Manji: Ujenzi uwanja wa mazoezi kuanza ndani ya siku 90 baada ya ridhaa ya wanachama

Akilimali sio msomi ila mjanja,yupo town kitambo. Yeye ndo almpinga Nchunga na kumshawishi manji. Sasa mzee ameona udikteta wa manji sasa anatumia mbinu zlezle kumnyoosha
 
Huwezi jua mkuu Gamaha lakini umenigusa sana katika hili.
Nimeona mtu mmoja kaandika comment hapa kuwa billion 60 kwa miaka 10 ni sawa na shillingi 600 million kwa mwaka. Kwa hesabu za haraka ni kuwa ukipangilia vizuri na kupata usimamizi wa kitaalamu katika uwanja wa Taifa mechi moja tu inaweza kuingiza kiwango cha chini millioni 800, au Kirumba, Mwanza wanaweza kuingiza million 450 walau. (Kwa uwanja wa taifa hebu hesabu viti 60,000 x kiingilio 15,000/= ni 900,000,000/-). Ikipangwa vizuri na kufanyika match promotion ikiwa ni pamoja na BAHATI NASIBU kwa kila ticket ina maana ticket zinaweza kuuzwa hata kwa wastani wa 25,000/- na kuisha ambapo inaweza kupatikana zaidi ya 1.5b kwa mechi moja tu. Hapo hakuna cha udhamini, hakuna vodacom, TBL, DTB bank nk. Na hapo hujaongelea michango ya wanachama wapatao sijui 4,000,000 wa klabu pamoja na 'well wishers'.
Huo ni mchanganuo wa mchezo mmoja tu hivyo timu ikiandaa successful matches walau moja kila mwezi inaweza kupata zaidi ya billion 10 kwa mwaka. Ikiamua kuajiri wataalamu wa kusimamia hivi vitu ambao ni professional (achana na wa sasa wenye upeo wa kuona siku moja tu mbele badala ya miaka 50 kama waliojenga klabu) wanaweza kulipwa sio zaidi ya billion 3 annually ili kusimamia billion 8 kitu ambacho ni sahihi!
Maelezo mengi lakini nikirudi hapo kwenye red ni wazi enzi klabu hizi zinajenga majengo waliofanya utafiti wa kila mtu 1 kati ya 4 naamini wakati huo wangepata mtu 1 kati ya 500,000 kulinganisha na matokeo ya sasa!
Huwa sitaki kujiaminisha eti 'tumelaaniwa' lakini matendo yetu yanatulamisha kwenda huko.
 
Mzee Akilimali yuko kitambo mjini na anaijua Yanga ndani nje, hivi mnaijua Pan African ilipotokea?? Kuna kitu kilikua kinaitwa " mgogoro wa Yanga", kilidumu kwa miaka kadhaa na alielianzisha alikua kanjibhai pia akiitwa Shiraz Sharriff, alitaka fanya hivi hivi kama Manji; Yanga sio timu ya kukodishwa ni timu inayoweza jiendesha bila Manji bali wanachama nchi nzima wakiamua kuuza na kununua hisa.. Manji mjanja na wajinga ndio waliwao.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…