Manyara: Mtuhumiwa wa Ujangili akamatwa

Manyara: Mtuhumiwa wa Ujangili akamatwa

Bushmamy

JF-Expert Member
Joined
Aug 18, 2019
Posts
9,140
Reaction score
15,963

IMG-20230423-WA0030.jpg

Mtuhumiwa wa ujangili wa Twiga ambaye amekuwa akisakwa kwa muda mrefu na askari wa Wanyamapori katika hifadhi ya Jamii ya Wanyamapori Burunge, wilayani Babati mkoa Manyara Amos Benard Meja amekamatwa Jana usiku.

Mtuhumiwa huyo amekamatwa kutokana na mtego ulioandaliwa na askari wa Mamlaka ya Usimamizi Wanyamapori (TAWA), Askari wa Burunge WMA na askari wa Taasisi ya Chemchem association ambayo imewekeza shughuli za Utalii katika eneo hilo.

Meja ambaye amekuwa akisakwa kwa tuhuma za uwindaji wa Twiga na kuuza Nyama maeneo mbalimbali amekamatwa maeneo ya Mfulwang'ombe kwenye Kambi ya samaki.

Mtuhumiwa huyo ambaye haikuwa rahisi kutiwa nguvuni alikamatwa na kikosi cha askari maalum wa Wanyamapori James Misuka, Samweli Bayo, Khamis Chamkulu, Mohamed Abdallah, Pascal Mandao, Emmanuel Duxo, Wilfred Ngitoor na Karoli Umbe baada ya kupata taarifa kwa siri.

Mwendesha Mashitaka wa Mamlaka ya Usimamizi Wanyamapori (TAWA) Getrude Kariongi amekiri kukamatwa mtuhumiwa huyo.

"Ni kweli amekamatwa huyu mtuhumiwa alikuwa anakabiliwa na kesi kadhaa za ujangili na tayari amekabidhiwa polisi," amesema.

Screenshot_20230423-170902_Google.jpg
 
Bora angekuwa anawaua kina nani sijui? Wanyama wamemkosea nn😔
 
Hongera kwa Serikali kukamatwa kwa Jangiri huyo, ili kukomeshwa na kudhibiti Ujangiri ni muhimu kudhibiti mnyororo mzima wa matukio hayo.

Hivyo huyo mtuhumiwa abanwe aweze kuwataja washirika wake kwenye huo mtandao.
 
Hiv na wale twiga wanaopandaga ndege huwa wanauzwa au waña vibali vya kwenda kutalii!
 
Naamini atakua amekutwa na nyama tu, msala ukamuangukia.
... wanaitaga vipande vya nyama and most likely kabeba tu begani masalia yaliyoachwa na simba anasaidiana na fisi kusafisha mapori. Kwa muonekano tu choka mbaya huyo.
 

View attachment 2597246

Mtuhumiwa wa ujangili wa Twiga ambaye amekuwa akisakwa kwa muda mrefu na askari wa Wanyamapori katika hifadhi ya Jamii ya Wanyamapori Burunge, wilayani Babati mkoa Manyara Amos Benard Meja amekamatwa Jana usiku.

Mtuhumiwa huyo amekamatwa kutokana na mtego ulioandaliwa na askari wa Mamlaka ya Usimamizi Wanyamapori (TAWA), Askari wa Burunge WMA na askari wa Taasisi ya Chemchem association ambayo imewekeza shughuli za Utalii katika eneo hilo.

Meja ambaye amekuwa akisakwa kwa tuhuma za uwindaji wa Twiga na kuuza Nyama maeneo mbalimbali amekamatwa maeneo ya Mfulwang'ombe kwenye Kambi ya samaki.

Mtuhumiwa huyo ambaye haikuwa rahisi kutiwa nguvuni alikamatwa na kikosi cha askari maalum wa Wanyamapori James Misuka, Samweli Bayo, Khamis Chamkulu, Mohamed Abdallah, Pascal Mandao, Emmanuel Duxo, Wilfred Ngitoor na Karoli Umbe baada ya kupata taarifa kwa siri.

Mwendesha Mashitaka wa Mamlaka ya Usimamizi Wanyamapori (TAWA) Getrude Kariongi amekiri kukamatwa mtuhumiwa huyo.

"Ni kweli amekamatwa huyu mtuhumiwa alikuwa anakabiliwa na kesi kadhaa za ujangili na tayari amekabidhiwa polisi," amesema.

View attachment 2597247
Huyu jamaa kama siyo Rufiji dam? Tusubiri tuone kama atakuwepo jamvin.
 
Back
Top Bottom