Maombi juu ya Corona: Kanuni za maombi ziko wazi - waombe msamaha uliowakosea ili maombi yako yasikilizwe, la sivyo unajisumbua bure!

Maombi juu ya Corona: Kanuni za maombi ziko wazi - waombe msamaha uliowakosea ili maombi yako yasikilizwe, la sivyo unajisumbua bure!

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
12,699
Reaction score
22,598
Nadhani wengi tunapenda kurahisisha sana suala la dini. Suala la kutaka taifa litoe maombi ili tuepuke ugonjwa wa Coronavirus ni nzuri - lakini je, mbona tunakuwa wepesi kusahau kanuni juu ya maombi?

Kanuni ziko wazi, ikiwa kama taifa tunataka mombi yetu yasikilizwe, basi kama taifa kwanza tunapaswa kuwaomba msamaha wale tuliowakosea - iwe ni katika masuala ya siasa, ya biashara, ya kuwanyima haki zao za kuishi, ya kuwanyima haki zao za binadamu, ya kuwanyima haki zao za kikatiba nk.

Ikiwa kama taifa tumefikia mahali, kwa sababu tu ya tofauti zetu za kisiasa tunauana, tunafungana jela kwa kuoneana, tunatekana, tunabambikiana kesi, nk, basi hatupaswi hata kudiriki kutoa wito wa kufanya maombi kabla hatujaomba msamaha juu ya dhambi zetu hizo nyekundu kama damu na wale tuliowakosea!

Tusipofanya hivyo, basi tutaomba hadi jasho la damu litutoke - na hatutasikilizwa! Tutabaki kuwa wafu tunaozika wafu wetu.
 
Nadhani wengi tunapenda kurahisisha sana suala la dini. Suala la kutaka taifa litoe maombi ili tuepuke ugonjwa wa Coronavirus ni nzuri - lakini je, mbona tunakuwa wepesi kusahau kanuni juu ya maombi?

Kanuni ziko wazi, ikiwa kama taifa tunataka mombi yetu yasikilizwe, basi kama taifa kwanza tunapaswa kuwaomba msamaha wale tuliowakosea - iwe ni katika masuala ya siasa, ya biashara, ya kuwanyima haki zao za kuishi, ya kuwanyima haki zao za binadamu, ya kuwanyima haki zao za kikatiba nk.

Ikiwa kama taifa tumefikia mahali, kwa sababu tu ya tofauti zetu za kisiasa tunauana, tunafungana jela kwa kuoneana, tunatekana, tunabambikiana kesi, nk, basi hatupaswi hata kudiriki kutoa wito wa kufanya maombi kabla hatujaomba msamaha juu ya dhambi zetu hizo nyekundu kama damu na wale tuliowakosea!

Tusipofanya hivyo, basi tutaomba hadi jasho la damu litutoke - na hatutasikilizwa! Tutabaki kuwa wafu tunaozika wafu wetu.
So dunia nzima iombe msamaha kwa tuliowakosea ikiwemo mimi na wewe kwani corona ipo duniani kote, sio ufipa tu
 
So dunia nzima iombe msamaha kwa tuliowakosea ikiwemo mimi na wewe kwani corona ipo duniani kote, sio ufipa tu
Huko kwingine hawajasema watapambana na Corona kwa maombi, wala usiwachokoze, wanajitambua!
 
  • Thanks
Reactions: prs
Hahahaha! Nawashangaa hawa viongozi wa dini wanaokimbilia kuitikia wito wa kutoa maombi kabla ya kulikumbusha taifa wajibu wa kuomba msamaha kwa tuliowakosea!

1587301193166.png
 
Hii hoja ni kama inaniingia hivi; tunamaswali hatujawahi kujibiwa
 
Nadhani wengi tunapenda kurahisisha sana suala la dini. Suala la kutaka taifa litoe maombi ili tuepuke ugonjwa wa Coronavirus ni nzuri - lakini je, mbona tunakuwa wepesi kusahau kanuni juu ya maombi?

