Maombi ya Wazazi wako hayana mchango wowote katika mafanikio yako. Matendo yao Mema ndio sadaka kwa mafanikio yako

Maombi ya Wazazi wako hayana mchango wowote katika mafanikio yako. Matendo yao Mema ndio sadaka kwa mafanikio yako

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
28,297
Reaction score
68,017
MAOMBI YA WAZAZI WAKO HAYANA MCHANGO WOWOTE KATIKA MAFANIKIO YAKO. MATENDO YAO MEMA NDIO SADAKA KWA MAFANIKIO YAKO.

Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli

Hata waombe na kubinuka. Hata wafunge 40 kama Yesu. Hata wafunge Ramadhan na Shaban.
Hata wagaregare na Kuvaa magunia. Ni Kazi bure tuu.

Maombi hayanaga Ñguvu yoyote kama matendo ya muombaji ni maovu, machafu na Ufuska Mtupu.

Oooh! Nakuombea mwanangu. Ooh! Acha nimwombee mwanangu. Oooh! Wazazi wàngu waliniombea.

Sikiliza; Wewe Mzazi kama unajijua Kabisa umchawi, muasherati, tapeli na dhulmati, Mshenzi, yàani Kwa ujumla wewe ni muovu. Ni Bora tuu uache kuwaombea Watoto wako. Maana unawatia tuu nuksi na Mikosi yako.

Huwezi kuwa Baba mchepukaji unayemsaliti Mkeo, Mama wa Watoto wako alafu ati jioni unaombea Watoto wako. Unawaombea au unawasagia kunguni.

Huwezi kuwa Mama na mke alafu ni unam-cheat Mumeo alafu ukirudi nyumbani unajifanya Mama wa Maombi alafu unawaambia Watoto wako unawaombea Maisha yenye mafanikio. Hivi wewe unaakili kweli Sawasawa?

Kama Mimi ndiye Mtoto wako nitakuambia sitaki Maombi yako. Sitaki Baraka zako. Sitaki uniombee Mimi.

Watoto wàngu, Ikiwa Mimi Baba Yenu, ndiye Mtibeli halisi ni muovu, ninafanya uovu íwe Kwa Siri au Kwa ninyi kujua. Msitake niwaombee. Msitake Baraka zangu. Sitakuwa na Baraka zaidi ya Laana wanangu. Huyo ninayemuomba hatanisikiliza. Nitakuwa nawasagia kunguni tuu.

Mwombeni Mungu ninyi wènyewe. Tenà muambieni kuwa kama Mimi Baba Yenu ninawaombeaga ninyi lolote asinisikilize. Maana kimsingi hatanisikiliza zaidi atawachapa ninyi Kwa Hasira.

Iko hivi, Hata kwèñye mahusiano ya kawaidà, Huwezi kumwomba Adui yako msaada. Ni Sawa úwe na ugomvi na Rais wa nchi alafu Muda huohuo unamwomba msaada akusaidie Watoto wako. Hivi unaakili Sawasawa kwèli?

Taikon mwisho namaliza Kwa kusema, Sisi kama Wazazi tunaowajibu wa kimatendo zaidi Kwa Watoto wetu kuliko wajibu wa kimaombi.

Unàtaka Mtoto wako afanikiwe, Maombi hayasaidii kitu.
MATENDO yako, Kuanzia Mtoto akiwa mdogo mtengenezee Mtoto mazîngira ya kufanikiwa. Mpe Elimu na ujuzi, mfundishe stadi za Maisha, mfundishe tàbia Njema, mfundishe mahusiano mazuri na Watu, mazîngira na mûda.

Muwekee Mtoto vitega uchumi, muandalie Urithi Mtoto. Hapo Mtoto lazima atoboe Kwa sababu wewe kama Mzazi umewajibika kimatendo.

Siô unamuombea, unamuombea nini? Unamuombea Mtoto apate Laana zako siô.

Kumuombea Mtoto au Watoto wako alafu unamatabia ya hovyo ni kuhamisha ugomvi Kutoka kwako kwenda Kwa Watoto.

