni moja kuzika, lakini pawe safi miaka yote. Pawekwe maua na nyasi na wazikwe kwa mstari ulionyooka
Kuna sehemu/mikoa/makabila wanajali na kusafisha vema makaburi ya wapendwa wao mara kwa mara.
 
Back
Top Bottom