Kanuni ziko wazi, ikiwa kama taifa tunataka mombi yetu yasikilizwe, basi kama taifa kwanza tunapaswa kuwaomba msamaha wale tuliowakosea - iwe ni katika masuala ya siasa, ya biashara, ya kuwanyima haki zao za kuishi, ya kuwanyima haki zao za binadamu, ya kuwanyima haki zao za kikatiba nk.

Ikiwa kama taifa tumefikia mahali, kwa sababu tu ya tofauti zetu za kisiasa tunauana, tunafungana jela kwa kuoneana, tunatekana, tunabambikiana kesi, nk, basi hatupaswi hata kudiriki kutoa wito wa kufanya maombi kabla hatujaomba msamaha juu ya dhambi zetu hizo nyekundu kama damu na wale tuliowakosea!

Tusipofanya hivyo, basi tutaomba hadi jasho la damu litutoke - na hatutasikilizwa! Tutabaki kuwa wafu tunaozika wafu wetu.
Aliyetoa agizo la maombi ni mnafki kupindukia. Sijui atamuomba lini msamaha Tundu
 
Nadhani wengi tunapenda kurahisisha sana suala la dini. Suala la kutaka taifa litoe maombi ili tuepuke ugonjwa wa Coronavirus ni nzuri - lakini je, mbona tunakuwa wepesi kusahau kanuni juu ya maombi?

Kanuni ziko wazi, ikiwa kama taifa tunataka mombi yetu yasikilizwe, basi kama taifa kwanza tunapaswa kuwaomba msamaha wale tuliowakosea - iwe ni katika masuala ya siasa, ya biashara, ya kuwanyima haki zao za kuishi, ya kuwanyima haki zao za binadamu, ya kuwanyima haki zao za kikatiba nk.

Ikiwa kama taifa tumefikia mahali, kwa sababu tu ya tofauti zetu za kisiasa tunauana, tunafungana jela kwa kuoneana, tunatekana, tunabambikiana kesi, nk, basi hatupaswi hata kudiriki kutoa wito wa kufanya maombi kabla hatujaomba msamaha juu ya dhambi zetu hizo nyekundu kama damu na wale tuliowakosea!

Tusipofanya hivyo, basi tutaomba hadi jasho la damu litutoke - na hatutasikilizwa! Tutabaki kuwa wafu tunaozika wafu wetu.

Uko sahihi

Ndiyo maana zimetengwa siku tatu za maombi

Toba ama kutubu makosa yako na ya watu wengine ni sehemu ya maombi yako.

Kama kweli wewe ni muumini safi na wa kweli wa Kikristo unajua Yesu Kristo alifanya nini

Alisulubiwa kwa sababu ya dhambi zetu, alionewa badala yetu, alidhihakiwa badala ya watu wa ulimwengu wote, alitemewa mate na mpaka kufa kwa sababu yetu. Alibeba makosa yetu kwani misumari ile aliyogongomelewa pale msalabani kiuhalisia kila mmoja wetu ndiye aliyepaswa kutundikwa kwenye ule msalaba na kugongomewa misumari kama adhabu na malipo ya dhambi ya kila mmoja!!

Tunapaswa kuwa kama Yesu Kristo. Tujifunze kusamehe wengine waliotukosea.

Tujifunze kubeba adhabu ya makosa ya wengine na kuyapeleka msalabani pa Yesu Kristo

Tusijihesabie haki kwa kusema "yule ndiye mwenye dhambi, mimi sina dhambi" na hivyo sistahili kuomba lolote.

Fikra za namna hii ni ishara ya uwepo wa moyo wa kiburi ndani ya mtu wa namna hii!!

Twendeni tuendelee kuliombea taifa letu. Waombee Rais, Makamu wa Rais, PM, Baraza la mawaziri, Makatibu wakuu, vyama vya siasa vyote, wakuu wa mihimili yote ya dola (serikali kuu, Mahakama, Binge), RCs, DCs viongozi wa tarafa, kata, vijiji, mitaa ama vitongoji na mtu mmoja mmoja

Hata RC mtata zaidi hapa Tanzania ndugu Makonda (DSM) naye usisite kumwombea. Huna namna ya kukwepa, huyo ndiye kiongozi wako. Dhambi zake yeye siyo jukumu lako. Yupo aliyemuumba na kumuweka katika nafasi hiyo, huyo ndiyo mlipa mshahara kwa yeyote atendaye dhambi. Hukumu iko mikononi make. Sisi hatuhukumu, tunaomba neema na rehema kwao!!