Sio ajabu wewe kîla Siku unawaambia Watoto wako unawaombea lakini Kila uchwao Hali inazidi kuwa mbaya.
Au Wazazi wako wanakuombea lakini kîla Siku afadhali ya Jana.
Mzazi Mchawi atakuombea nini bhana? Ati Mimi Mzazi Mchawi ati nimwombee Mtoto wàngu hivi ataswii kweli Kwa Akili za Kawaida?

Kama unàtaka Mtoto afaulu Shule Kanuni zinajulikana na Mungu Alishaziweka bayana. Tafuta Shule nzuri, Zenye waalimu wazuri na mazîngira ràfiki ya kujifunza. Shule yenye maadili Kisha peleka Mtoto. Lazima Mtoto Afanye Vizuri. Huna haja ya kuomba.

Huwezi kuomba kwèñye Jambo ambalo ni Wajibu wako kulifanya.

Ninajaribu kusema, wewe kama Mzazi unajijua Kabisa umchafu, Mikono yako, midomo yako, Roho yako ni chafu Kamwe Huwezi kumwombea Mtoto wako awe msafi . Never ever!

Huwezi kuogesha Mtoto ukiwa na Mikono michafu utamchafua tuu.
Safisha Mikono yako, Roho yako, midomo yako ñdipo umwombee Mtoto wako.

NI akheri kama unajijua ni mchafu uachane na mambo ya kuombea Watoto muachie Kazi hiyo Mkeo kama yeye ni Msafi au muachie Mumeo kama yeye NI Msafi.
Kama wôte ni wachafu Basi tafuteni Mtu mnayemwona ni mtumishi wa Mungu awafanyie Kazi hiyo.

Mumpe SADAKA, aitakase Kisha yeye awe kama Wakil wenu kuwaombea Watoto wenu badala Yenu.

Mimi Taikon Acha nipumzike sasa. Kama hujanielewa siô lazima.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa Sasa Dar es salaam
 
Kwa ufipi unamanisha walifanikiwa wote ni kwasababu ya wema wao, sio dua za wazazi imamu mchungaji au kutoa kafara zao, wizi ufisadi au Yesu......

Sisi waislamu tunaamini utajiri sio jitihada zako tu kuna kadari za Allah, pia some time mtu mbaya anaweźa akapewa mali ikawa kama mtihani kwa waumini wengine.....kwa hali yoyote sisi tuna sema allahamudullillahi nima amuzi ya Mola wetu.
 
Kwa ufipi unamanisha walifanikiwa wote ni kwasababu ya wema wao, sio dua za wazazi imamu mchungaji au kutoa kafara zao, wizi ufisadi au Yesu......

Sisi waislamu tunaamini utajiri sio jitihada zako tu kuna kadari za Allah, pia some time mtu mbaya anaweźa akapewa mali ikawa kama mtihani kwa waumini wengine.....kwa hali yoyote sisi tuna sema allahamudullillahi nima amuzi ya Mola wetu.

Upo Sahihi pia
 
Kwa ufipi unamanisha walifanikiwa wote ni kwasababu ya wema wao, sio dua za wazazi imamu mchungaji au kutoa kafara zao, wizi ufisadi au Yesu......

Sisi waislamu tunaamini utajiri sio jitihada zako tu kuna kadari za Allah, pia some time mtu mbaya anaweźa akapewa mali ikawa kama mtihani kwa waumini wengine.....kwa hali yoyote sisi tuna sema allahamudullillahi nima amuzi ya Mola wetu.
Hoja yako ni nzuri na nimeipenda pia.
 
Ninapingana na hili mimi ni shuhuda wa maombi ya mzazi wangu kunifikisha hapa nilipo.Na katika kuombea atakuambia nimeona moja mbili tatu na ukienda sehemu husika unakuta kama alivyosema.Maombi ya wazazi ni muhimu na matendo mema ni muhimu sana
 
Napinga ,Maombi pia ni muhimu .... Yaani sitaki kusema Maneno mengi ila Maombi ni muhimu na yanatakiwa kuwa na mwendelezo kutoka kwa mzazi mpaka mtoto Hadi vizazi
 
Back
Top Bottom