Maombi na ushauri kwa TFF na Wadau wote wa soka kwa pamoja

Maombi na ushauri kwa TFF na Wadau wote wa soka kwa pamoja

mazaga one

JF-Expert Member
Joined
Apr 16, 2015
Posts
2,514
Reaction score
4,042
Nimekaa nimewaza sana. Hivi sisi Watanzania kuna wachezaji wengi wa kutoka nchi za nje wanakuja kucheza huku kwetu, na wengineo wana viwango vizuri tu ila timu zao za Taifa wanakotoka hawapati nafasi.

Je, sisi Watanzania kupitia TFF hatuwezi kuona hii ni fursa ya sisi kuanza kuwashauri baadhi ya wachezaji kubadili Uraia wao na Kuwa Watanzania na kuanza kuwatumia kwenye Timu yetu ya Taifa Stars kama ambapo Mataifa mengine yanafanya kwa Wachezaji wanaocheza kwenye vilabu vya nchi zao.

Tuseme ukweli Kocha Ndayiragije tukimpa muda tutafika mbali nadhani tu tutafute na wachambuzi wa Soka kadhaa hasa Hawa waandishi wa habari wawe ni watu wa Karibu na benchi Letu la Ufundi. Sasa Timu inacheza na unategemea kabisa matokeo yatapatikana.

Nawasilisha.
 
Timu yetu ya taifa ina mda mchache sana wa kukaa pamoja , ni heri kuwe na timu ya taifa ambayo wachezaji hawatoki kwenye vilabu, wanakaa pamoja mda wote ,sasa mechi kubwa kama hizi na Tunisia wachezaji hawajakaa pamoja hata week moja
 
Timu yetu ya taifa ina mda mchache sana wa kukaa pamoja , ni heri kuwe na timu ya taifa ambayo wachezaji hawatoki kwenye vilabu, wanakaa pamoja mda wote ,sasa mechi kubwa kama hizi na Tunisia wachezaji hawajakaa pamoja hata week moja
Fikiria mchezaji hatoki kwenye klabu na hajawahi pitia shule za mpira, unategemea huyo mchezaji anafaa kuwa timu ya taifa? Mchezaji mpira ni zaidi ya kujua control na chenga..Mchezaji anapaswa pia awe na stamina, umakini , nidhamu, kujua mifumo (formations) n.k na hivyo vyote vinafundishwa akiwa klabuni au shule za mpira.
 
Ligi yetu ni mbovu kwa hiyo mgeni anaewika hapa hawezi kutusogeza popote tukimchukua. Kiufupi wanastahili kutoitwa kwenye timu za mataifa yaliyopiga hatua kwenye soka. Na ni kweli kwamba mataifa yanayoita wachezaji kutoka ligi yetu ni yale yanayojikongoja kisoka.
 
Back
Top Bottom