General Mangi
JF-Expert Member
- Dec 21, 2013
- 15,303
- 23,064
Tutapewa katiba alafu mtakuja na mengiee, watanzania ni wavivu sana!!!
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mbweha kabisa wewe. Manyerere humfikii kwa namna yoyote. Kosoa hoja, siyo kuropoka.
chief Manyenyere. ulichosema hapo juu makes sense but kama kweli wewe ni mchambuzi mbobevu then unahitaji kujiongeza kidogo and have a critical look at the flip side as well.
je vipi akitokea "Kikwete" mwingine baada ya tenure ya Magufuli kwisha.... si tutarudi tena kule kule?
wengi tunaolilia katiba mpya tunataka upatatikanaji wa rais ya aina ya Magufuli uwe sustainable (japo 50 days in office ni mapema sana ku-judge, let me give Magufuli the benefit of the doubt for now na nikubaliane nawe kuwa in rais effective - I mean so far, so good...save for the Zanzibar bit!).
tunataka katiba ambayo inawapa uwezo wananchi kuchagua viongozi walio bora.
katiba ambayo (kwa kutumia mfano wako wa Kikwete) haitatuletea other "Vikwetes" at the helm!
katiba ambayo inamuwajibisha kiongozi anaposhindwa kutekeleza majukumu yake.
katiba ambayo inawapa wananchi uwezo wa kumuwajibisha kiongozi waliyemchagua, pale inapobidi.
in short, tunahitaji mfumo endelevu usiotegemea sura/roho nzuri au mbaya za watu wanaopewa dhamana ya uongozi.
chief Manyenyere, pamoja na sababu nyingine nyingi za why we need katiba mpya, in the context of your topic I think nilichoainisha hapo juu tells the whole story why we need it!
Mkuu, asante sana. Nimekutana na mjadala huu muda huu. Nimpongeze mleta mada. Ukisoma kwa makini, hutaona mahali ambako nimepinga ujio wa Katiba mpya. Nilichojaribu kueleza hapa ni kwamba Kumbe yapo mambo ambayo hata kabla ya ujio huo wa Katiba mpya, tunaweza kabisa kuyafanya. Ilivyo sasa ni kama vile watu wengi wanaamini kwa katiba mpya, kila kitu kitakwenda sawa-nadharia ambayo naipinga. Katiba mpya (kama ile iliyopendekezwa na Jaji Warioba, ukiacha vipengele vichache) ni muhimu. Hoja yangu ni kwamba tusibweteke kwa kuamini kuwa kuwashughulikia hawa mafisadi au vibaka, lazima kwanza tuwe na Katiba mpya. Nadhani wakati tukielekea kwenye hiyo Katiba mpya, yapo ambayo tunaweza kabisa kuyarekebisha. Ilivyo sasa ni kama vile wengi wanaamini kufeli kwa Kikwete kulisababishwa na Katiba mpya. Dhana hiyo ina ukweli mdogo sana. Kuwa na viongozi wenye maono na wenye kuipenda nchi yao ni jambo muhimu sana.
Hadhari yangu ni kuwa wananchi wasibweteke sasa kwa kuamini kuwa mwarobaini wa kero zao zote ni Katiba mpya. Kama nilivyosema, upya wa gari pekee si jibu la kukomesha ajali. Kuwa na sheria kali pekee si mwisho wa kukomesha ubakaji na makosa mengine. Muhimu kuliko yote hapa ni kwa wananchi wenyewe kujenga utamaduni wa kuheshimu hicho kilichopo. Mfano mdogo tu, hivi kipindupindu kinaweza kumalizwa kwa Katiba mpya? Ajali zitapunguzwa kwa Katiba mpya? Hofu yangu ni kwamba tunaweza kupata Katiba mpya, lakini wananchi wengi wakawa bado wenye kuwaza na kutenda vilevile walivyotenda kwenye Katiba ya mwaka 1977. Sijapinga Katiba mpya, isipokuwa Katiba hiyo pekee si suluhisho la matatizo yetu. Matatizo ya Watanzania (baaadhi) ni zaidi ya Katiba. Tuna matatizo ya Watanzania wengi kutoipenda Tanzania. Tuanze na la kujitambua ili hiyo Katiba mpya iwe na tija.