Maonesho ya Biashara ya Sabasaba Dar es Salaam 2017

Emc2

JF-Expert Member
Joined
Sep 26, 2011
Posts
16,808
Reaction score
16,887
Nitakuwa nawaletea maonesho haya makubwa sana Africa Mashariki na Kati.

Ufunguzi ni tarehe 01/07/2017. Yatafunguliwa na rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Mh. John Pombe Magufuli. Ni zaidi ya nchi 33 zimethibitisha kuwepo hapo.

Kwa hiyo wapenzi wa Africa mashariki ni fursa kubwa kutangaza biashara zetu.
Tanzania moja, Africa mashariki moja, Na Africa ni moja.

Tanzania inapaa sana.
 
Maonesho yanafanyika Dar es salaam uwanja wa maonesho wa Nyerere maarufu kwa jina la viwanja vya sabasaba. Vimetajwa kuwa maonesho ya sabasaba kwa sababu ki utamaduni yalikuwa yakifanyika 07/07.

CCTV camera zimefungwa kila corner. Kwa hiyo ulinzi ni mkubwa. Haya maonesho ya sabasaba yanatambulika kimataifa na yamepata certificate ya kuwa maonesho bora Africa Mashariki na kati.

Zaidi ya makampuni 2500 yatakuwepo kwenye maonsho hayo.
 
Haya haya, nas tutajumuika pamoja kama kawaida kupata bei cheeeee
 
Maandalizi yanaendelea kwama kawaida.



CRDB Wanawakaribisha kwenye maonesho

 

Na: Mwandishi Wetu-MAELEZO
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, anatarajiwa kufungua Maonesho ya 41 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam maarufu kama Sababsaba Julai Mosi mwaka huu.
Kwa mujibu wa taarifa kwa Vyombo vya Habari iliyotolewa na Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage, Rais atafanya ufunguzi huo katika Uwanja wa Maonesho wa Mwalimu Julius Nyerere, Barabara ya Kilwa Jijini Dar es Slaam.
Waziri Mwijage ameeleza katika taarifa hiyo kuwa lengo la maonesho ni kutoa fursa kwa wafanyabiashara wa ndani na nje ya nchi, pamoja na taasisi mbalimbali kutangaza biashara na huduma, kutoa fursa kwa wafanyabisashara wa ndani kujifunza mambo ya biashara na uzalishaji bora wa bidhaa kulingana na soko la kimataifa, kutengeneza mitandao ya mawasiliano baina yao ambayo itasaidia kukuza biashara na kufikia malengo waliyojiwekeka na pia kutoa fursa ya kuuza bidhaa.
“Maonesho haya yanabeba kauli mbiu isemayo Ukuzaji wa Biasha kwa Maendeleo ya Viwanda,inanalenga kutumia Maonesho haya kama jukwaa la kutangaza biashara na huduma mbalimbali kwa ajili ya ukuzaji wa sekta ya viwanda, ikizingatiwa kuwa Serikali ya Awamu ya Tano inaweka mkazo mkubwa katika kuendeleza uchumi wa viwada hapa nchini”, anaeleza taarifa ya Waziri.
Aidha Maonesho ya mwaka huu yatatoa fursa kwa wenye viwanda vidogo, vya kati na vikubwa kukutana na wanunuzi wa bidhaa zao na kutakuwa na kampeni maalum ya kuhamasisha wananchi kupenda na kutumia bidhaa zinazozalishwa hapa nchini.
“Napenda kuwafahamisha kuwa Tan Trade kwa kushirikiana na washirika wake kwa mara ya kwanza imeandaa Siku ya ‘Afrika Mashariki’ ambayo itaadhimishwa tarehe 6 Julai, 2017. Lengo la siku hii ni kuimarisha biashara katika nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki. Kama inavyojulikana nchi hizi zimejaliwa kuwa na rasilimali nyingi hali ambayo itatoa fursa nzuri katika maendeleo ya kiuchumi katika nchi hizo ili kuwe na uchumi endelevu”, ilieleza taarifa hiyo.
Katika maonesho hayo, Waziri anaeleza kuwa Tan Trade imeandaa eneo maalum litakalojulikana kwa jina la ‘Banda la Tanzania’ kwa ajili ya wazalishaji wa bidhaa mbalimbali zinazotengenzezwa ndani ya nchi na ‘Banda la Asali’ kwa ajili ya kukuza bidhaa za nyuki na pia kutakuwa na eneo maalum la wazalishaji wa bidhaa za ngozi ambalo washiriki wake watapata fursa ya kuonesha bidhaa bora za ngozi kwa ajili ya kuvutia wananchi wengi kupenda bidhaa zinazozalishwa hapa nchini.
Katika kuimarisha huhusiano wa kibishara na kuwakutanisha wafanyabiashara wa Kitanzania na wenzao kutoka nje ya nchi, kutakuwa na banda maalum kwa ajili ya mikutano ya kibiashara yaani Business to Business (B2B) na pia banda maalum litakalotumika kwa utoaji wa mafunzo ya kibiashara.
Hadi sasa washiriki zaidi ya 2500 kutoka ndani na nje ya Afrika wamethibitisha kushiriki Maonesho ya mwaka huu. Nchi zitakazoshiriki ni Burundi, China, Comoro, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Misri, Ujerumani, Ghana, India, Indonesia, Iran, Italia, Japan, Kenya, Malawi na Mauritius.
Nchi zingine ni pamoja na Morocco, Msumbiji, Namibia, Pakistani, Rwanda, Singapore, Afrika Kusini, Sudani Kusini, Syria, Uturuki, Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE), Uganda, Marekani, Uingereza na Vietnam.

