Manyara: Basi la Shule lagongana na Lori la mizigo, Wanafunzi Watatu, dereva wafariki, watano mahututi

Manyara: Basi la Shule lagongana na Lori la mizigo, Wanafunzi Watatu, dereva wafariki, watano mahututi

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607

Mkuu wa Mkoa, Queen Sendinga amesema ajali iliyotokea jana Agosti 31, 2024 ikihusisha Costa iliyobeba Wanafunzi wa Shule ya Endasak Sekondari na Lori la mizigo lililokuwa linatokea Burundi, imepoteza Wanafunzi Watatu na dereva wa Costa huku majeruhi wakiwa 31

Amesema “Ajali imetokea eneo la Guardian, Halmashauri ya Babati, uchunguzi umeonesha kulikuwa na uzembe wa dereva wa Lori, amekimbia lakini ameacha vitambulisho vyake na vitu vingine, tumevitambua, Jeshi la Polisi na Vyombo vya Usalama vinaendelea kumtafuta.”

Ameongeza “Majeruhi wote wanatibiwa kwa gharama za Serikali, miili ya marehemu imehifadhiwa ikisubiri taratibu za familia na Serikali tutatoa ushirikiano wote watakapohifadhiwa
 
Elimu bora ya msingi kwa Watanzania NI muhimu sana ili kuepusha baadhi ya ujinga.

Askari polisi mabarabarani wajikite Sana kuangalia hali ya usalama na kuacha kuwaza madili tu muda wote na rushwa pia.

Serikali iboreshe mishahara ya Askari polisi angalau kima cha chini kiwe 700K angalau itawapunguzia umasikini na kuwafanya akili iwe kwenye kazi kidogo.

Serikali iitambue ajira ya udereva iwe rasmi sasa na madereva wawe na Elimu ya form four na mafunzo ya udereva kutoka taasisi zinazotambulika, walipwe mishahara na wawe na bima, NSSF kama wafanyakazi wengine.

Serikali iweke udhibiti kwa wafanyabiashara ya usafirishaji, sio lazima hiyo biashara ifanywe na kila mtu sasa, wengine wanaweza kufanya biashara nyingine ili kudhibiti magari mabovu barabarani huko.

Tanroad wawe makini na ubora wa Barabara ikiwa pamoja na kuacha kuzibaziba viraka hovyo na kuondoa smoothness ya Barabara, lakini pia wawe wanafanya patrol ya Barabara zao mara kwa mara kubaini maeneo mabovu na kuyadhibiti haraka.
Tuache kuwaza urahisi na kuwapa kazi za barabara wakandarasi Vimeo, tujikite kwenye ubora wa Barabara zinakazodumu miaka mingi na sio hizi tunazoziba viraka kila kukicha na mibonyeo kila mahala.

Mwisho kabisa, viongozi wa CCM na watumishi wa umma mjikite kutumikia wananchi na keto zao na sio kuwaza siasa za uchaguzi na kiutawala tu.

RIP watoto wa Mungu, mmekufa kwa uzembe na ujinga wasisi wazazi wenu.
 

Mkuu wa Mkoa, Queen Sendinga amesema ajali iliyotokea jana Agosti 31, 2024 ikihusisha Costa iliyobeba Wanafunzi wa Shule ya Endasak Sekondari na Lori la mizigo lililokuwa linatokea Burundi, imepoteza Wanafunzi Watatu na dereva wa Costa huku majeruhi wakiwa 31

Amesema “Ajali imetokea eneo la Guardian, Halmashauri ya Babati, uchunguzi umeonesha kulikuwa na uzembe wa dereva wa Lori, amekimbia lakini ameacha vitambulisho vyake na vitu vingine, tumevitambua, Jeshi la Polisi na Vyombo vya Usalama vinaendelea kumtafuta.”

Ameongeza “Majeruhi wote wanatibiwa kwa gharama za Serikali, miili ya marehemu imehifadhiwa ikisubiri taratibu za familia na Serikali tutatoa ushirikiano wote watakapohifadhiwa
Ccm kwa kafara hamjambo
 
Argument of the short-sighted mind person.

Kwani wakienda kwa miguu hawataweza kupata ajali wakiwa njiani? Hawataweza kupata ajali Kama vile za kugongwa na waendesha pikipiki (bodaboda) au gari?
Hahaha jamaa hapendi boarding school ndio msimamo wake. Sasa anajikuta ana dis kila kitu
 
Kupitia nukuu hiyo mkuu wa mkoa hafahamu kwamba polisi ni chombo cha usalama! Anasema dereva amekimbia ila akaacha vitambulisho vyake na kwamba polisi na vyombo vya usalama vinamtafuta. Huyo ni mkuu wa mkoa na anaitwa kiongozi wa watu wenye changamoto mbalimbali zinazohitaji utatuzi wa kiserikali.
 
Kupitia nukuu hiyo mkuu wa mkoa hafahamu kwamba polisi ni chombo cha usalama! Anasema dereva amekimbia ila akaacha vitambulisho vyake na kwamba polisi na vyombo vya usalama vinamtafuta. Huyo ni mkuu wa mkoa na anaitwa kiongozi wa watu wenye changamoto mbalimbali zinazohitaji utatuzi wa kiserikali.
Mkuu,maisha sio magumu hivyo.
 
Poleni sana wazazi mliopoteza watoto wenu.

Inapendeza zaidi watoto wasome kwenye shule za karibu ili wawe wanaenda shule kwa miguu.
Najua umejibana tu kumwaga hoja yako Ile ya msingi 😄😄
 
Hizi tour za kijinga ambazo watoto hupelekwa baada ya kufunga shule zimekuwa zikiambatana ajali za mara kwa mara na kupoteza maisha ya watoto..huku zikiacha wazazi na machungu mengi. Wazazi kataeni tour zote za hovyo hovyo na watoto warudi wapunzike nyumbani wanapofunga shule, kama ni tour wataenda kutalii na wazazi wao.
 
Back
Top Bottom