Omba kwa kutubu dhambi zao. Simama mahali pao we we. Sema; Mungu tumekutenda dhambi, tumekukasirisha na hata kustahili adhabu na hukumu yako. Mwambie Mungu, tunaona aibu hata kukutazama usoni mwako kwa sababu ya dhambi zetu za kuabudu sanamu, uzinzi, uasherati, kuua, kutukana nk no

Tukiwa hivi, tutaiona Rehema na Neema ya Bwana juu yetu na nchi yetu. Hii ndiyo maana ya andiko 2 Mambo ya Nyakati 7:14 linaongoza maombi haya siku tatu ya kitaifa ili taifa letu lipate kuponywa na kuepushwa na tauni hii!!
 
Swala la kutubu lipo, na lina sehemu ya personal na sehemu ya public. Na ni kweli toba inachukua sehemu kubwa sana ya maombi. Ubinadamu umetoweka, tunachukiana na kuuana. Tumepotoka sana, na inatupasa kumrudia mwenyenzi Mungu kwa TOBA. Hoja yako ni ya msingi, na nafikiri hata hapa tulipofikia ni pazuri, wengi wetu tunatubu personally, hopefully Mungu atatuelekeza kuwa kutubu publically pia, huko tuendako!!
 
Sikupoteza muda wangu kuungana na wauaji kuliombea taifa. Wanaodhulumu haki ya kuishi ya watz wasio na hatia watubu kwanza
 
Sikupoteza muda wangu kuungana na wauaji kuliombea taifa. Wanaodhulumu haki ya kuishi ya watz wasio na hatia watubu kwanza

Nakushauri uikatae kabisa roho hiyo, itakupoteza na kukuangamiza

Beba roho ya kuachilia na kusamehe.

Usijihesabie haki na kuwahukumu wengine

Jukumu na kuiona dhambi ya mtu na kisha kuihukumu dhambi hiyo ni la Mungu mwenyewe.

Sisi hebu tuombeane Rehema na Neema iliyo katika Kristo Yesu

Hebu jiulize swali hili; Yesu Kristo alikuwa na kosa gani hata kuteswa, kusulubiwa msalabani na hatimaye kufa na baadaye kufufuka na leo yuko hai?

Jibu: Obviously, hakuwa na kosa. Isipokuwa alijitolea kufa kwa ajili ya makosa (dhambi) za ulimwengu (watu) wote na kuanzia hapo tumekuwa huru na dhambi.

Yeye ndiye nguvu pekee ya kuishinda dhambi ambayo ndiyo huzaa mauti. Ukimkubali yeye na kumkiri kuwa alikufa na kufufuka kwa ajili yako, utaokoka!!

Tuwe na upendo kama ule wa Yesu Kristo. Tuwapende waliotukosea, tuwaombee na kamwe tusiwahukumu!!
 
What if Covid-19 returns annually, like the common cold?
 
Kwa hiyo Italy hawasali? Wanajitambua?? Spain UK, who
Aliyekuambia Italy, Spain, UK kama taifa wana mambo ya kuomba msamaha kuhusu kunyima watu haki za kuishi ni nani?

Kuna watu mnakurupuka na ni wazi mnajibu thread bila ya kuzisoma.
 
Nakushauri uikatae kabisa roho hiyo, itakupoteza na kukuangamiza

Beba roho ya kuachilia na kusamehe.

Usijihesabie haki na kuwahukumu wengine

Sawa, lakini kukubali kuongozwa katika mambo ya kiroho na watu ambao unajua kabisa wana mapungufu makubwa na hatia dhidi ya wengine ni upinguani fulani hivi.

Je wewe unaweza kukubali kahaba ndio awe anakuelekeza ni wakati gani wa kuomba na ukawa unafuata kama mwanakondoo kwa kuwa tu huwezi kuhukumu watu?
 
Back
Top Bottom