http://www.matukiodaima.co.tz/2017/06/rais-magufuli-kufungua-maonyesho-ya.html
 
Maonyesho ya Sabasaba kuja kivingine



Dar es Salaam. Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) imejipanga kufanya mabadiliko kwenye maonyesho ya kimataifa ya biashara (Sabasaba) kwa mwaka huu ikiwa ni pamoja na kutumia vitambulisho vya washiriki kwa mfumo wa kieletroniki.

Pia, wakati wa maonyesho hayo ya 41, kutakuwa na siku ya Afrika Mashariki ambapo washiriki kutoka nchi wanachama watakutana na kubadilishana uzoefu juu ya uzalishaji bidhaa pamoja na siku ya kuonja asali ambapo washiriki wanaofanya biashara ya asali watawaonjesha wateja wao.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TanTrade, Edwin Rutageruka amesema wamefanya maboresho hayo kutokana na ushindani uliopo kwenye biashara.

“Tumeamua kujipanga na yapo mambo mengi tuliyoyafanyia marekebisho. Kuanzia vitambulisho vya washiriki ambapo mfumo unaotumika ni wa kielektroniki hadi utaratibu wa watazamaji kuingia kwenye maonyesho, hakutakuwa na foleni ndefu na hata ukataji tiketi utakuwa wa haraka,” amesema Rutageruka na kuongeza.

“Tutakuwa na mikutano ya mara kwa mara kati ya wafanyabiashara, watabadilishana uzoefu na mshiriki atakayefanikiwa kumshawishi mwenzake hadi akapata mkataba wa kufanya naye biashara na atasaini makubaliano hayo mbele ya mgeni rasmi siku ya kufunga maonyesho ili ulimwengu mzima uone.”

Maonyesho ya Sabasaba kuja kivingine
 
Hii upuzi haiusu Kenya in anyway
Tulia dogo hapa tunaongelea maendeleo ya Africa Mashariki. Africa Mashariki ni pamoja na Kenya na Tanzania.
Naona umevimba unataka kupasuka. This is Tanzania my friend. Usisikie ya kuambiwa njoo sabasaba ujionee mwenyewe.
Hii ni International exhibitions ndugu. Itabidi upoe tu.
 
Niwe mkweli
Maonesho ya 77 huwa si maonesho bali uuzaji wa bidhaa

Waliotembea kwenye maonesho makubwa duniani wataelewa hili
Hatua kwa hatua tutawafikia wale wa duniani.
 
Kiwanda cha kuunganisha Matrekta Tanzania

 
Nataka nikanunue asali nyingi sana, nadhan maliasili TAWIRI watakuepo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…